Manara Amepata Hukumu Kubwa Kutokana na Makosa ya Kujirudiarudia

nyehura

Member
Jun 4, 2022
6
15
Haji Manara alifungiwa mwaka 1 na faini ya shilingi Milioni 9 mwezi April 2017 baada ya kukutwa na Makosa 3 ambayo yaliwekwa wazi na Kamati ya Maadili ya TFF.

1) Kuituhumu na Kuidhalilisha TFF na Viongozi wake kwa kutoa maneno yasiyo na Staha.
2) Kueneza Chuki za Ukabila. 3) Kuingilia Utendaji wa TFF.

Kosa la kwanza alihukumiwa kwa mujibu wa kanuni 41 Kifungu cha 9 ambapo alihukumiwa kulipa milioni 1. Kosa la pili alihukumiwa kwa kanuni ya 53 kifungu cha 1 & 2.

Kutokana na kifungu hicho, alihukumiwa kifungo cha miezi 3 na faina ya shilingi milioni 3. Kosa la tatu alihukumiwa kwa kanuni ya 1 & 2 inayohusu Maadili ya TFF.

Haji alitakiwa ahukumiwe kifungo cha miaka 7 na faini ya Milioni 5 kutokana na kukutwa na hatia kwenye kosa lake la 3 la Kuingilia Utendaji wa TFF.

Ila kutokana na kwamba hayo yalikuwa makosa yake ya mara ya kwanza, Kamati ilitumia mamlaka yake kwa kumpunguzia adhabu hadi miezi 12 na faini ya milioni 5.

Adhabu hizo ziliunganishwa , hivyo alitakiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja na kulipa faini ya shilingi milioni 9 Lakini Uongozi wa Karia ulimsamehe adhabu hizo zote.

Septemba 2020, Haji alitozwa faini ya shilingi milioni 5 baada ya kukutwa na kosa la kuingilia majukumu ya Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi ya Wachezaji.

Haji alipewa na onyo la kukaa miaka 2 bila kufanya kosa lolote la kimaadili. Julai 2022 Haji alikutwa na hatia kwa makosa mawili 1) Kumtishia 2) kumdhalilisha Rais wa TFF.

Katibu wa Kamati ya Maadili ya TFF, Walter Lungu amesema Haji alimwambia Rais wa TFF, Wallace Karia "Niondolee Upuuzi wako" Aisee ni makosa sana.

Pia alimwambia Rais Karia "Unanifuata fuata sana na hii ni mara ya 3, sikuogopi kwa lolote na nina uwezo wa kukufanya lolote na huna uwezo wa kunifanya lolote".

This time amefungiwa miaka 2 kutojihusisha na soka ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na faini ya milioni 20.
 
Kila la kheri timu ya Soka la Taifa la Somalia kwenye mechi yake ya leo na KARIA FC!
 
Hajji akidekezwa sana na wazazi udogoni , hadi ukubwani bado jamii imdekeze tu?
Eti, kumbe kuna watu hawaruhusiwi kuguswa, ila wakifungiwa wengine sawaa!!!!!! Huo ndiyo mpira wa nchi hii ulipofikia.
Huyu akitolewa kifungoni mwake; wengine nao wafanye yao watolewe. Hakuna jinsi,
kama mbwai na iwe mbwai.
 
Jamaa ni mshamba Sana. Kipindi anaanzia kazi ya usemaji wa Simba nilikuwa namkubali Ila kadri siku zilivyokuwa zinaenda nimegundua jamaa ni matatizo Sana.

Huwezi kumsema mtu mwenye hadhi ya Karia maneno hayo Tena hadharani, mbele za watu.

Aisee!!! Alimkosea heshima mno. Mpira ni mchezo wa kiungwana, Ni mchezo wa watu waliostaarabika.

Jamaa naona siku hizi sifa zimemzidia, anajiamini mno sababu anajiona yupo karibu na GSM siku hizi.

Ana zile tabia za mswahili aliye karibu na tajiri, kudharau watu wengine walio juu yake akidhani kwa kuwa karibu na tajiri kila anachofanya atasupportiwa ni Tatizo la muda Tu, Soon GSM atamchoka.
 
Haji Manara alifungiwa mwaka 1 na faini ya shilingi Milioni 9 mwezi April 2017 baada ya kukutwa na Makosa 3 ambayo yaliwekwa wazi na Kamati ya Maadili ya TFF.

1) Kuituhumu na Kuidhalilisha TFF na Viongozi wake kwa kutoa maneno yasiyo na Staha.
2) Kueneza Chuki za Ukabila. 3) Kuingilia Utendaji wa TFF.

Kosa la kwanza alihukumiwa kwa mujibu wa kanuni 41 Kifungu cha 9 ambapo alihukumiwa kulipa milioni 1. Kosa la pili alihukumiwa kwa kanuni ya 53 kifungu cha 1 & 2.

Kutokana na kifungu hicho, alihukumiwa kifungo cha miezi 3 na faina ya shilingi milioni 3. Kosa la tatu alihukumiwa kwa kanuni ya 1 & 2 inayohusu Maadili ya TFF.

Haji alitakiwa ahukumiwe kifungo cha miaka 7 na faini ya Milioni 5 kutokana na kukutwa na hatia kwenye kosa lake la 3 la Kuingilia Utendaji wa TFF.

Ila kutokana na kwamba hayo yalikuwa makosa yake ya mara ya kwanza, Kamati ilitumia mamlaka yake kwa kumpunguzia adhabu hadi miezi 12 na faini ya milioni 5.

Adhabu hizo ziliunganishwa , hivyo alitakiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja na kulipa faini ya shilingi milioni 9 Lakini Uongozi wa Karia ulimsamehe adhabu hizo zote.

Septemba 2020, Haji alitozwa faini ya shilingi milioni 5 baada ya kukutwa na kosa la kuingilia majukumu ya Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi ya Wachezaji.

Haji alipewa na onyo la kukaa miaka 2 bila kufanya kosa lolote la kimaadili. Julai 2022 Haji alikutwa na hatia kwa makosa mawili 1) Kumtishia 2) kumdhalilisha Rais wa TFF.

Katibu wa Kamati ya Maadili ya TFF, Walter Lungu amesema Haji alimwambia Rais wa TFF, Wallace Karia "Niondolee Upuuzi wako" Aisee ni makosa sana.

Pia alimwambia Rais Karia "Unanifuata fuata sana na hii ni mara ya 3, sikuogopi kwa lolote na nina uwezo wa kukufanya lolote na huna uwezo wa kunifanya lolote".

This time amefungiwa miaka 2 kutojihusisha na soka ndani na nje ya mipaka ya Tanzania na faini ya milioni 20.
Hii adhabu ni ndogo sana huyu alitakiwa afungiwe miaka kumi bila faini. Faini haimuumi kwa vile wapo wapumbavu wenzake watamlipia hivyo hawezi kujutia hilo kosa na kamwe hawezi kujirekebisha. Huyu adhabu inayomfaa ni ya yeye mwenyewe kuibeba na adhabu hiyo ni kumfungia.
 
Jamaa ni mshamba Sana. Kipindi anaanzia kazi ya usemaji wa Simba nilikuwa namkubali Ila kadri siku zilivyokuwa zinaenda nimegundua jamaa ni matatizo Sana.

Huwezi kumsema mtu mwenye hadhi ya Karia maneno hayo Tena hadharani, mbele za watu.

Aisee!!! Alimkosea heshima mno. Mpira ni mchezo wa kiungwana, Ni mchezo wa watu waliostaarabika.

Jamaa naona siku hizi sifa zimemzidia, anajiamini mno sababu anajiona yupo karibu na GSM siku hizi.

Ana zile tabia za mswahili aliye karibu na tajiri, kudharau watu wengine walio juu yake akidhani kwa kuwa karibu na tajiri kila anachofanya atasupportiwa ni Tatizo la muda Tu, Soon GSM atamchoka.
Anatamba kuwa Jakaya Kikwete yuko nyuma yake hivyo kilio chake kitamfikia Rais Samia na atafunguliwa kabla ya siku ya mwananchi tena anatamba hivyo hadharani na hata vile vizee vya Yanga vimepita humo humo kwenye tamko lao. Basi tuone kama Rais mstaafu Jakaya Kikwete anao uwezo wa kuingilia maamuzi halali ya TFF. Tunamsubiri kwa hamu sana kumuona Haji Manara siku ya mwananchi akiunguruma kwa hisani ya JK, dj lete maneno!!!!!!
 
Back
Top Bottom