Makutupora Nimekuja Kutoa Shukurani! Mungu Awabariki Sana!

Makutupora Nimekuja Kutoa Shukurani! Mungu Awabariki Sana!

makutupora

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2015
Posts
2,482
Reaction score
5,133
Mwenzenu Makutupora nimekuja kutoa shukurani!


Mwenzangu, wanajukwaa wenzangu!
Najua imepita muda tangu nitume ombi langu la msaada, lakini ninachoamini ni hiki: Asiyeweza kuwa mwingi wa shukurani ni mtu mbaya sana!

Kwanza kabisa, naomba kutoa shukrani za dhati kwa kila mmoja wenu mlionitafuta kwa PM, mlioonyesha nia ya kunisaidia — kwa namna moja ama nyingine, hata kama hatukufikia muafaka, bado ninyi ni watu wa kipekee sana kwangu. Moyo wangu unawashukuru sana!

Wale wote tuliowahi kuongea kwa simu, au hata kwa kuchat kawaida — naomba moyo wangu wa shukurani uwafikie pia!
Mmeonyesha upendo na kujali zaidi ya maneno.

Shukurani za pekee na za kipekee kabisa naomba zifike kwa Shangazi Mambo — mbali na mada zako za kufurahisha watu, hujawahi kuniacha, umebaki kuwa Malkia wa nguvu kwangu. Mungu pekee ndiye anayejua hili.

Kwa Rais wa Majobless, Balotola, na wengine wote ambao kwangu mmekuwa kama ndugu, japo hata sura zenu sizijui — nawashukuru sana sana.

Nimekuja hapa kutoa shukurani kwenu nyote mliojali maumivu yangu. Kikubwa zaidi ni kwamba, nimepata kazi ya kujitolea hapa Mwanza — nimeanza na hadi sasa nimefikisha wiki moja!
Walionipa kazi wamenipatia malazi na chakula cha mchana. Ni taasisi nzuri yenye ushirikiano mkubwa sana. Leo hii ndio nimepewa barua rasmi ya kutambulika kama mfanyakazi tarajiwa, lakini wameshanisaidia mambo mengi sana.

Nina amani, furaha, na muda wa kuomba na kumuabudu Mungu. Napata muda wa kufuatilia ibada za Koinonia. Kubwa zaidi, Mama pia anaendelea vizuri — jambo ambalo kwangu ni faraja kubwa mno.

Kwa hakika sitaki kuongea mengi, ila nimekuja kutoa shukurani zangu za kweli. Sijui ni nani aliwahi kuongelea ule wimbo wa Lucky Dube - “Usizi” — ila ndiyo wimbo ninaousikiliza hata sasa… nausikiliza kila muda.

Katika yote, poleni shukurani zangu!
Mungu awabariki sana — Mlikuwa nami kwenye giza, na sasa mnashuhudia nuru!

Makutupora!
Samaleko.

Soma Pia: Shida haina hodi, mwenzenu nimefika mwisho, naombeni msaada
 
Mwenzenu Makutupora nimekuja kutoa shukurani!


Mwenzangu, wanajukwaa wenzangu!
Najua imepita muda tangu nitume ombi langu la msaada, lakini ninachoamini ni hiki: Asiyeweza kuwa mwingi wa shukurani ni mtu mbaya sana!

Kwanza kabisa, naomba kutoa shukrani za dhati kwa kila mmoja wenu mlionitafuta kwa PM, mlioonyesha nia ya kunisaidia — kwa namna moja ama nyingine, hata kama hatukufikia muafaka, bado ninyi ni watu wa kipekee sana kwangu. Moyo wangu unawashukuru sana!

Wale wote tuliowahi kuongea kwa simu, au hata kwa kuchat kawaida — naomba moyo wangu wa shukurani uwafikie pia!
Mmeonyesha upendo na kujali zaidi ya maneno.

Shukurani za pekee na za kipekee kabisa naomba zifike kwa Shangazi Mambo — mbali na mada zako za kufurahisha watu, hujawahi kuniacha, umebaki kuwa Malkia wa nguvu kwangu. Mungu pekee ndiye anayejua hili.

Kwa Rais wa Majobless, Balotola, na wengine wote ambao kwangu mmekuwa kama ndugu, japo hata sura zenu sizijui — nawashukuru sana sana.

Nimekuja hapa kutoa shukurani kwenu nyote mliojali maumivu yangu. Kikubwa zaidi ni kwamba, nimepata kazi ya kujitolea hapa Mwanza — nimeanza na hadi sasa nimefikisha wiki moja!
Walionipa kazi wamenipatia malazi na chakula cha mchana. Ni taasisi nzuri yenye ushirikiano mkubwa sana. Leo hii ndio nimepewa barua rasmi ya kutambulika kama mfanyakazi tarajiwa, lakini wameshanisaidia mambo mengi sana.

Nina amani, furaha, na muda wa kuomba na kumuabudu Mungu. Napata muda wa kufuatilia ibada za Koinonia. Kubwa zaidi, Mama pia anaendelea vizuri — jambo ambalo kwangu ni faraja kubwa mno.

Kwa hakika sitaki kuongea mengi, ila nimekuja kutoa shukurani zangu za kweli. Sijui ni nani aliwahi kuongelea ule wimbo wa Lucky Dube - “Usizi” — ila ndiyo wimbo ninaousikiliza hata sasa… nausikiliza kila muda.

Katika yote, poleni shukurani zangu!
Mungu awabariki sana — Mlikuwa nami kwenye giza, na sasa mnashuhudia nuru!

Makutupora!
Samaleko.

Soma Pia: Shida haina hodi, mwenzenu nimefika mwisho, naombeni msaada
Ubarikiwe kwa kuja na shukrani japo sijakuelewa ulisaidiwa nini na kwa shida gani na watajwa juu
 
Aliyeelewa ani pm
Haha furaha aliyonayo imemfanya ashindwe kupangilia vizuri kile haswa alichotaka kukileta mbele ya hadhila. Ila kiufupi anashukuru maana amepata kazi ya kujitolea huko Mwanza baada ya mahangaiko ya muda mrefu. Pia anashukuru kwa members wote waliompa moyo na kumfariji kipindi chote alichokuwa anapitia magumu bila kazi. Mungu ambariki na asimame vizuri maana mwanzoni huwa wanyenyekevu na mipango mingi ya mafanikio ila mazoea yakishakolea binadamu tuna hurka ya kusahau tulivyohenya nakuanza kuishi kutokana na nafasi tulizonazo.
Hongera sana makutupora na Mungu akutangulie katika njia mpya ya kimaisha
 
Haha furaha aliyonayo imemfanya ashindwe kupangilia vizuri kile haswa alichotaka kukileta mbele ya hadhila. Ila kiufupi anashukuru maana amepata kazi ya kujitolea huko Mwanza baada ya mahangaiko ya muda mrefu. Pia anashukuru kwa members wote waliompa moyo na kumfariji kipindi chote alichokuwa anapitia magumu bila kazi. Mungu ambariki na asimame vizuri maana mwanzoni huwa wanyenyekevu na mipango mingi ya mafanikio ila mazoea yakishakolea binadamu tuna hurka ya kusahau tulivyohenya nakuanza kuishi kutokana na nafasi tulizonazo.
Hongera sana makutupora na Mungu akutangulie katika njia mpya ya kimaisha
Nashauri aprint maoni haya
 
Mwenzenu Makutupora nimekuja kutoa shukurani!


Mwenzangu, wanajukwaa wenzangu!
Najua imepita muda tangu nitume ombi langu la msaada, lakini ninachoamini ni hiki: Asiyeweza kuwa mwingi wa shukurani ni mtu mbaya sana!

Kwanza kabisa, naomba kutoa shukrani za dhati kwa kila mmoja wenu mlionitafuta kwa PM, mlioonyesha nia ya kunisaidia — kwa namna moja ama nyingine, hata kama hatukufikia muafaka, bado ninyi ni watu wa kipekee sana kwangu. Moyo wangu unawashukuru sana!

Wale wote tuliowahi kuongea kwa simu, au hata kwa kuchat kawaida — naomba moyo wangu wa shukurani uwafikie pia!
Mmeonyesha upendo na kujali zaidi ya maneno.

Shukurani za pekee na za kipekee kabisa naomba zifike kwa Shangazi Mambo — mbali na mada zako za kufurahisha watu, hujawahi kuniacha, umebaki kuwa Malkia wa nguvu kwangu. Mungu pekee ndiye anayejua hili.

Kwa Rais wa Majobless, Balotola, na wengine wote ambao kwangu mmekuwa kama ndugu, japo hata sura zenu sizijui — nawashukuru sana sana.

Nimekuja hapa kutoa shukurani kwenu nyote mliojali maumivu yangu. Kikubwa zaidi ni kwamba, nimepata kazi ya kujitolea hapa Mwanza — nimeanza na hadi sasa nimefikisha wiki moja!
Walionipa kazi wamenipatia malazi na chakula cha mchana. Ni taasisi nzuri yenye ushirikiano mkubwa sana. Leo hii ndio nimepewa barua rasmi ya kutambulika kama mfanyakazi tarajiwa, lakini wameshanisaidia mambo mengi sana.

Nina amani, furaha, na muda wa kuomba na kumuabudu Mungu. Napata muda wa kufuatilia ibada za Koinonia. Kubwa zaidi, Mama pia anaendelea vizuri — jambo ambalo kwangu ni faraja kubwa mno.

Kwa hakika sitaki kuongea mengi, ila nimekuja kutoa shukurani zangu za kweli. Sijui ni nani aliwahi kuongelea ule wimbo wa Lucky Dube - “Usizi” — ila ndiyo wimbo ninaousikiliza hata sasa… nausikiliza kila muda.

Katika yote, poleni shukurani zangu!
Mungu awabariki sana — Mlikuwa nami kwenye giza, na sasa mnashuhudia nuru!

Makutupora!
Samaleko.

Soma Pia: Shida haina hodi, mwenzenu nimefika mwisho, naombeni msaada
Moyo wa shukrani ni moyo Safi,kila la kheri Mkuu!
 
Back
Top Bottom