Majuto ni Mjukuu huja Baadae

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
2.JPG


A/allaykum ndugu zangu wa Kizanzibar? Nipenda kutowa shukukrani zangu hizi na wingi wa pongezi kwa wale wenye kuiteteaZanzibar na Wazanzibar kwa jumla zidi ya maonevu, mateso na Zulma inayofanyiwaZanzibar na watu wake katika mwevuli huu wa Muungano.
Kuna waliokwisha kutanabahi kuwa binadamu mbele ya Allah nikiumbe zaofu tu na anaweza kumfanya vyovyote atakavy Allah.
Na kuna ambao baado hawajatanabahi na baado wanaendeleza vitendo vya uovu nakuto kujikubalisha kufuata njia ya haki na njia yenye kuwaletea usalama hukotwendako ambako ni mbele ya Allah.
Tukija katika hali ya nchi yetu ya Zanzibar , takribani %99ya wakazi wa nchi ya Zanzibar ni waislamu kiasili ya Babu na Bibi lakinivitendo vinavyofanywa na viongozi wetu wa nchi havilingani na Dini yetu na milaza Wazanzibar wenyewe tulivyo.
Kuna vitendo vya kinyama na wenye kufanya hivyo wamesahau kabisa kuwa M/mungu yupo na yupomilele na yeye hana haraka na hukumu zake ispokuwa sisi binadamu ndio tunaharaka kwa vile tuna ukomo wa maisha yetu.
M/mungu kaweka msamaha kwa wale wenye kufanya makosa nabaadae kutanabakhi na kuomba msamaha(taubat nasuha ).
Sasa kuna njia nyingi za kuomba msamaha na mwenyewe M/munguakakukubalia na kukupokea, kwanza ni ile ya kumkera yeye moja kwa mmoja hioinahitaji kumuomba yeye mwenyewe na kuonyesha kweli umetanabahi na unajuta kwa ulilo fanya?.
Na hii mara nyingi inakwendana na Kafara yani kutowa kitu aukufanya kitu ili kumridhisha allah kuwa kweli unahitaji kusamehewa kama vipi.
Kwa mfano kama una uwezo kidogo kufanya (Sadagah Jariyah),hii nisawa na kuonyesha kuwa kweli umeingia katika kufuta mambo ulio yafanya nakuchangia heri zako ziendelee kuwa juu na kufuta mizani ele ya maasi uliofanya.
Mfano mwengine wa kuomba radhi kwa makosa ulio fanya ni yaleya kumkosa mtu fulani au jamii ya watu, sasa hili la jamii ndio maada yetu yaleo hapa?.
Hili lakukosa jamii ndilo linalo fanyika hapa kwetu Zanzibardhidi ya viongozi wetu kuwa wadilifu mbele ya jamii na kusababisha maafa kwajamii wanayo isimamia na kuiongoza?.
Kuna vitendo vingi tu viongozi wetu wamezitia jamii na kwachuki za kisiasa ambazo zilisababisha maafa na vitendo vya hujuma hapa kwetuZanzibar na jamii yake.
Tushukuwe mfano moja hai wa Rais wetu alopita katika awamuyake Mh alokuwa akijita Kamandoo Mh Salmini Bin Amour.
Huyu jamaa Baado anateseka na baado hajatanabahi kuwa hivisasa moto wake unazima kama vile Karabai iloishiwa na mafuta.
Na Baado hajajitokezakwa jamii alio ikosea na kuiparaganya na kuisababisha maafa na kujenga misingi ambayo haiendani na madili yakislamu na utamaduni wetu wa kizanzibar.
Kuna viongozi wengi tayari wameshajitokeza katika hadhara zawatu na kuomba radhi na ili kujisafasha kuwa wendako ni karibu kumekaribiakuliko waliko toka.
Kwa jamii yetu ya Kizanzibar na imani zetu za kustahamilianana kuvumiliana wengi rudisha imani yanafsi zao na kumshukuru Allah ,sasa hii ndio kumkosea mtu/Jamii na M/munguakakukubali kwa vile umerudi kwa jamii yenyewe ulio ikosa.
Sasa Wazanzibar tumulize huyu Rais wetu Kamandoo Mh Salminiamour jee maafa alio tupandikizia na kututia na kujenga misingi ya fitna ambayomizizi yake mpaka leo inaendelea ,jee karudi kwa jamii ya kizanzibar kujikoshana kujisafisha?.
Mh Salmin ana mfano wa pekee katika nchi hii yetu ya watu waZanzibar, kaziparakanya familia nyingi kwa kupandikiza mbegu ya chuki ya Upemba na Unguja,Ukaskazini naukusini,kuwafukuza kazi watu wa asili fulani, kuvunja majumba na vitendi vingi tu vya unyanyasaji katikajamii yetu iliokuwa na uchirikiano na upendo .
Na baaya dhaidi alilo lifanya ambalo litamla na kumtafunahuko endako ni kujiwekea (SADAGAH TU JARIYAh) yake mwenyewe, kujenga misingi yana mbegu za kupandikiza chuki katika jamii kama vile –
Kutengeza maskani za Wahuni (KISONGE) kutuletea Masheha watuwenye itikadi mmoja tu ya Chuki na Ubaya wa Manyanyaso katika jamii na kuletambegu ya ubaguzi kwenye jamii ya Watu waZanzibar.
Hii ndio Sadagah tu Jariyah ya Mh Salmini alio jitengenezeakwa makazi yake ya huko usoni.
Hivi sasa alivyo vipanda ndio vinakuwa na vinamea na watukuvu na kutumia matunda yake,leo utaona matusi yanayo andikwa na kubandikwa Katika Maskani ya KISONGE basi unashangazwana kujuwa kuwa Uko Zanzibar katika Kisiwa Cha amani au uko wapi?.
Watu wenye heshima katika jamii yetu wanatukanwa nakuzalilishwa bila ya hatua yoyote kushukuliwa na Serekali ya Mh Shein, ikiwa niUhuru wa Kuzungumza ndio, lakini sio uhuru wakulanika na kuvunja maadili yetuna mila zetu za Jamii ya kizanzibari.
Mh Rais wetu Shein hua unahubiri siku zote kuwa Wazanzibartulinde Amani ya nchi yetu ,ambayo tuliipata kwa harama kubwa na atakaye vunjaamani yoyote tuta mzibiti na Kumshuhulikia kwa vile.
Jee wale KISONGE wanalolifanya ni nini Mh Rais Shein kama sikuhatarisha amani ya nchi iliopo? Au na wewe ni ndumi la kuwili , usisahau kuwakuna adhabu yenye kumiza Mbele ya Allah na Mchunga hulizwa alicho kichunga.
Nchi hii wewe ndio Rais wa wazanzibar wote na ni mchungazidi yao kwa hio ,madamu umekubali kuwa mchungaji na ukubali zima mbele ya Allahwala usiangukie upande moja hata kama ni mfuasi wa ccm, lakini ujuwe kuwa nirais wa wazanzibar wote, sio wa ccm tu au cuf ni wawate wenye vyama na wasio navyama.
 
Dah hata usoni hawatazamani,, komandoo kweli hata mie wa Bara utawala wake haukunifurahisha kabisa! jamaa alikuwa katili sana sasa anavuna mabua hahahahah
 
Mimi siyo Muislamu lakini wakati matokeo ya Uchaguzi yanatangazwa nikuwa najua wazi wazi kuwa CCM haikushinda, Nilitegemea Aman kama "Muislam safi" akatae kuapishwa kama Rais kwani alijua fika kuwa hakushinda. Tangu hapo nilitoa imani kwa mtu kuitwa Muislam au Mkristu safi. hata leo huwa nasema Huwezi kujiita Muslamu safi au Mkristu safi ukawa ndani ya CCM.
 
nataka tanganyika yetu nimechoka kuona tunavyonyonywa na kisiwa kidogo chenye idadi ndogo ya watu kuliko hata mji tu wa morogoro
 
Mimi siyo Muislamu lakini wakati matokeo ya Uchaguzi yanatangazwa nikuwa najua wazi wazi kuwa CCM haikushinda, Nilitegemea Aman kama "Muislam safi" akatae kuapishwa kama Rais kwani alijua fika kuwa hakushinda. Tangu hapo nilitoa imani kwa mtu kuitwa Muislam au Mkristu safi. hata leo huwa nasema Huwezi kujiita Muslamu safi au Mkristu safi ukawa ndani ya CCM.
HUO NDIO UKWELI. ndani ya ccm watu hupanga nani awe kiongozi mezani na kura huwa ni kiini macho tu.viongozi wengi ndani ya ccm ni washirikina wakubwa na kwa macho yangu nimewaona wengi tu tena wengine wakijinasibu kuwa ni washika dini sana.huko ccm hakuna msafi hata mmoja tofauti na chama cha CHADEMA kila aliye shinda uongozi wa umma ni kwa nguvu ya MUNGUna watu wameidhinisha alilo litaka MUNGU na ndio maana watu wanawakubali sana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom