mageuzi1992
JF-Expert Member
- Apr 9, 2010
- 2,503
- 252
SAKATA la wimbi la viongozi wa vyama vya siasa nchini kujiunga na Chadema, limeendelea mkoani hapa baada ya Makamu Mwenyekiti mstaafu wa TLP, Tanzania Bara, Westgate Rumambo kujiunga na chama hicho.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Babati hivi karibuni, Rumambo alisema amejiunga Chadema baada ya kubaini ndicho chama pekee kinachotetea wanyonge.
"Jamani hivi sasa TLP haina mvuto tena, kwa wana mageuzi nchini kimeonekana ni chama cha mtu mmoja kuliko Chadema ambacho kina malengo mazuri ya kukomboa Watanzania hasa wa ngazi ya chini," alisema Rumambo.
Alisema atatumia uzoefu wake wa harakati za kuongoza mageuzi nchini, kuhamasisha jamii na kuiimarisha Chadema mkoani hapa, ili uhuru na mabadiliko ya kweli vipatikane.
Katibu Mwenezi wa Chadema Babati Mjini, Zahir Musa alisema wanampokea kwa mikono miwili Rumambo kwani ni mtu makini mwenye uchungu na mabadiliko.
Musa alisema watashirikiana na Rumambo katika uendelezaji wa Chadema mkoani hapa na wanatarajia kupata ushirikiano mkubwa kutoka kwake kwani ana uzoefu wa uongozi wa mageuzi nchini.
"Tumempokea mwanachama mpya wa Chadema na tunatarajia kumkabidhi kadi ya Chadema na kuanza mapambano ya kuhakikisha mwaka 2015 tunachukua jimbo la Babati Mjini," alitamba Musa.
Rumambo hakukabidhi kadi yake ya TLP kwa madai kuwa ilishapotea muda mrefu na baadhi ya wafurukutwa wa Chadema mjini Babati walimpongeza kwa uamuzi wa kujiunga Chadema.
Walisema hivi sasa chama pekee cha upinzani kilicho na nia ya mabadiliko makini na chenye lengo la kuwafikisha wananchi wanakotaka ni Chadema pekee na ndiyo sababu vijana wengi wanaiunga mkono.
Source HabariLeo.
Chadema andaeni ANTIVIRUS ya kutosha kwa ajili ya ku-scann virus
Ajitokeze mtu TUPINGE hapa JF Kikwete ama kabla ama baada ya kustaafu atahamia Airtel
habari zinazo uza ni za cdm za ccm ni hasara tu.
...
Rumambo hakukabidhi kadi yake ya TLP kwa madai kuwa ilishapotea muda mrefu na baadhi ya wafurukutwa wa Chadema mjini Babati walimpongeza kwa uamuzi wa kujiunga Chadema.
...
Source HabariLeo.
CHADEMA, kemeeni upuuzi huo hapo kwenye red; misemo ya kimagamba. Misamiati ya magamba na makuwadi zao isiruhusiwe kuingizwa wala kuhusishwa kwa namna yoyote na mfumo wa ukombozi wa taifa letu.
Mkuu nafikiri 'wafurukutwa' ni msamiati wa CUF toka miaka ya 90 wakati CCM wanatumia 'wakereketwa', inaendana sambamba na Ngangari ya CUF na Ngunguri ya CCM enzi za Mahita. Wapenzi wa Chadema wanajulikana kama 'makamanda' ingawa kuna baadhi ya magazeti yanalazimisha kuwaita 'wafurukutwa'.Mkuu dudus,
Napenda nikuhakikishie kwamba huo msamiati ni msamiati wa CHADEMA. CCM wanatumia neno la Wakereketwa!
Mkuu dudus,
Napenda nikuhakikishie kwamba huo msamiati ni msamiati wa CHADEMA. CCM wanatumia neno la Wakereketwa!
Mkuu nafikiri 'wafurukutwa' ni msamiati wa CUF toka miaka ya 90 wakati CCM wanatumia 'wakereketwa', inaendana sambamba na Ngangari ya CUF na Ngunguri ya CCM enzi za Mahita. Wapenzi wa Chadema wanajulikana kama 'makamanda' ingawa kuna baadhi ya magazeti yanalazimisha kuwaita 'wafurukutwa'.
Kazi nzuri rafiki, nimejifunza misamiati kadhaa hapo!Nampongeza mtoa mada kutujuza ila naomba wanachadema waje ni misemo mpya tofauti na huo hapo kwenye BLUE (wafurukutwa!!!) hii ni misemo ya kimagamba tuje na misemo kama;
>Makamanda
> Wanaharakati
>Wapigania haki
> Wachapa kazi
>Viongozi bora
> Wanadira
> Wanamwongozo
> Watetezi wa wanyonge
> Wasemakweli daima
> Wakombozi wetu
> Watenda Haki
> Wawakilishi bora
> Majemedari
> Wachapa kazi
> Wanademokrasia wakweli
>Watetezi wa wanyonge