Majipu yataondoka na CCM

ccm ikifa nchi inaweza ikapiga hatua,

lakini kama ccm bado ipo hai,hata tuletewe malaika nchi hii itabaki palepale
 
\
\
boya kabisa!

Ni habari yenye lengo la kufitinisha! N mwaandishi anaonyesha wazi kufanya kazi hii maluumu kwa kutumwa na watu maalumu, na hasa ili kujenga hofu kwa mtumbuaji!

Kuna wanachama na baadhi ya viongozi waandamizi wanajiona wao ndio CCM na kwamba kuguswa wao ama ufisadi wao, ni kukigusa chama! CCM siyo mtu ama genge la watu hasa wahuni na wahujumu wa uchumi!

CCM kimepoteza wanachama wengi na hasa imani kwa wananchi kutokana na wahuni wachache wanaojiona wenyewe ndio Chama Cha Mapinduzi! Na imlikuwa ni vigumu sana kukinadi chama kwa jinis vile kilinuka katika uchaguzi uliopita! Wananchi walikichoka!

Ili kukiimarisha Chama, ni lazima haki itendeke na Haki hiyo ionekane inatendeka mbele ya jamii kwa kuwaondoa wale woote ambao jamii inawajua bila shaka yeyote ni mafisadi! Hatua anazozichukua Maguli ni njema kabisa, na zimedhoofisha upinzani bila ya siasa yeyote!

Acha kutishia watu Gurumo kwa vipande vya dinari ulivyochukua, hakuna aliemkuu kuliko chama, tumuunge Magufuli mkono kwa kumsadia na siyo kumkatisha tamaa kila uchwao kwa ngonjera zenje sumu ya maneno matamu!

Viva JPM, wanaopiga kelele ni wote wale wanao hofia nafsi na matumbo yao!
 
Chama cha MAJIPU
 
magufuli si mtu wa maneno,tusubiri na wewe ukae usubiri atakayoyafanya,tuombe mungu uzima............
 
Ndio mtindo wa ccm?

Ni wakina nani waliokuwa wanapiga kelele bungeni kuwa, "China huwa wanawanyonga mafisadi, na tunaomba rais asiwaonee haya mafisadi ikiwezekana awanyonge"..........Sasa hivi wanatumbuliwa, wanasema "Rais haangalii hakiza binadamu!"

Ukiibu hapo juu, ntajibu kama huo ni mtindo wa CCM au la!
 
Mpaka mahakama iwadhibitishe kua nimafisadi siyo kukurupuka
 


Ungekuwa na chembe ya AKILI ungeshambulia hoja ya Ngurumo badala ya kumshambulia Ngurumo as a person.

SIMPLE MINDS DISCUSS PEOPLES
 
Uboya mtupu, we sema hiv "magufuli endelea kutumbua mafisadi yaje kwetu upinzani" na mtawasomba kwel kwel, mpaka boss atoke kuchunga n'gombe
Ficha upumbavu wako jadili hoja iliyopo, Kuna kashfa nyingi za ufisadi rada, mikataba ya madini, IPTL, EPA, ESCROW, meremeta, UDA na nyinginezo kibao zilizotengenezwa na kukumbatiwa na kulelewa na CCM, wahusika wamehamia upinzani?

Magufuli mwenyewe jipu, na jipu kuu Riz 1na babaake hathubutu kuingia kwenye anga zao, mmebakia majuha ya lumumba na buku 7 kukariri upuuzi
 
Upinzani umedhoofika kivipi? Hadi leo rejea kauli ya prof Tibaijuka (ingawa wengine hawataki kujadili kauli yake bali wanamjadili yeye binafsi ) kuwa Magufuli anakamua nyama na si majipu.

Moyo wa majipu unajulikana, ni viongozi wakuu wa CCM, maana katika kila ufisadi mkubwa nyuma yuko mwanasiasa nguli wa CCM, Magufuli anajua ila anatafuta umaarufu kwa watumishi wa serikali.

Tumbua waliofanya utapeli wa IPTL wale waliofungua kampuni ya simba trust ya Australia wanaohusika na familia ya mzee wa Msoga.

Tumbua waliojigawia shirika la UDA kimagumashi.

Bila hivyo tuacheni wenye jicho la tatu tusiovutwa na ushabiki bali tu nasubiria majipu na si nyama
 
Mwili wa binadamu una sehemu tofauti tofauti.
Kuna sehemu rahisi hata kuzikata na kuzitoa bila kuleta athari kubwa za kiafya.

Jipu linapotokea kwenye mwili wa binadamu linauma sana. Maumivu yanakua makali zaidi kulingana na sehemu ya mwili lilipotokea.
Kuna baadhi ya sehemu za mwili wa binadamu zinauma sana zinapotokwa na jipu.
Mfano jipu likitokea Puani,kwenye sikio, sehemu za siri, tumboni ,kwenye jicho n.k. linauma sana sana.

Jipu linalotokea sehemu inayouma sana pia linakua ni vigumu kulitumbua kwa haraka bila utaalam wa ziada. Ukicheza nalo linaleta madhara makubwa zaidi.

Mfano likitokea jipu mkononi au kwenye paja la mguu inakua ni rahisi kulitumbua ukilinganisha na sehemu kama kwenye sikio.

Ni kweli kuwa Magufuli bado hajatumbua majipu yaliyoliyolisababishia taifa hili maumivu makali sana sana. Lakini hiyo isiwe sababu ya kukejeli kazi aliyoianza ya kutumbua baadhi ya majipu yaliyoko sehemu nyepesi kutumbua bila madhara makubwa.

Kazi aliyoianza ni nzuri lakini pia inapunguza idadi ya majipu yaliyoko kwenye taifa letu.
Ninaimani kuwa mwisho wa yote itabidi tu atumbue na yale majipu yanayolisababishia taifa letu maumivu makali sana. Asipofanya hivyo maumivu haya yataendelea kwa muda mrefu.

Ni lazima majipu yote yatumbuliwe bila kujali umuhimu wao kwenye kununua kura za wabunge wa CCM kupata ushindi wa kishindo bungeni. Hatuhitaji kuongozwa na bunge la wala rushwa. Wabunge na madiwani wengi wa CCM ni matokeo ya majipu na ufisadi wa kupata fedha za kununua nafasi hizo za uwakilishi hasa pale wasipokubalika.

Ni vizuri Magufuli akasafisha wale wakuu wa taasisi za umma na wafanyabiashara wanaotumiwa na mafisadi ndani ya vyama vya siasa ili kupata ubunge na baadae uwaziri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…