Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,802
- 50,393
Kuna chereko chereko nyingi sana toka kwa wananchi wengi kuhusu matendo ya Rais Magufuli anapoonesha kwamba anapambana na ubadhirifu na ufisadi uliotamalaki ndani ya Serikali. Matendo hayo ambayo yeye mwenyewe Rais ameyabatiza jina la "kutumbua majipu" na pia kujipa kazi ya "mtumbua majipu" bila shaka ni muendelezo wa kauli mbiu yake ya "Hapa kazi tu".
Lakini swali la kujiuliza hayo yanayoitwa majipu yalitokeaje tokeaje mpaka yakafika kuja kutumbuliwa na Magufuli? Maana majipu chanzo chake ni uchafu au mchafuko wa ndani ya mwili, kwa haya majipu anayotumbua Magufuli chanzo chake ni nini hasa?
Je chanzo chake ni uzembe wa Uongozi uliopita chini ya Marais Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete au chanzo ni Mfumo wa uendeshaji wa mambo ndani ya serikali, au chanzo kikuu ni Chama kilichotoa Marais Kabla ya Magufuli kuwa Rais?
Majipu yakitumbuliwa bila chanzo chake kushughulikiwa au kujulikana huko mbele ya safari si yatarudi tena? Majipu ni watu au ni mfumo unaoleta majipu? Kwa mfano yule Mkurugenzi wa Muhimbili aliyeomba hela za kukarabati mashine za CT Scan na hakupewa, yeye ndiye jipu au waliomnyima hela ndiyo jipu?
Lakini swali la kujiuliza hayo yanayoitwa majipu yalitokeaje tokeaje mpaka yakafika kuja kutumbuliwa na Magufuli? Maana majipu chanzo chake ni uchafu au mchafuko wa ndani ya mwili, kwa haya majipu anayotumbua Magufuli chanzo chake ni nini hasa?
Je chanzo chake ni uzembe wa Uongozi uliopita chini ya Marais Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete au chanzo ni Mfumo wa uendeshaji wa mambo ndani ya serikali, au chanzo kikuu ni Chama kilichotoa Marais Kabla ya Magufuli kuwa Rais?
Majipu yakitumbuliwa bila chanzo chake kushughulikiwa au kujulikana huko mbele ya safari si yatarudi tena? Majipu ni watu au ni mfumo unaoleta majipu? Kwa mfano yule Mkurugenzi wa Muhimbili aliyeomba hela za kukarabati mashine za CT Scan na hakupewa, yeye ndiye jipu au waliomnyima hela ndiyo jipu?