BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Date::12/23/2008
Makamba:Sijaenguliwa, ni utaratibu
Na Jackson Odoyo
Mwananchi
SIKU moja baada ya Kamati Kuu ya CCM kumuengua katibu Mkuu wake Yusufu Makamba kuongoza kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Mbeya Vijijini, Yusuf makamba amejitetea kuwa hajaenguliwa, bali huo ndio utaratibu mpya wa chama chake.
Makamba ndiye aliyekuwa kinara wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime ambako CCM iliangushwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), lakini sasa hatasimamia tena kampeni kwenye jimbo la Mbeya Vijijini baada ya Kamati Kuu ya CCM kuamua kuuachia mkoa jukumu hilo.
Kutokana na kushindwa kwa CCM kwenye jimbo la Tarime, Makamba, ambaye ni katibu mkuu wa chama hicho, alilaumiwa sana akidaiwa kushindwa kuzika tofauti zilizoibuka kwenye uchaguzi wa mwaka 2005, kutumia wapiga debe kutoka Dar es salaam ambao walihamia CCM kutoka vyama vya upinzani, na kushindwa kutumia vizuri vitendea kazi alivyopewa, ikiwa ni pamoja na helikopta mbili kwenye uchaguzi huo unaosemekana kuwa ulitumia fedha nyingi.
Lakini Makamba, akiongea na Mwananchi, alisema kuenguliwa kwake kunatokana na CCM kubadilishwa kwa utaratibu, akidai kuwa CCM ina utaratibu wake na mbinu nyingi za kufanya kampeni.
Huu uliotumika ni moja kati ya taratibu zetu na si kwamba nimeondolewa, alisema na kuongeza:
Mimi sijaondolewa ila mimi safari hii ni mwezeshaji katika kampeni hizo na kazi yangu ni kuangalia mahitaji muhimu wakati wa kampeni, mfano kamati ikiniambia niwapelekee flana nitapeleka; wakiniambia wanataka fedha, nitawapa; wakiniambiwa niwape usafiri wa magari ama helikopta, pia nitawapa.
Tarime tulikwenda na tukakaa huko kipindi chote cha kampeni na huo ulikuwa utaratibu wetu. Safari hii tutakwenda kusaidia kampeni na kurudi, huo pia ni utaratibu wa CCM.
"Mfano mimi ninakwenda Januari mbili, na Januari tatu tutakuwa na mkutano wa kamati ya siasa, January nne ni siku ya uzinduzi baada ya hapo nitaongoza kampeni hadi Januari saba na baadaye nitarejea Dar.
Alisema baada ya kurudi ataendelea na majukumu mengine ya kazi na akitaka kwenda Mbeya siku yoyote ataenda na kwamba hakuna wa kumzuia kwa sababu yeye ndiye msimamizi.
Makamba pia alirejea kauli yake kuwa alikubali kupokea lawama katika uchaguzi wa Tarime kwa sababu yeye ni kiongozi wa chama na kwamba endapo CCM ingeshinda katika uchaguzi huo, ni yeye ambaye angepongezwa.
Aliongeza kwamba hata katika uchaguzi huo wa Mbeya Vijijini, CCM ikishindwa tena yuko tayari kupokea lawama kwa kuwa ni kiongozi na kwamba wala hawezi kuwazuia wanachama kumlaumu.
Kulaumiwa ni kitu cha kawaida kwa kiongozi yeyote na ukiogopa lawama huwezi kuwa kiongozi," alisema.
Uchaguzi huo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Richard Nyaulawa kufariki dunia wiki chache zilizopita.
Katika Uchaguzi huo CCM imemsimamisha Mchangaji Luckson Mwanjale.
Makamba:Sijaenguliwa, ni utaratibu
Na Jackson Odoyo
Mwananchi
SIKU moja baada ya Kamati Kuu ya CCM kumuengua katibu Mkuu wake Yusufu Makamba kuongoza kampeni za uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Mbeya Vijijini, Yusuf makamba amejitetea kuwa hajaenguliwa, bali huo ndio utaratibu mpya wa chama chake.
Makamba ndiye aliyekuwa kinara wa kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime ambako CCM iliangushwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), lakini sasa hatasimamia tena kampeni kwenye jimbo la Mbeya Vijijini baada ya Kamati Kuu ya CCM kuamua kuuachia mkoa jukumu hilo.
Kutokana na kushindwa kwa CCM kwenye jimbo la Tarime, Makamba, ambaye ni katibu mkuu wa chama hicho, alilaumiwa sana akidaiwa kushindwa kuzika tofauti zilizoibuka kwenye uchaguzi wa mwaka 2005, kutumia wapiga debe kutoka Dar es salaam ambao walihamia CCM kutoka vyama vya upinzani, na kushindwa kutumia vizuri vitendea kazi alivyopewa, ikiwa ni pamoja na helikopta mbili kwenye uchaguzi huo unaosemekana kuwa ulitumia fedha nyingi.
Lakini Makamba, akiongea na Mwananchi, alisema kuenguliwa kwake kunatokana na CCM kubadilishwa kwa utaratibu, akidai kuwa CCM ina utaratibu wake na mbinu nyingi za kufanya kampeni.
Huu uliotumika ni moja kati ya taratibu zetu na si kwamba nimeondolewa, alisema na kuongeza:
Mimi sijaondolewa ila mimi safari hii ni mwezeshaji katika kampeni hizo na kazi yangu ni kuangalia mahitaji muhimu wakati wa kampeni, mfano kamati ikiniambia niwapelekee flana nitapeleka; wakiniambia wanataka fedha, nitawapa; wakiniambiwa niwape usafiri wa magari ama helikopta, pia nitawapa.
Tarime tulikwenda na tukakaa huko kipindi chote cha kampeni na huo ulikuwa utaratibu wetu. Safari hii tutakwenda kusaidia kampeni na kurudi, huo pia ni utaratibu wa CCM.
"Mfano mimi ninakwenda Januari mbili, na Januari tatu tutakuwa na mkutano wa kamati ya siasa, January nne ni siku ya uzinduzi baada ya hapo nitaongoza kampeni hadi Januari saba na baadaye nitarejea Dar.
Alisema baada ya kurudi ataendelea na majukumu mengine ya kazi na akitaka kwenda Mbeya siku yoyote ataenda na kwamba hakuna wa kumzuia kwa sababu yeye ndiye msimamizi.
Makamba pia alirejea kauli yake kuwa alikubali kupokea lawama katika uchaguzi wa Tarime kwa sababu yeye ni kiongozi wa chama na kwamba endapo CCM ingeshinda katika uchaguzi huo, ni yeye ambaye angepongezwa.
Aliongeza kwamba hata katika uchaguzi huo wa Mbeya Vijijini, CCM ikishindwa tena yuko tayari kupokea lawama kwa kuwa ni kiongozi na kwamba wala hawezi kuwazuia wanachama kumlaumu.
Kulaumiwa ni kitu cha kawaida kwa kiongozi yeyote na ukiogopa lawama huwezi kuwa kiongozi," alisema.
Uchaguzi huo unafanyika baada ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Richard Nyaulawa kufariki dunia wiki chache zilizopita.
Katika Uchaguzi huo CCM imemsimamisha Mchangaji Luckson Mwanjale.