Naomba kujua kwa kipindi hichi cha mwisho wa Mwaka, ni mambo gani ya muhimu kujitathmini binafsi ili kujua ni kwa kiasi gani umefanikiwa katika malengo yako.
Kila mmoja anakipimo chake cha mafanikio, na hiyo hutokana tofauti ya malengo kwa kila mmoja.
Mafanikio yanaweza yakawa:
1. Kuoa
2. Kujenga nyumba
3. Kununua gari
4. Kupanga chumba
5. Kupanda cheo
6. Kuzaa mtoto/watoto
7. Kumaliza kukipa ada
8. Kuhamia kwenye nyumba yako
9. Kuingeza mke
10. Kupata kazi
Na kadhalika na kadhalika
Kwa maisha ya mtanzania wa kawaida, hayo ni mafanikio. Kwasababu kwa maisha yetu besic needs hazikuji kama hauto jiwekea malengo wewe binafsi.
Namaanisha besic needs hazishushwi kutoka Mbunguni na hata Serikali haitugawii.
Jana kuna member mmoja aliweka picha ya chumba chake kikiwa kimeenea na akasema wazi kabisa kwamba huo ndio ulikuwa mpango na malengo yake kwa mwaka huu 2019 na hayo ndio mafanikio aliyo yafikia.
Maana ya maisha imechanganyikana kwa undani na dhana za falsafa na imani za dini na hugusia masuala mengine mengi, kama vile
ontolojia, tunu , kusudi , maadili , hiari , uwepo wa
Mungu , roho , na kinachoendelea baada ya maisha haya kwisha.