Manyoni: Wasiojulikana wafukua kaburi na kuondoka na mwili wa mtoto

lwambof07

JF-Expert Member
Jul 12, 2016
4,593
5,203
Mwili wa mtoto Christian Samson (1), aliyezikwaa siku ya Jumapili katika makaburi ya kitongoji cha Kipondoda wilayani Manyoni mkoani Singida, umefukuliwa na kuchukuliwa na watu wasiojulikana licha ya ndugu kuutafuta bila mafanikio.

Simanzi na huzuni zilitawala katika makaburi hayo hii ikiwa sio mara ya kwanza vitendo hivyo vya ufukuaji wa makaburi kujitokeza, na mara hii imejitokeza hali isiyokuwa ya kawaida kwa kuwa mwili marehemu umetafutwa kwa zaidi ya saa manne huku jitihada hizo zikishindikana.

Kufuatia hali hiyo imemlazimu Mkuu wa wilaya ya Rahabu Mwagisa, na kuzungumzia vitendo hivyo huku akisisitiza suala la maombi kuwa ni la muhimu na jeshi la polisi linafuatilia ili kuwabaini waliohusika na kitendo hicho.

Screenshot_20220119_105816.jpg
 
Back
Top Bottom