LIKUYU SEKA
Member
- Nov 15, 2013
- 53
- 24
Habari watanzania wenzangu natumai tumeianza wiki vyema,kwa wale wagonjwa nawapa pole mungu awaponye na wenye matatizo pia mungu awape njia ya kutatua matatizo yao.
Ndugu zangu sote tunajua kuwa nchi yetu inaelekea kwenye uchaguzi mkuu oktoba mwaka huu ikiwa ni sambamba na zoezi la uandikishaji kwenye daftari la kudumu la mpiga kura,zoezi la uandikishaji lilianza mwanzoni mwa mwaka huu likizinduliwa mkoani njombe na safari hii tukitumia mfumo mpya Wa uandikishaji unaotambulika kama Biometric Voter Registration (BVR).
Huu ni mfumo mpya Wa uandikishaji kwa hapa nyumbani mfumo huu una uwezo mkubwa Wa kutambua muandikishwaji,Tume ya taifa ya Uchaguzi imesambaza mashine za Uandikishaji katika kanda ambazo zoezi hilo linafanyika.
Mpaka sasa tayari mikoa 5 imekamilisha zoezi la Uandikishaji wa wapiga kura mikoa hiyo ni Njombe,Lindi,Mtwara,Iringa na Ruvuma,yapo mambo muhimu kwa wale ambao bado hawajafikiwa kuandikishwa kuyajua.
Mambo muhimu kwa wale ambao hawajaandikishwa ya kuzingatia mosi ni kuwa zoezi la kujiandikisha limepata muitikio mkubwa sana,wananchi wengi nimeshuhudia wakijitokeza kwa wingi katika vituo vya kuajindikisha,jambo la kwanza la msingi ni kuwahi katika kituo cha kujiandikisha ukiweza uwahi mapema sana uzoefu unaonesha kuwa vituo vinafunguliwa saa mbili asubuhi hvyo kuwahi ni jambo la msingi sana ili waandikishaji watakapofika uwe wakwaza kujiandikisha.
Pili ni kwamba yapo mambo ambayo wakati Wa kuajindikisha unaulizwa,miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na jina lako kamili,mahali ulipozaliwa,tarehe na mwaka pamoja anuani yako ya kudumu haya ni mambo muhimu sana..
Tatu ni kuwa mashine ya BVR kwasiku huandikisha watu wasiozidi 120 na idadi hii ni pale endapo mashine haijaleta hitilafu yoyote,yapo maeneo ambayo mashine inaandikisha zaidi ya watu 120 lakini haivuki 180,hvyo kama umefika kwenye kituo cha kuajindikisha na ukaona wewe foleni yako umepitwa na watu zaidi ya 120 ujue hutaweza kuajiandikisha siku hiyo.
Kwauchache watanzania wenzangu haya ni mambo ambayo tunapaswa kuyazingatia ili kufanikiwa katika zoezi la kujiandikisha,Natoa rai Watanzania wenzangu kujitokeza kwa wingi kushiriki kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura.
Ndugu zangu sote tunajua kuwa nchi yetu inaelekea kwenye uchaguzi mkuu oktoba mwaka huu ikiwa ni sambamba na zoezi la uandikishaji kwenye daftari la kudumu la mpiga kura,zoezi la uandikishaji lilianza mwanzoni mwa mwaka huu likizinduliwa mkoani njombe na safari hii tukitumia mfumo mpya Wa uandikishaji unaotambulika kama Biometric Voter Registration (BVR).
Huu ni mfumo mpya Wa uandikishaji kwa hapa nyumbani mfumo huu una uwezo mkubwa Wa kutambua muandikishwaji,Tume ya taifa ya Uchaguzi imesambaza mashine za Uandikishaji katika kanda ambazo zoezi hilo linafanyika.
Mpaka sasa tayari mikoa 5 imekamilisha zoezi la Uandikishaji wa wapiga kura mikoa hiyo ni Njombe,Lindi,Mtwara,Iringa na Ruvuma,yapo mambo muhimu kwa wale ambao bado hawajafikiwa kuandikishwa kuyajua.
Mambo muhimu kwa wale ambao hawajaandikishwa ya kuzingatia mosi ni kuwa zoezi la kujiandikisha limepata muitikio mkubwa sana,wananchi wengi nimeshuhudia wakijitokeza kwa wingi katika vituo vya kuajindikisha,jambo la kwanza la msingi ni kuwahi katika kituo cha kujiandikisha ukiweza uwahi mapema sana uzoefu unaonesha kuwa vituo vinafunguliwa saa mbili asubuhi hvyo kuwahi ni jambo la msingi sana ili waandikishaji watakapofika uwe wakwaza kujiandikisha.
Pili ni kwamba yapo mambo ambayo wakati Wa kuajindikisha unaulizwa,miongoni mwa mambo hayo ni pamoja na jina lako kamili,mahali ulipozaliwa,tarehe na mwaka pamoja anuani yako ya kudumu haya ni mambo muhimu sana..
Tatu ni kuwa mashine ya BVR kwasiku huandikisha watu wasiozidi 120 na idadi hii ni pale endapo mashine haijaleta hitilafu yoyote,yapo maeneo ambayo mashine inaandikisha zaidi ya watu 120 lakini haivuki 180,hvyo kama umefika kwenye kituo cha kuajindikisha na ukaona wewe foleni yako umepitwa na watu zaidi ya 120 ujue hutaweza kuajiandikisha siku hiyo.
Kwauchache watanzania wenzangu haya ni mambo ambayo tunapaswa kuyazingatia ili kufanikiwa katika zoezi la kujiandikisha,Natoa rai Watanzania wenzangu kujitokeza kwa wingi kushiriki kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la mpiga kura.