Manager wa TanRoads mkoa wa Arusha amejisahau

Manager wa TanRoads mkoa wa Arusha amejisahau

xtra-Pen

Member
Joined
Jan 5, 2018
Posts
20
Reaction score
22
Huyu Manager wa Tanroads mkoa wa Arusha sijui anafikiri mkoa wake wote una barabara za lami? Barabara ya kutoka Karatu mkoani Arusha kuelekea Mbulu mkoa wa Manyara ni mbaya sana ni mashimo matupu na rasta kilichobaki ni wajawazito kujifungua njiani kabla ya muda wao kufika. Huyu jamaa aitwaye Eng. Johnny Kalupale amejikalia zake pale mjini Arusha anakula bata wakati mwenzake wa mkoa wa Manyara Eng. Bashir Rwesingisa anafanya periodic maintenance kwa mara ya tatu sasa ndani ya miezi kama sita. Hili utalishuhudia ukifika tu mpakani mwa mkoa wa Arusha na Manyara eneo la Kilimapunda. Upande wa Mkoa wa Manyara hata km ni ya vumbi ni nzuri sana, upande wa mkoa wa Arusha Kilomita km 53 ni balaa sijawahi sehemu yoyote ktk hii Tanzania. Mh. Rais huyu Manager wa mkoa wa Arusha anasubiri nini ofisini? Pongezi zake Eng. Bashir Rwesingisa kwa kazi nzuri
 
Ongezea na ile barabara ya kuelekea Mererani kuanzia Moshono mwisho wa lami pale....nakiri nimewahi kupita mara moja tu pale ila ni kero tupu.
 
Barabara mpya ya Moshi arusha kuna sehemu zingine kuna walakini,kuna majengo yameachwa na yapo ndani ya barabara
 
Back
Top Bottom