Mama Ake Anataka Mwanae Aolewe Na Mwanaume Aliezaa Nae Tu

Mama Ake Anataka Mwanae Aolewe Na Mwanaume Aliezaa Nae Tu

ZebyK

Member
Joined
Oct 19, 2018
Posts
12
Reaction score
4
Wana jf, mm ni kijana niliekatika mahusiano ya kimapenzi na bint mmoja, ambae bint huyu kiukweli japo nmemkuta akiwa na mtoto nmetokea kumpenda sana hadi kufikia maamuzi ya kutaka kuishi nae kama mke na kwa kiasi kikubwa ni kama namsaidia kumlelea mwanae kwa kumsaidia kila kitu,lkn changamoto ninayokutana nayo ni kua mama ake mzazi anamwambia bint kua hawezi olewa na mwanaume mwingne zaid ya aliezaa nae, jambo hili linaniumiza sana kwasababu ni mwanamke ambae toka nmfaham hakika sitaman kumuacha kabisa..naombeni ushauri na mawazo yenu wanajamvi.
 
Msichana msimamo wake ndio suluhusho lako

Huyo baba wamtoto anahudumia mwanae?? Na hata kama anahudumia je moyo wa msichana uko kwa nani??

Huyo mama anapaswa kujua jukumu la kumlea mwanae na kua chini yake lina kikomo,na kila mtu yuko huru kichagua mtu anaemtaka wa kuishi nae sio kupangiana
 
Kuna muda mama zetu huwa wanakosea basi tu...

Kuna best yangu nae aliolewa sababu mama yake alimlazimisha aolewe eti kisa mkaka kamtoa bikra so lazima amuoe binti yake...matokeo yake best yangu ndoa imemshinda yuko nyumbani na mtoto

Pole mkuu..
Hapo wewe huna cha kufanya zaidi ya kusikiliza msimamo wa huyo bidada unayetaka kumuoa
 
Hilo lisikuumize sana kwa kuwa unayempenda ndio mwenye maamuzi ya mwisho. Tulia muangalie mwenzako kwa macho yote mawili, yeye atasimamia upande gani wa kulia, au kushoto. Lakini mara nyingi mambo yakishakuwa hivi huna budi kujiandaa kuyapokea maumivu kwa sababu ni mara chache sana kutokea mtu kuacha kufuata matakwa ya mzazi, au wazazi hasa pale inapotekea mvutano katika mahusiano yenu hata kama mapenzi ya dhati ya kubebana kama sumaku yapo juu yako bado kunakuwa hakuna tena lile daraja la kuwakutanisha kuwafanya muendelee kuwa kitu kimoja kutokana na mwenzako kutawaliwa na hofu ya kutengwa na wazazi, au hata ndugu.

Pole sana mkuu kwa maelezo marefu, ndio dunia hii kua uyaone!
 
Kuna muda mama zetu huwa wanakosea basi tu...

Kuna best yangu nae aliolewa sababu mama yake alimlazimisha aolewe eti kisa mkaka kamtoa bikra so lazima amuoe binti yake...matokeo yake best yangu ndoa imemshinda yuko nyumbani na mtoto

Pole mkuu..
Hapo wewe huna cha kufanya zaidi ya kusikiliza msimamo wa huyo bidada unayetaka kumuoa
Ndo tatizo la wazazi wengi kujiona wana haki na maamuzi kwenye mahusiano ya watoto wao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msichana msimamo wake ndio suluhusho lako

Huyo baba wamtoto anahudumia mwanae?? Na hata kama anahudumia je moyo wa msichana uko kwa nani??

Huyo mama anapaswa kujua jukumu la kumlea mwanae na kua chini yake lina kikomo,na kila mtu yuko huru kichagua mtu anaemtaka wa kuishi nae sio kupangiana
ofcoz baba wa mtoto anahudumia mwanae kwa nafasi yake, na mm pia pale huyu mdada anahitaji msaada juu ya malezi ya mwanae sijawai kuacha kumsaidia wala kumtupa pale anapohitaji msaada wangu katika malezi ya mtoto wake.
 
Hilo lisikuumize sana kwa kuwa unayempenda ndio mwenye maamuzi ya mwisho. Tulia muangalie mwenzako kwa macho yote mawili, yeye atasimamia upande gani wa kulia, au kushoto. Lakini mara nyingi mambo yakishakuwa hivi huna budi kujiandaa kuyapokea maumivu kwa sababu ni mara chache sana kutokea mtu kuacha kufuata matakwa ya mzazi, au wazazi hasa pale inapotekea mvutano katika mahusiano yenu hata kama mapenzi ya dhati ya kubebana kama sumaku yapo juu yako bado kunakuwa hakuna tena lile daraja la kuwakutanisha kuwafanya muendelee kuwa kitu kimoja kutokana na mwenzako kutawaliwa na hofu ya kutengwa na wazazi, au hata ndugu.

Pole sana mkuu kwa maelezo marefu, ndio dunia hii kua uyaone!
ahsante kwa ushauri kwakweli hata mm nmejiandaa kisaikolojia kwa lolote.. japo huyu mdada kanihakikishia kwa asilimia zote hawez ntupa. nina matumaini huenda mama ake akaja kunielewa ni kipind cha mida tu.
 
Back
Top Bottom