Malaigwanani wajichanganya Kiteto

Malaigwanani wajichanganya Kiteto

JAMHURI

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
449
Reaction score
60
Zikiwa zimebakia siku tatu wananchi kuingia kwenye chumba cha kufanya maamuzi ya nani aongoze kwa kupiga kura, hii leo hapa Wilayani Kiteto lile dili la kisiasa kwa viongozi wa mila Malaigwanani wa jamii ya kifugaji maasai, kutaka kupata fedha kupitia siasa limebainika baada ya kujikuta hawana mwelekeo na kuwafanya jamii hiyo kutanga wasijue wakumchagua.

Wagombea watatu wa ngazi ya Ubunge akiwemo wa CCM Emanuel Papian, CHADEMA Kidawa Othaman, na CUF Hasani Losioki wamekuwa wakihaha juu ya jamii hiyo iliyodaiwa kutishia kutompa kura mgombea asiyekubalika na mwenye maslahi kwao.

Baada ya kuhaha kwa muda mrefu huku wakila fedha za wagombea hao sasa wamebakia njia panda baada ya kukosa mwelekeo wa nani wawaelekeze wafuasi wao kuwa ndiye atakayelinda maslahi yao ya kifugaji.

Maslahi hayo ni yale ya kulinda maeneo ya malisho ambayo yamekuwa na changamoto kubwa kwao na kusababisha mgogoro wa wakulima na wafugaji

CCM, CHADEMA, CUF wote wanatumainia hatma ya jamii hiyo wanaotamba kuwa wako wengi kuliko makabila mengine hapo wilayani Kiteto.

Hali bado sio shwaari, hakuna anayejua nani ni nani.
 
Katika hatua hiyo kumekuwepo na sarakasi kibao toka kwa jamii hiyo ya kifuagaji maasai ambapo mwenyekiti wa CCM mkoa wa manyara Ole Mukus alilazimika kuzungumza na jamii hiyo kwa kina ambapo kwa mujibu wa kauli yake alisema kuwa mambo yamekaa sawa..
 
Kwa upande wake Emmanuel Papiani akizungumza hivi karibuni alisema hali shwari upepo unamwelekea yeye huku kidawa naye akijitapa sambana na kuzunguna na baadhi ya vijana wa kifugaji kuwa kura za jamii hiyo zote ziko kwake na hasani Losiok naye akidai amemaliza kazi kwa kula amini na jamii hiyo kuwa watampa kupa ili awe mshindi wa ubunge mwaka huu
 
Mirembe wamefungua internet cafe for those who are doing well

Msameheni bure mleta uzi
 
Labda na mimi natakiwa nipate elimu, elimu, elimu. Maana kama sielewi vile.
 
Back
Top Bottom