Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,798
- 71,218
Kumbe ndio maana siku hizi kamisheni za maafisa wa Jeshi zinatolewa nje ya kambi zao ili kuwapa nafasi wanasiasa kuongea utumbo wao ambao wasingeweza kuusema pale TMA Monduli maana sio mahali pa siasa.
RC wa Arusha alipopewa nafasi ya kutambulisha wageni akatumia nafasi hiyo kuingiza ujinga wa siasa kwa kusema "hizi unazoziona mheshimiwa rais ni rasharasha, mvua yenyewe ni 2020" kisha akawageukia wananchi "watatuwezaaa!"
Sura za makamanda wa Jeshi jukwaani zilionyesha kukereka na kushangaa! Kwenye shughuli kubwa za kijeshi huwa hakuna mambo ya "vyama" lakini amiri mkuu anaonyesha halielewi hilo.
Je haelewi kwa sababu zile alizosema Zitto? Ushamba na uzumbukuku au kuna kingine!
RC wa Arusha alipopewa nafasi ya kutambulisha wageni akatumia nafasi hiyo kuingiza ujinga wa siasa kwa kusema "hizi unazoziona mheshimiwa rais ni rasharasha, mvua yenyewe ni 2020" kisha akawageukia wananchi "watatuwezaaa!"
Sura za makamanda wa Jeshi jukwaani zilionyesha kukereka na kushangaa! Kwenye shughuli kubwa za kijeshi huwa hakuna mambo ya "vyama" lakini amiri mkuu anaonyesha halielewi hilo.
Je haelewi kwa sababu zile alizosema Zitto? Ushamba na uzumbukuku au kuna kingine!