Wadao natumai mu wazima na pole kwa waliopatwa na maswaibu mbalimbali ikiwa ni pamoja na wasafiri waliolala njiani kutokana na athari za mvua barabarani.
Nimefuatilia malumbano ya hoja yanayoendelea ITV na RADIO ONE. Nami ninao ushuhuda ufuatao.
Niseme kwamba nina mwanangu yupo kidato cha kwanza katika shule ya kata iitwayo MUGABE iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Nimemdadisi na kugundua shule ina changamoto zifuatazo.
1. IDADI KUBWA YA WANAFUNZI DARASANI.
Hii ndiyo changamoto kubwa inayosababisha mengine mengi mabaya katika shule hii. Darasa lina wanafunzi zaidi ya 100. Sijui sera ya elimu inasemaje katika hili. Ikumbukwe shule hii ipo jijini Dar na eneo lenye vitegauchumi vya kutosha hivyo ukosefu wa vyumba vya madarasa ni uzembe wa mamlaka husika.
2. UTOVU WA NIDHAMU KWA WANAFUNZI.
Nidhamu siyo tena jukumu la mwalimu mkuu na timu yake. Hili nilimuuliza mkuu wa shule alasema yeye hahusiki nalo. Kwa ufupi watoto hasa wa kiume wanatumia MIHADARATI na ni wezi. Na wale wa kike ki WAHUNI au MALAYA. Kwa hili la nidhamu matokeo yale ni kutofaulu vizuri kwa wanafunzi.
3.MAZINGIRA MABAYA/HATARISHO YA KUJIFUNZIA
ukiachana na upungufu wa vyumba vya madarasa. Kuna upungufu wa viti kwa wanafunzi. Vyooni hakuna maji na ni vichafu. Walimu kutofundisha ipasavyo. Ukosefu wa walimu hasa wa fani za Sayansi. nk.
Rai yangu ni kwamba mamlaka husika zifanye kazi zake ili kuboresha hii elimu. Na pia waandishi wa habari watusaidie kuandika habari za uchunguzi kuhusu namna elimu yetu inavyotolewa ili kuoa hiki kizazi.
Nimefuatilia malumbano ya hoja yanayoendelea ITV na RADIO ONE. Nami ninao ushuhuda ufuatao.
Niseme kwamba nina mwanangu yupo kidato cha kwanza katika shule ya kata iitwayo MUGABE iliyopo Jijini Dar es Salaam.
Nimemdadisi na kugundua shule ina changamoto zifuatazo.
1. IDADI KUBWA YA WANAFUNZI DARASANI.
Hii ndiyo changamoto kubwa inayosababisha mengine mengi mabaya katika shule hii. Darasa lina wanafunzi zaidi ya 100. Sijui sera ya elimu inasemaje katika hili. Ikumbukwe shule hii ipo jijini Dar na eneo lenye vitegauchumi vya kutosha hivyo ukosefu wa vyumba vya madarasa ni uzembe wa mamlaka husika.
2. UTOVU WA NIDHAMU KWA WANAFUNZI.
Nidhamu siyo tena jukumu la mwalimu mkuu na timu yake. Hili nilimuuliza mkuu wa shule alasema yeye hahusiki nalo. Kwa ufupi watoto hasa wa kiume wanatumia MIHADARATI na ni wezi. Na wale wa kike ki WAHUNI au MALAYA. Kwa hili la nidhamu matokeo yale ni kutofaulu vizuri kwa wanafunzi.
3.MAZINGIRA MABAYA/HATARISHO YA KUJIFUNZIA
ukiachana na upungufu wa vyumba vya madarasa. Kuna upungufu wa viti kwa wanafunzi. Vyooni hakuna maji na ni vichafu. Walimu kutofundisha ipasavyo. Ukosefu wa walimu hasa wa fani za Sayansi. nk.
Rai yangu ni kwamba mamlaka husika zifanye kazi zake ili kuboresha hii elimu. Na pia waandishi wa habari watusaidie kuandika habari za uchunguzi kuhusu namna elimu yetu inavyotolewa ili kuoa hiki kizazi.