figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,720
- 55,859
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KUEPUKA MATUKIO YA MOTO UNAOSABABISHWA NA UMEME MAJUMBANI.
1.Hakikisha utandazaji nyaya (wiring) inafanywa na mkandarasi aliyesajiliwa na Serikali
2.Hakikisha vifaa vyote vinavyofungwa vimethinitishwa na TBS (K.m: nyaya, soketi swichi, saketi breka na main swichi)
3.Hakikisha waya wa ethi umethibitishwa na TBS na umechimbiwa chini ardhini inavyotakiwa
4.Hakikisha unapotumia pasi usiiache ikiwaka ukaenda kufanya kazi nyingine. Vyivyo hivyo tutumiapo hita za kuchemshia maji na majiko ya umeme.
5.Tusinyooshe nguo kwa pasi ya umeme kitandani
6.Tuepuke utumiaji wa extension cable wa kudumu. Zitumike kwa dharura tu. Pia tusiweke extension cables kwenye mazuria (carpets)
7.Tusichaji simu na kuziweka kitandani. Pia tusitumie kompyuta mpakato (laptops) tukiwa tumezieka kitandani
8.Tusi plagi vitu vingi vinavyotumia umeme kwenye soketi moja kwa mfano TV radio na friji kwenye soketi moja
9.Tusiweke mapazia marefu kwenye madirisha yanayofunika soketi za umeme
10.Tutumie mapazia yasiyoshika moto kwa urahisi; kwa mfano mapazia ya nguo za pamba
11.Tuangalie magodoro ya vitanda yasikaribie au kugusa sokti au swichi za umeme
12.Makochi yetu tusiyaweke yakagusa au kukaribia sana swichi au soketi ya umeme. Yawekwe angalau umbali wa inchi sita (15sm)
13.Vyandarua vya vitanda visisogelee swichi au soketi ya umeme
14.Tupunguze wingi wa vitu vinavyoweza kuwaka moto ndani ya nyumba; kwa mfano, ni vizuri kuwa na seti moja tu ya makochi
15.Kama umeme ulikuwa umezima, ukiwaka tena kitu cha kwanza tuhakikishe mishumaa yote tuliyoiwasha wakati umeme umezimika tumeizima.
16.Kama fyuzi ya umeme itakatika au soketi breka ikajizima, tuhakikishe tumemwita fundi kukagua kwa nini ilizima. Tusiweke fyuzi nyingine au kuwasha tu saketi breka.
17.Tuhakikishe tunamwita mkandarasi aliyesajiliwa kupitia mfumo wote wa umeme kwenye nyumba (hasa maungio yote) kila baada ya miaka mitano
18.Tusiongeze vitu vinavyotumia umeme mwingi kama viyoyozi bila kuwahusisha makandarasi waliosajiliwa kuangalia uwezo wa mifumo yetu ya umeme kuhimili mzingo unaoongezeka.
19.Tusiunganishe umeme kutoka nyumba moja kwenda nyingine au kwenda kwenye banda la kuku bila ya kuwatumia wakandarasi waliosajiliwa
20.Ikitokea hitilafu yeyote ya umeme kuanzia kwenye mita ya TANESCO, braketi nguzo na kwenye laini ya umeme, tutoe taarifa katika kituo chochote cha TANESCO kwa kutumia namba za dharura.
TANESCO ''TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO''.
1.Hakikisha utandazaji nyaya (wiring) inafanywa na mkandarasi aliyesajiliwa na Serikali
2.Hakikisha vifaa vyote vinavyofungwa vimethinitishwa na TBS (K.m: nyaya, soketi swichi, saketi breka na main swichi)
3.Hakikisha waya wa ethi umethibitishwa na TBS na umechimbiwa chini ardhini inavyotakiwa
4.Hakikisha unapotumia pasi usiiache ikiwaka ukaenda kufanya kazi nyingine. Vyivyo hivyo tutumiapo hita za kuchemshia maji na majiko ya umeme.
5.Tusinyooshe nguo kwa pasi ya umeme kitandani
6.Tuepuke utumiaji wa extension cable wa kudumu. Zitumike kwa dharura tu. Pia tusiweke extension cables kwenye mazuria (carpets)
7.Tusichaji simu na kuziweka kitandani. Pia tusitumie kompyuta mpakato (laptops) tukiwa tumezieka kitandani
8.Tusi plagi vitu vingi vinavyotumia umeme kwenye soketi moja kwa mfano TV radio na friji kwenye soketi moja
9.Tusiweke mapazia marefu kwenye madirisha yanayofunika soketi za umeme
10.Tutumie mapazia yasiyoshika moto kwa urahisi; kwa mfano mapazia ya nguo za pamba
11.Tuangalie magodoro ya vitanda yasikaribie au kugusa sokti au swichi za umeme
12.Makochi yetu tusiyaweke yakagusa au kukaribia sana swichi au soketi ya umeme. Yawekwe angalau umbali wa inchi sita (15sm)
13.Vyandarua vya vitanda visisogelee swichi au soketi ya umeme
14.Tupunguze wingi wa vitu vinavyoweza kuwaka moto ndani ya nyumba; kwa mfano, ni vizuri kuwa na seti moja tu ya makochi
15.Kama umeme ulikuwa umezima, ukiwaka tena kitu cha kwanza tuhakikishe mishumaa yote tuliyoiwasha wakati umeme umezimika tumeizima.
16.Kama fyuzi ya umeme itakatika au soketi breka ikajizima, tuhakikishe tumemwita fundi kukagua kwa nini ilizima. Tusiweke fyuzi nyingine au kuwasha tu saketi breka.
17.Tuhakikishe tunamwita mkandarasi aliyesajiliwa kupitia mfumo wote wa umeme kwenye nyumba (hasa maungio yote) kila baada ya miaka mitano
18.Tusiongeze vitu vinavyotumia umeme mwingi kama viyoyozi bila kuwahusisha makandarasi waliosajiliwa kuangalia uwezo wa mifumo yetu ya umeme kuhimili mzingo unaoongezeka.
19.Tusiunganishe umeme kutoka nyumba moja kwenda nyingine au kwenda kwenye banda la kuku bila ya kuwatumia wakandarasi waliosajiliwa
20.Ikitokea hitilafu yeyote ya umeme kuanzia kwenye mita ya TANESCO, braketi nguzo na kwenye laini ya umeme, tutoe taarifa katika kituo chochote cha TANESCO kwa kutumia namba za dharura.
TANESCO ''TUNAYAANGAZA MAISHA YAKO''.