Malalamiko: Kampuni ya Tigo mnakera

Malalamiko: Kampuni ya Tigo mnakera

Maulid Daniel

Senior Member
Joined
Jul 4, 2012
Posts
140
Reaction score
72
Ndugu wana jamiiforums.

Mimi ni mteja wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO lakini cha kushangaza tokea nimefika hapa mjini Morogoro takribani mwezi mmoja na nusu nimeshuhudia huduma mbovu za kimtandao ndani ya Mkoa huu.

Ikifika saa 12 jioni mpaka saa 4 usiku network inakuwa zero haswa kwa watumiaji wa internet. Yani hata uwezo wa kufungua link za humu jamii forum ni shida, Facebook wanayoisema ni ya bure kwa kiswahili haifunguki, SMS za whatsapp haziingii wala hazitoki.

Tunaomba wahusika mlishughulikie hili tatizo maana nimejaribu kwenda ofisi zao pale mjini karibu na stend lakini hawajanisikiliza na kwa ninavyoona hawana nia ya kulishughulikia hili tatizo.
 
Aisee yaani inakera ni hivyo hivyo hata dsm,na sisi tulionunua simu zinazotumia line ya tigo tu imekula kwetu.
 
mi leo nimewahama rasmi pesa yangu simu yangu yanini kuangaishwa ki ukweli TIGO hamna kitu!
 
ni kweli kabisa TIGO wameshindwa kazi. Sijui sheria zipoje ili kama kuna uwezekano wa kuwaburuza kortini nifanye hivyo mara moja.
 
Ndugu wana jamii forum mimi ni mteja wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO lakini cha kushangaza tokea nimefika hapa mjini Morogoro takribani mwezi mmoja na nusu nimeshuhudia huduma mbovu za kimtandano ndani ya Mkoa huu. Ikifika saa 12 jioni mpaka saa 4 usiku network inakuwa zero haswa kwa watumiaji wa internet. Yani hata uwezo wa kufungua link za humu jamii forum ni shida, FB wanayoisema ni ya bure kwa kiswahili haifunguki, msg za whatsapp haziingii wala hazitoki. Tunaomba wahusika mlishughulikie hili tatizo maana nimejaribu kwenda ofisi zao pale mjini karibu na stend lakini hawajanisikiliza na kwa ninavyoona hawana nia ya kulishughulikia hili tatizo.

Hamia Airtel
 
hapa Tanga,usumbufu wa intanet ni kuanzia saa 12 hadi 6 usiku.tigo wanaboa sana.
 
yaani hata mm baada tu ya kifurushi kuisha imekua kero yaani nikiongea nao huduma kwa wateja wanasema wanakutumia configuration lakini uki install bado tatizo linakuwa palepale sasa sijui wanafanya makusudi
 
tiGO wameshapata wateja wengi, sasa wameelemewa, kuna suala la voucher zao, hazina ubora kbs, ukikwangua ikatokea umekwangua hadi zile namba, ndo imetoka hutarudishiwa huo muda wa maongezi hata kama umewasilisha hiyo card ya vocha ktk ofisi husika!
 
Tigo sikuiz wana wateja wengi ndio maana wanatuletea mapoz.....
 
Network yao kimeo haipiti masaa 2 inazngua
 
ina maana haya tunayolalamikia kwao sio issue?hadi sasa tatizo liko palepale!
 
Tigo ni mzigo tunaitumia kwasababu ya wenzetu wanao tumia unless otherwise haifai... Angalia menu ya MPESA na TIGO PESA.. Total different.. ya Tigo haieleweki kabisa ... Matangazo mengi sana na sijui kama hata wanayalipia.. ukiweka vocha utapokea messege kama 4 Hivi... Menu yao us kijiunga na vifurushi tatizo leo iko Hivi kesho vingine.. vifurushi vina badilika kila kukicha... Tigo Acheni uswahili..
 
Ndugu wana jamiiforums.

Mimi ni mteja wa kampuni ya simu za mkononi ya TIGO lakini cha kushangaza tokea nimefika hapa mjini Morogoro takribani mwezi mmoja na nusu nimeshuhudia huduma mbovu za kimtandao ndani ya Mkoa huu.

Ikifika saa 12 jioni mpaka saa 4 usiku network inakuwa zero haswa kwa watumiaji wa internet. Yani hata uwezo wa kufungua link za humu jamii forum ni shida, Facebook wanayoisema ni ya bure kwa kiswahili haifunguki, SMS za whatsapp haziingii wala hazitoki.

Tunaomba wahusika mlishughulikie hili tatizo maana nimejaribu kwenda ofisi zao pale mjini karibu na stend lakini hawajanisikiliza na kwa ninavyoona hawana nia ya kulishughulikia hili tatizo.

Mtoa mada, kuanzia muda huo ni NCHI NZIMA. Kila watu walioko mikoa tofauti wanalalamikia suala hilo. Yaani network iko very poor ikishafika saa12 na kuendelea hadi saa6 hivi usiku. Huwez kuamini hata Dar ambako hali ilikuwa afadhali sasa imejirudia.
 
Tigo ni mzigo tunaitumia kwasababu ya wenzetu wanao tumia unless otherwise haifai... Angalia menu ya MPESA na TIGO PESA.. Total different.. ya Tigo haieleweki kabisa ... Matangazo mengi sana na sijui kama hata wanayalipia.. ukiweka vocha utapokea messege kama 4 Hivi... Menu yao us kijiunga na vifurushi tatizo leo iko Hivi kesho vingine.. vifurushi vina badilika kila kukicha... Tigo Acheni uswahili..

Sijui kama nimekuelewa vizuri, kama nimekuelewa vyema Tigo ndio the best one kwenye e-money na wana app yao kabisa ingia playstore ujipakulie.

Ila kwa huduma zingine kampuni zote hovyo kabisa na wizi wa bunde umeshika kasi.
 
Back
Top Bottom