Mambo Matano yaliyotikisa Dunia

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
10,439
Reaction score
18,495
1)Bomu la Hiroshima

Bomu la Hiroshima ni tukio lilitokea mwezi wa 8 mwaka 1945, ni moja kati ya tukio baya kuwahi tokea duniani.
Bomu hilo liliuwa watu takribani 70,000 na baadaye ndani ya miaka 5 watu wengine 70,000 walikufa kutokana na sumu ya Bomu hilo.

2)Translantic slave trade.

Hii ni biashara ya utumwa, ilianza
Katika karne ya 15 hadi ya 19 ilipoondolewa. Katika biashara hii waafrika zaidi ya milioni 60 walikufa.

3)Vietnam war.

Vita hii ilitokea Vietnam na Cambodia kutoka Nov /1 /1955 hadi April 30 1975 katika vita hii watu zaidi ya milioni 3 walikufa, kati yao watu 58,148 walikuwa raia wa marekani. Na watu wengine 75, 000 Walitoka Vilema.

4)Rwanda Genocide

Mauaji ya kimbari ya Rwanda yalitokea mnamo April 17 hadi July 15 mwaka 1994. vita hii ilikuwa kati ya hutu na tutsi ikipelekea mauaji ya watu milioni moja( 1000000)

5) September 11.

Mashambulizi ya kigaidi katika majengo pacha 2 huko marekani mwaka y 2011 yalipelekea watu zaidi ya elf tatu 3,000 kufariki dunia. Kati ya hao watu 400 walikuwa zimamoto na polisi.
 
😅😅😅😅 hivi ilikuwa ni world wide? Au huku kwetu ndio ilitikisa sana?
Nakumbuka kidogo tu…
Ilikuwa world wide!!

Zama zamani dunia ilikuwa ikiendeshwa na propaganda nyingi sana.
 
Siku ya hili tukio la 911 linatokea mahali nilipokuwepo ilikua ni alfajiri ya saa kumi na Moja...

Nachungulia nje nakuta barriers na askari kama wote hakuna raia kupita pita eneo hilo...
Keep memories alive 😉
 
Corona imetikisa shehe na hii vita ya Ukraine. Kuliko September 11, Wala Rwanda genocide
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…