Makao makuu ya Halmashauri ya Singida Kaskazini

Makao makuu ya Halmashauri ya Singida Kaskazini

Kundya Rajabu

Member
Joined
Mar 22, 2018
Posts
7
Reaction score
0
Kumekuwa na vuta nikuvute ya wapi makao makuu ya halmashauri ya singida kaskazini yajengwe kati ya Ilongero na saga rumba. Kwa tabia ya wana singida kaskazini hili lisingekuwa tatizo kubwa wangepokea vyovyote vile.

Tatizo linakuja kwa kuwa wananchi wa Ilongero walishaaminishwa kuwa makao makuu yatakuwa ilongero.

Serikali kwa maana ya Mkuu wa Mkoa alikwenda kuwajulisha na akaagiza halmashauri ihamie huko, mapema halmashauri ilishaamua makao makuu yawe ilongero kabla ya kubadilika, CCM iliamua makao makuu yawe ilongero na wameshafungua ofisi ya wilaya, ofisi ya mbunge ipo ilongero.

Sasa unapowaambia watu makao makuu yanaenda sagarumba hawaelewi na hawataelewa. Jambo hili linafanywa ni rahisi lakini ni gumu maana Kwenye mioyo limeshapandizwa na chuki na mifarakano inaonekana japo wasiotaka kuona wanajifanya hawaoni.

Tatizo linabaki je watu kufarakana na kujenga chuki ni jambo dogo? Viongozi wa CCM na Serikali hasa ngazi ya mkoa lazima waketi pamoja haraka na kwa pamoja waende kuonana na Serikali kuu wakiwa na msimamo mmoja kisha warudi kukabiliana na wananchi.

Kujisikia, kujiona, hakupaswi kuwa sababu ya kupoteza upendo na msikamano baina ya wananchi na baina ya wananchi na Serikali yao.
 
Siku zote hayo maswala yanaamuliwa na siasa zilizopo badala kuangalia vitu vya kitalamu na kisomi inasikitisha sana
 
Hata yakiwa angani singida mmesahaulika sana mnakumbukwa kipindi cha kusaka kura tuu.Singida Lindi Kigoma Mtwara Katavi Rukwa Tabora
 
Wangeainisha kwanini ilongero na si Saga rumba basi naamini maamuzi sahihi yangefikiwa.. kosa kubwa ni kulifanya hili jambo kuwa la kisiasa na kuamuliwa na wanasiasa.
 
Ramani ya makao makuu ipo na imeandaliwa kitaalam na ni Sagarumba
Achana na siasa, Ilongero haifai.
Miaka michache ijayo itamezwa na manispaa, halafu muanze kuhaha kutafuta sehemu nyingine
 
Mkuu wa mkoa kwa maana ya serikali wamesema yaende Ilongero,CCM imesema yaende Ilongero,sasa nani mwingine anakataa? We unaasume watu wote wanaujua huo mgogoro.Siku nyingine fafanua vzr.

Ilongero imedumaa kimaendeleo ni ya mda mrefu lakini mabadiliko ni kidogo sana, Pia ipo ndani ya 30kms kutoka Singida mjini so iko ndani ya manispaa, kwa ajili ya kupanua maendeleo ya mkoa me naona yaende Saga rumba,Sio kila kitu kiwe Ilongero,kwanza kutakuwa na movement nzuri sana,kama Sagarumba itakuwa sub-town- Ilongero tayari ni sub town, ata vijana wa boda boda watakuwa bize kufanya kazi.
 
Ramani ya makao makuu ipo na imeandaliwa kitaalam na ni Sagarumba
Achana na siasa, Ilongero haifai.
Miaka michache ijayo itamezwa na manispaa, halafu muanze kuhaha kutafuta sehemu nyingine


Hiyo ndio poindi ya Msingi mkuu,Ila ukienda pale Ilongero ukatamka hayo maneno,kupigwa na wazee wa kwenye Gahawa sio kitu cha ajabu
 
Ramani ya makao makuu ipo na imeandaliwa kitaalam na ni Sagarumba
Achana na siasa, Ilongero haifai.
Miaka michache ijayo itamezwa na manispaa, halafu muanze kuhaha kutafuta sehemu nyingine
Haifai hata kidogo, tarafa ya miaka mingi iliyopita ila maendeleo yake yanazidiwa hata na vijiji vingi.
 
Back
Top Bottom