Malezi ya watoto na changamoto zake

Malezi ya watoto na changamoto zake

The Icebreaker

Platinum Member
Joined
Apr 24, 2014
Posts
34,177
Reaction score
102,950
Wakuu,mada hii ni maalum kwa wazazi au walezi wa watoto,changamoto tunazopitia katika malezi ya watoto na jinsi ya kukabiliana nazo,wote tunatambua kua malezi ya watoto ni muhimu na watoto ndio taifa la kesho,maadili mema,utambuzi wa mambo na mengineyo,mtoto huanza kujifundisha kupitia watu waliomzunguka katika makuzi yake na hasa wazazi/walezi wake,kwani ndio anakua nao kwa muda mwingi zaidi tangu kuzaliwa kwake,

Hivyo basi,mada hii ni vizuri tukashare matatizo yanayotukabili katika malezi ya watoto na jinsi ya kukabiliana nayo,mfano mtoto kutokupenda kwenda shule,kutokupenda kuchanganyika na wenzake,kutokupenda kula,uwezo wake kimasomo na mengineyo,

Kama mzazi/mlezi yeyote ambaye amewahi kukumbana na tatizo la kimalezi kisha akalitatua na kufanikiwa,ni vizuri akashare nasi hapa ili wengine wajifundishe kupitia kwake,kama mzazi/mlezi ana changamoto katika malezi ya watoto,basi ataweka changamoto anazopitia ili wataalamu waje na kutoa solution au njia za kumaliza/kupunguza tatizo hilo,

Karibuni sana.
 
Bado sijafikia cheo chenu ila Kuna mambo umeyaandika hapo nimeona yanamapungufu!,mkuu ni lazima wazazi mjue saikolojia za watoto wenu.
Kuna tabia mtoto atazionyesha ni haiba yake na ni ama hawezi pia kuziepuka.. mfano kupenda kukaa peke yake,hii ni aina ya tabia ambayo introvert hupenda na ndivyo walivyo kwani kwao inawafanya wanakuwa strong zaidi na creative!. Unatakiwa ufahamu kabla hujaanza kumshambulia na mijeledi.muda mwengine si ati mzazi kamshindwa mtoto ila mtoto kamshindwa mzazi maana unakuta mzazi anataka anayotaka yeye ambayo mtoto kutokana na saikilojia yake hawezi kuyatimiza!!.
Hivyo huu ni ushauri tu kwa wazazi na pia unatakiwa ujue uwezo wa akili wa mwanao si kumlazimisha afanye Kama fulani watu tu tofauti unatakiwa uelewe hili.
 
Best feeling ever ilikua ni kutumia pesa yangu kumnunulia binti yangu soksi, kofia, gauni na diapers.

Asikwambie mtu nilchokihisi siwezi kuelezea.

Juzi ameanza kuota jino.
 
Mimi nitakuja kutoa mrejesho kwa binti yangu yupo darasa la 3 ambaye alikuwa akiishi kwa mama yake toka kindergarten hadi darasa la pili changamoto Za malezi nilizopitia kwa muda huu Mfupi toka nianze kuishi nae na upande wa taaluma toka hali Niliyomkuta nayo hadi sasa huu mrejesho nitautoa baada ya kumaliza term ya 2 Au mwaka 1 toka niishi naye nadhan mtapata funzo kubwa wazazi wenzangu
 
Bado sijafikia cheo chenu ila Kuna mambo umeyaandika hapo nimeona yanamapungufu!,mkuu ni lazima wazazi mjue saikolojia za watoto wenu.
Kuna tabia mtoto atazionyesha ni haiba yake na ni ama hawezi pia kuziepuka.. mfano kupenda kukaa peke yake,hii ni aina ya tabia ambayo introvert hupenda na ndivyo walivyo kwani kwao inawafanya wanakuwa strong zaidi na creative!. Unatakiwa ufahamu kabla hujaanza kumshambulia na mijeledi.muda mwengine si ati mzazi kamshindwa mtoto ila mtoto kamshindwa mzazi maana unakuta mzazi anataka anayotaka yeye ambayo mtoto kutokana na saikilojia yake hawezi kuyatimiza!!.
Hivyo huu ni ushauri tu kwa wazazi na pia unatakiwa ujue uwezo wa akili wa mwanao si kumlazimisha afanye Kama fulani watu tu tofauti unatakiwa uelewe hili.
Shida ipo hapa... ...


Vita ya akili ya ndani kwa ndani baina ya mzazi na mtoto...

Hii Ni mbaya Sana na inasaidia kuvuruga mno .. .saikolojia ya watoto..
 
Back
Top Bottom