FabNXTzqEtcgazfbjjfo
JF-Expert Member
- Jan 17, 2019
- 1,579
- 2,131
- Thread starter
-
- #21
Jisaidieni Wenyewe kwa Wenyewe acheni kupeleka vitu Vinavyoenda Nufaisha Watu. Mtu kakutendea mema mpelekee huyo mtu zawadi na Mshukuru. Pesa zenu Zipelekeni kwa Wahitaji maana Wao ndio wanaona Kweli nimepewa na MtuMleta mada ameshauri fungu la kumi na shukurani zetu tuzipeleke moja kwa moja kwa wasio jiweza. Kanisani zinawanufaisha wenye uwezo kwa kufungua miradi isiyo na msaada kwa wenye uhitaji...
#tuamkekanisanitunapigwanakitukizitodeile
Bwana hapokei kitu maana Hana Mikono na Wala Mungu haitaji hayo wanayofanya. Wameandika hivyo ili Ukapigwe vizuri hukoHuu ujumbe uwafikie kina mwa. Nimewahi uliza hili vipi muumini masikini ananufaika vipi kiuchumi akijiunga na dhehubu lake. Inatakiwa madhehebu yaanzishe vyuo vya ujuzi kupitia sadaka na michango ya waumini kisha waumini masikini wasome wapate ujuzi Ili wazalishe kisha watoe sadaka. Nyumba za ibada zichunge watu kiroho na kiuchumi. Hata maandiko usema usiende nyumbani mwa Bwana mikono mitupu.
aiseeFIRST WE MUST COLONIZED OUR MIND
Kupitia binadamu unamuona Mungu.Bwana hapokei kitu maana Hana Mikono na Wala Mungu haitaji hayo wanayofanya. Wameandika hivyo ili Ukapigwe vizuri huko
Mungu haitaji Shule
Mungu haitaji Chuo
Mungu haitaji Benki
Mungu haitaji Majengo
Hayo yote Ni mahitaji yako wewe binadamu sasa Akuombea Sadaka yako ya Nini wakati hana Mahitaji ya Kibinadamu wanayofanya hao Wachungaji na Mapadri huko
Sasa Hizo sadaka Wanazosema Za Mingu ila Tunaona Zinafanya Mahitaji ya Kibinadamu
Hayo ni madhaifu ya wanadamuNijitolea kwa hali na mali kujenga shule moja ya kanisa mkoa fulani,Cha kushangaza nilimaliza chuo nilienda kuomba kazi pale NIKAKOSA nafasi walipewa Ndugu,na watoto wa wachungaji.Niliumia sana mpka leo nishabadili mfumo.
Na mimi nimepata udhaifu wa kutoaHayo ni madhaifu ya wanadamu
Hiki kiingereza chako dada kimefanana sana na cha yule the dedi "ankali" wa chattle.DAAH!!
FIRST WE MUST COLONIZED OUR MIND ,
ukweli mchungu aisee...
Ngoja nijitafakari na nichukue hatua....
Mkuu hii comment ndio imenileta wala sijasoma tittle. Kweli tupambane wanetu wasome hizo shule za gharama tunazojenga kwa michangoDAAH!!
FIRST WE MUST COLONIZED OUR MIND ,
ukweli mchungu aisee...
Ngoja nijitafakari na nichukue hatua....
Ni he/she? Nimefadhaika kwakweliMkuu hii comment ndio imenileta wala sijasoma tittle. Kweli tupambane wanetu wasome hizo shule za gharama tunazojenga kwa michango
Hali hiyo unayoisemea kama iko makanisani peke yake ila kwenye misikiti na mahekalu waumini wakitoa sadaka zinawarudia swala ni dogo tu ni kuachana na makanisa unajiunga huko kwingine ambapo ukitoa sadaka zitakuwa zinakurudia.Sasa Hivi Wasomi wanazidi kuwa Wengi wajinga Wanapungua Kwa Kasi na Serikali ndio hiyo Inazidi kujenga Madarasa hata Kama Haijui Itawapeleka wapi hao wasomi inaowajengea madarasa
Waumini wenu wanaokuja Makanisani (wale wenye Akili Timamu) Wanaona Jinsi gani Mnavyoyaendesha Makanisa Bila Wao Kufaidia Directly na hizo pesa Mnazosema Mnampelekea Mungu wakati ukweli ni Kwamba Hazifiki kwa Mungu bali mnazipigia Bajeti zenu za Kujinufaisha Au Kutengeneza Future Za Maisha Na Makanisa Yenu na Kuanzisha Miradi ambayo haimnufaishi Muumini Directly
Hakuna Siri kwamba Makanisa Hapa Nchini yamekuwa yakikusanya Michango.. Sadaka.. Shukrani..Harambee...Bahasha...Michango ya Redio...n.k Milioni na Bilioni kwa Mwaka Zinakusanywa Katika Makanisa. ila Msaada kwa Waumini kama Waumini husika haiendi Directly Kitu ambacho Kinasababisha hata Watu kuona Wanachotwa Mifukoni kwa Kisingizio cha Watabarikiwa au Wanamtolea Mungu
Mfano 1: Leo hii Muumini Apate Ugonjwa au Kuzeeka Asijiweze. Kanisa Linakaa Pembeni waumini ndio wachange Tena Pesa katika Jumuiya zao Na Pengine Asipoudhuria Misa au Jumuiya ingawa Ni Muumini Aliyekuwa Anachangia Anapotezewa kama Vile ni Mpagani tu
Katika Vikundi mbalimbali hapa Nchini Watu wanachanga Pesa Na wanauliza Zitawanufaisha Vipi wao kama Wao either wakiwa Wameugua Au Wakiwa Na Sherehe au Kifo. Kitu Ambacho waumini Ambao wamepumbazwa Wanashindwa Kuulizia Sadaka na Michango yao Kanisani itawasaidia nini Katika maisha Mmoja Mmoja.
Wameambiwa Sadaka Ni Za Mungu wakati Wakishazitoa Wanaona Majengo, viwanja, Mashule na Mahospitali yanajengwa bila Wao kuwapewa hata Asilimia moja Ya Mapato kutoka Katika Vyanzo hivyo.
Na Wakijaribu Kupeleka Watoto au Wao wenyewe wanakutana Na Bei ambayo hata Asiyemuumini Anatozwa hiyo hiyo Pesa haijalishi.
Fungukeni Macho Mnapigwa kwa Kivuli cha Mnamtolea Mungu. Hii Siri Baada ya Wengine Kuijua Wameamua na Wao kufungua makanisa kwa Kasi na Wanaendelea Kupiga Pesa maana Waumini akili timamu Hazipo Zimeshafubazwa kwa Kuambiwa Mungu ndie Anayetolewa
Wakati Huyo Mungu kwanza Haitaji kitu chochote kile Kutoka Kwako maana Hana Mapungufu kama Wewe ulivyo. Yeye kakamilika Haitaji sadaka wala Dhabihu wala Kitu Chochote kutoka Kwako maana Huwezi Mlipa Chochote.
Umekuwa Muumini Wa Muda Mrefu mpaka Unazeeka Hapo. Kanisa Lako halina hata Account ya Kusaidia Waumini wake wanapopatwa na Matatizo. Hivi hamuoni Mmechanganyikiwa na Mnaendeshwa Kunufaisha Watu. Kazi yako ni Kupeleka Fungu la Kumi kanisani ambalo wenye Nalo wanaenda Kuweka Mabati kwenye Miradi ya Kanisa
Jisaidieni Nyie kwa Nyie. Pelekeni Fungu la Kumi mnalotoa huko Kanisani kwa Watu wenye Mahitaji maana Mungu ndio kawaumba Hivyo ,msaidianeni Nyie kwa Nyie si kumpelekea Binadamu mwenzako Pesa Halafu Yeye anakuhadaa eti Unampa Mungu.
Chukueni Pesa zenu Pelekeni wagonjwa..Pelekeeni Watoto Yatima Wanautunzwa Na Watu..wasaidieni wazee walio majumbani Hawana Uwezo wa Kujipatia Vyakula Wakat kanisa lako hilo Likisubiri Afe ili Lije Limpe Upako Tu na Kumzika na likimkuta Haudhulii Misa Linamuacha
Mtu anapata Ajali ya Gari tena Unakuta ni Mahala pa Kijijini anaokolewa na Mwanakijiji hapo anamuwahisha Hospitali anapatiwa matibabu. Halafu kwa Sababu Akili timamu hana anachukua Pesa anaenda Kutoa Shukurani kwa Mchungaji au anapeleka Sadaka Ya Shukurani kanisani. Aliyemuokoa Kule Kijijini na Hospitali waliomtibu hawakumbuki
Hivi wewe unategemea utabarikiwa wewe. Au ndio mabalaa ya Maisha Yatakuandama. Yaani Yule Mwanakijiji aliyekutoa Kwenye Gari na Kukuokoa Hana Maana Na Sometimes alikuwa anajipitia Tu ..kwanini Usiende Kumpa Yule na Hao wa Hospitali waliokusaidia Ukapona Wangekuacha Je Huyo mungu wa Huko Kanisani na Kwa Mchungaji wako angekuja Kukupeleka hospitali. Tujitambue Wana Ndugu tumepotoshwa sana na Tumepotoka Kweli kweli
Tutumie Akili Timamu na Tumwabudu Mungu asiyetaka Vitu bali Aliyeumba Vitu vyote bila Yeye Kukutaka Kitu Chochote kile kutoka Kwako. Huyo ndio Mungu wa Kweli hana Mapungufu ya Kutaka Taka Vitu. Si Kama ukimnyima Anakuchukia na Kukupa Mabalaa hapa Duniani hakuna Mungu wa Hivyo
Asanteni
Ungeweka Zinavyorudi ungesaidiaHali hiyo unayoisemea kama iko makanisani peke yake ila kwenye misikiti na mahekalu waumini wakitoa sadaka zinawarudia swala ni dogo tu ni kuachana na makanisa unajiunga huko kwingine ambapo ukitoa sadaka zitakuwa zinakurudia.
Ukiona mtu anasononeka kama wewe ujue maisha yako ni magumu sana, usilalamikie kanisa lalamikia serikali kupandisha bei vitu, ndio jibu lako msisingizie makanisa coz miaka na miaka yapo hivyo hivyo wewe nani umezaliwa juzi tu eti unaliwa??!! Unajitafutia laana ungehama tu amia din nyingine ambayo haitoi sadakaNikawaza sana eti nitoe elfu 20 ya sadaka kanisani wakati ndugu yangu kule kijijini hali yake ngumu wengine wanasoma kwa tabu, nikasema alie juu anaona mpaka moyoni mwangu , basi nikatuma 18 kijijini elfu 2 ibaki kanisani na hii policy ni mpaka kesho nasaidia wenye uhitaji kwa hali na mali, Kanisani tupo wengi nisipotoa mimi atatoa mwingine.
Sema Wewe manufaa unayopata. Maana wengine Humu kuna Uwezekano ni Wachungaji huwezi penda madaUnaonesha unaposali wewe ndio pana majanga usijumlishe makanisa yote ndugu, hama ukiona uoni faida ya sadaka yako au amia kabisa din nyingine ambayo hawatoi sadaka
Ungeweka Zinavyorudi ungesaidia
Maisha yakiwapiga msikimbilie kusema makanisa, huo ni mfumuko wa bei shughulikeni na serikali zenu, au hamia din nyingine ambayo hawatoi sadakaKama jehanamu ipo kweli ! Walio na Makanisa wataungua sanaaaaa. Makanisa ni Biashara za watu wenye kuwatumia maskini na matajiri kujiongezea kipato. Yapo Makanisa machache sana viongozi wao wataiona mbingu. Haya ya walokole hakuna hata moja litasalia yataungua kama mti mkavu.. kwani ni wachafu kuliko mnyama....hawana tofauti na waganga wa kienyeji..
Badala mpambane na serikali zinazopandisha bei kila kitu eti mnapambana na kanisa ni dhambi yaani maisha yawachape eti sadaka tunaliwa??!!makanisa yapo miaka na miaka leo wewe umezaliwa juzi unatoa maneno kama hayo🙄🙄🙄 pambaneni na serikal zinazoongeza matozo hizo ndio zinafanya muone kanisa linakula hela mnatia aibu na umasikini wenu visadaka vyenu vitawapeleka wapi ??! Badilika wewe ni aibu hama amia fin ambayo haitoi sadaka usilalame tuuTukirudi kwenye fikira dini zote tulizo nazo ni dini za mchongo tuu ni vile tuu tumezaliwa na kukuta wakubwa wetu wanaabudu.
Fikiri kabla ya biashara ya utumwa watu walikua hawajui uislam africa.
Fikiri kabla ya kuja wazungu watu walikua hawajui ukristo africa.
Je walioishi kabla hukumu zao zikoje.
Jambo tafakarishi tunaomba kwa pamoja juu ya kinga fulani ila hilo hilo jambo lina kwenda tupata, mfano ufaulu, nafuu ya mgonjwa, ajari.
Kikubwa tuishi kwa kuwajari wenzetu, tutende yaliyo mema.
Mwenyewe hiki kiingereza changu sikielewi ...Hiki kiingereza chako dada kimefanana sana na cha yule the dedi "ankali" wa chattle.
Nyie bado mmepumbazwa. Hiyo serikali ingekuwa inakukata Kodi Halafu haijengi Barabara na Kukuwekea Huduma za Afya nahisi akili yako ingekaa sawa. Usisingizie watu wana Maisha magumu kwa Kuhisi hisi kwenye mada Hatujaweka Akaunti zetu za Benki na miradi ungeona Nani ni Masikini na Mwenye maisha Magumu.Ukiona mtu anasononeka kama wewe ujue maisha yako ni magumu sana, usilalamikie kanisa lalamikia serikali kupandisha bei vitu, ndio jibu lako msisingizie makanisa coz miaka na miaka yapo hivyo hivyo wewe nani umezaliwa juzi tu eti unaliwa??!! Unajitafutia laana ungehama tu amia din nyingine ambayo haitoi sadaka