sayoo
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 5,272
- 7,870
Kwanza kabisa tambua watu waliopo mitandaoni ndio hao hao mnaokutana mitaani, vyuoni, kwenye nyumba za ibada, maeneo ya starehe, kazini, ufukweni. Lakini zingatia haya yafuatayo sababu maeneo yote hayo kama ilivyo mitandaoni kuna watu wenye tabia mbaya na za kihuni na kuna wenye tabia nzuri. Mtu anaweza kuwa na nia kweli ya kutaka kupata mke au mume but akakutana na changamoto ya kupata mtu sahihi anayemtaka. So zingatia haya
1.Hasa kwa kinadada kwa mara ya kwanza usikubali kukutana na mwanaume nyumbani kwake, lodge au hotelini unaweza lazimishwa kufanya mapenzi bila ridhaa yako au kubakwa bila kumjua mtu vizuri. Kutana nae sehemu ya wazi yenye watu mkishafahamiana vizuri baadaye ndio unaweza kwenda
2.Kwa kinadada ukienda kukutana na mwanaume sehemu ya wazi hakikisha una pesa yako kidogo japo elfu kumi ili hata ikitokea kutokuelewana uwe na pesa yako ya kukusaidia nauli au uweze kulipia kinywaji mwenyewe ili kuepuka kufanya jambo ambalo moyo wako hautaki. Epuka kula vitu vya gharama kama huna pesa inaweza kukuletea changamoto mwanaume akakugeuka
3.Kwa wote wanaume na wanawake ukiona mtu hata hamjaonana lakini ana kuomba omba pesa huyo hakufai achana nae Kama lengo lako lilikuwa kutafuta mwenzi wa kweli mjenge maisha
4.Ukimwambia uliyeonana nae mkapime afya zenu lakini anakupigapiga chenga hataki kwenda kupima afya huyo hakufai achana nae yeye atakuwa anajijua tabia zake hajatulia. Mitandaoni huku wapo watu waliotulia wanaojiheshimu lakini pia wapo machangudoa na wanaume wanaonunua ovyo machangudoa. Kwahiyo umakini wa afya yako ni muhimu
5.Usiwe na haraka kwenda kumuonesha mtu unapoishi maana Kuna wengine ni matapeli hawana nia ya dhati
6.Kama unatafuta mchumba, mume halafu uliyekutana nae anataka penzi fasta fasta bila kujuana vizuri wala kupima afya huyo hakufai
7.Hasa kwa kinadada, Kama mmeshafahamiana kwa muda vizuri ila jamaa hataki kukupeleka anapoishi au kukutambulisha kwa ndugu zake basi tambua huyo ni mume wa mtu
8.Unapokuwa na nia ya dhati kutafuta mpenzi mtandaoni jieleze vizuri kwa uwazi na hiyo itasaidia kupunguza au kuwachuja haraka idadi ya watakaokutafuta ambao hawana vigezo unavyotaka ili kukupunguzia usumbufu
1.Hasa kwa kinadada kwa mara ya kwanza usikubali kukutana na mwanaume nyumbani kwake, lodge au hotelini unaweza lazimishwa kufanya mapenzi bila ridhaa yako au kubakwa bila kumjua mtu vizuri. Kutana nae sehemu ya wazi yenye watu mkishafahamiana vizuri baadaye ndio unaweza kwenda
2.Kwa kinadada ukienda kukutana na mwanaume sehemu ya wazi hakikisha una pesa yako kidogo japo elfu kumi ili hata ikitokea kutokuelewana uwe na pesa yako ya kukusaidia nauli au uweze kulipia kinywaji mwenyewe ili kuepuka kufanya jambo ambalo moyo wako hautaki. Epuka kula vitu vya gharama kama huna pesa inaweza kukuletea changamoto mwanaume akakugeuka
3.Kwa wote wanaume na wanawake ukiona mtu hata hamjaonana lakini ana kuomba omba pesa huyo hakufai achana nae Kama lengo lako lilikuwa kutafuta mwenzi wa kweli mjenge maisha
4.Ukimwambia uliyeonana nae mkapime afya zenu lakini anakupigapiga chenga hataki kwenda kupima afya huyo hakufai achana nae yeye atakuwa anajijua tabia zake hajatulia. Mitandaoni huku wapo watu waliotulia wanaojiheshimu lakini pia wapo machangudoa na wanaume wanaonunua ovyo machangudoa. Kwahiyo umakini wa afya yako ni muhimu
5.Usiwe na haraka kwenda kumuonesha mtu unapoishi maana Kuna wengine ni matapeli hawana nia ya dhati
6.Kama unatafuta mchumba, mume halafu uliyekutana nae anataka penzi fasta fasta bila kujuana vizuri wala kupima afya huyo hakufai
7.Hasa kwa kinadada, Kama mmeshafahamiana kwa muda vizuri ila jamaa hataki kukupeleka anapoishi au kukutambulisha kwa ndugu zake basi tambua huyo ni mume wa mtu
8.Unapokuwa na nia ya dhati kutafuta mpenzi mtandaoni jieleze vizuri kwa uwazi na hiyo itasaidia kupunguza au kuwachuja haraka idadi ya watakaokutafuta ambao hawana vigezo unavyotaka ili kukupunguzia usumbufu