Makinda na Zungu tutawakumbuka daima

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,252
8,003
Binafsi hua sipendi kummwagia mtu misifa hovyo hovyo lakini Leo hii acha hawa watu nisiwanyime haki zao pamoja na mapungufu walivyokua nayo kama wanadamu wengine.Ni wanasiasa wazoefu, watulivu, wastahamilifu na wenye kuongozwa na busara na hekima zaidi.Hawa viongozi waliliongoza bunge kwa ubunifu wa hali ya juu sana mpaka kufikua kujenga heshima ndani ya bunge.

Ni viongozi ambao walitambua kwamba kua njia pekee ya kuendesha mambo vizuri ni mawasiliano mazuri ama maridhiano katika pande mbili zinazokinzana! Ni viongozi waliojua kua utatuzi pekee wa migogoro ndani ya bunge ni majadiliano inapotokea kutokuelewana baina ya pande mbili kinzani, ni viongozi waliosoma vizuri mwenendo wa bunge na mazingira yaliyokuepo na wakati wake pia badala ya kutumia ubabe.

Ndio kuna mahali walijaribu kutumia ubabe lakini ni pale ambapo mambo yalionekana kua magumu sana kufikia kukosa maamuzi mengine zaidi ya kutumia nguvu kiasi.Ukiwa kiongozi bila kuangalia na kuwasoma surbodinates wako, bila kusoma wakati, bila kusoma mazingira uliopo kwa hakika uongozi utakushinda! Utatumia sana ubabe lakini lakini itafika mahali utashindwa na dhamira yako itakusuta kufikia kuikimbia nafasi yako ya uongozi.

Ni washauri tu ndugu zangu Chenge, Ndungai pamoja na Dkt Tulia kwamba bado ni mapema sana kwao watumie muda huu kujirekebisha mapema wasianze vibaya! Watumje zaidi njia ya majadiliano kila inapotokea kutoelewana baina ya pande kinzani ndani ya bunge, watumishi kamati za bunge kurekebisha mambo mfano kàmati ya uongozi na kamati ya maadili. Inapotokea serikali inakosolewa wachukulie kua ndio kazi ya bunge kufanya hivyo kuliko kutanguliza ukada zaidi, unapokua kiongozi wa pinde mbili kinzani lazima uwe neutral bila kupendelea upande wowote.
 
Kwa maoni yangu ushauri wako unawahusu Chenge na Dr Turia.

Kwa upande wa ndungai ni mapema mno kumuhukumu,
Kwenye sakata la escrow alionyesha mwelekeo mzuri tumpe mda.
 
Nyie huwa mko hivyo hivyo wanafikiwanafiki sana. Jk mlimwita dhaifu lakini eti Leo mnasema mnamkumbuka sana na ana afadhali sana! Mi siku hizi simwamini mwanasiasa yeyote.
 
Mtoa hoja nyie ni watu wa kubadilika badilika (unrealiable) Sasa hivi tunawapuuza tu.Mara museme Lowasa Fisadi kesho sio fisadi.
Kikwete akiwemo madarakani mnasema mpole anacheka cheka tu akija asiyecheka Magufuli mnasema mtu gani mkali na asiyecheka na watu.

Sasa tuna kazi moja tu kuwapuuza na kuwaambia CCM mbele kwa mbele ,Ndugai na Tulia mbele kwa mbele na Magufuli Mbele kwa Mbele
 
Mtoa hoja nyie ni watu wa kubadilika badilika (unrealiable) Sasa hivi tunawapuuza tu.Mara museme Lowasa Fisadi kesho sio fisadi.
Kikwete akiwemo madarakani mnasema mpole anacheka cheka tu akija asiyecheka Magufuli mnasema mtu gani mkali na asiyecheka na watu.

Sasa tuna kazi moja tu kuwapuuza na kuwaambia CCM mbele kwa mbele ,Ndugai na Tulia mbele kwa mbele na Magufuli Mbele kwa Mbele
hawa ngedere waliendekezwa sana na Mama Makinda na Mzee Kikwete. walifikia hata hatua ya kuwatukana. sasa acha kwanza wakutane na mkono wa chuma wa mh. Magufuli na Mtemi wa ukweli Chenge a.k.a Mnyatunzu. mbona wataisoma number bila kupenda!
 
Back
Top Bottom