Diason David
JF-Expert Member
- Aug 2, 2018
- 7,562
- 7,348
Mnada wa mali zilizomo ndani ya makontena 20 ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda unaendelea na tayari wateja wameshakagua bidhaa na wanashindana kununua
Asilimia kubwa ya bidhaa zilizomo kwenye makontena hayo ni samani za ofisini kama vile viti, meza na makabati
Itakumbukwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango aliagiza makontena hayo kupigwa mnada licha ya RC Makonda kutoa vitisho kuwa atakayenunua vitu vilivyopo kwenye makontena hayo atapata laana kali
Mnada wa Makontena hayo unakuja ikiwa ni baada ya RC Makonda kushindwa kulipia kodi ya Tsh. Bilioni 1.2