Makamba fungua kesi ya uharifu wa mtandao au resign

2kimo

JF-Expert Member
Jan 23, 2014
2,029
2,071
Mod naomba uitafutie mahali sahihi pa kuiweka hii thread!

Kwa hali ilivyo sasa, mh January ameshachafuliwa vya kutosha kwa kuhusishwa na kashfa kubwa ya rushwa na matumizi mabaya ya ofisi!
Kwa kauli yake January amekiri kuwepo kwa taarifa za clips zinazomchafua lkn amedai kuwa hizo ni propaganda na ni uzushi wa kutengeneza!
Kingine January Amekiri kuwepo kwa mtaliano tapeli na anayejihusisha na madawa ya kulevya!
Sasa waziri wetu mtukufu, kama mtu ametengeneza clips za kukuchafua na unajua anapopatikana, please mreport polisi ili sheria ichukue mkondo wake!
Kama tukikumbuka vema, ulisimamia kwa nguvu upitishwaji wa sheria hii, unaijua vema na unajua kuwa ndio njia pekee ya kuiweka salama hadhi yako! Kimantiki mtu hawezi kumsamehe yeyote anayefanya makusudi kuchafua hadhi yake, lkn hapa heshima, dhamana na uwekezaji wako wote katika siasa unaweza kuangamia! Kwa yeyote aliyeifanya kazi ya kuitengeneza clip ile ameamua kukuangamiza na upotee kabisa! Kwa heshima yako na serikali yako ya awamu ya 5, hebu Fanya mambo makubwa miongoni mwa haya!
1. Mshtaki mtaliano kwa kukupandikizia uongo
2. Kuwa muungwana, kubali na resign ujenge heshima ya serikali yako

Option 2 ni ngumu sana lkn ni salama zaidi. Hadi sasa najua raisi wako atakuwa na wakati mgumu zaidi, chama chako kitakuwa kimeumia, familia yako na mashabiki wako watakuwa wanaumia pia. Ila option namba 1 ina apply tu kama hukuhusika kabisa na hayo madeal haramu! Ni very tricky kwa kuwa somehow umekiri kujihusisha na huyo mzungu hata kama ingekuwa karne moja nyuma bado shutuma zingekuwa na value kwa kuwa uliyafanya yote ukiwa kiongozi na hata sasa wewe bado ni kiongozi!
Ndio ubinadamu, huwa tunateleza na yanapoturudia huja na impact kubwa sana!
 
Back
Top Bottom