Majibu yangu kwa Eric Shigongo kuhusu umaskini

Anthony10

Member
Sep 13, 2016
91
102
Kutoka insta, Shigongo anadai kwamba umaskini ni laana ,na mafundisho ya dini yanasababisha umaskini huo kwa wakristo..

Majibu yangu

Erick Shigongo sio watu wote wanaweza kuwa na fedha za kutosha kama unavyodhani ,hakuna mahali katika biblia panaposemwa kwamba "Umaskini ni laana" hakuna kitu kama hicho ..

Yesu alisema Yohana 12 : 8 - kwa maana maskini mnao sikuzote pamoja nanyi; bali mimi hamnami sikuzote...Na

Yakobo 1 : 27 -inasema kuwa dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu baba ni hii, kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa. Na Yesu anaeleza kwamba kadiri tunavyowajali maskini ni kama tunamtendea yeye Mathayo 25 : 35 - kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha.

Erick Shigongo mungu huwabariki watu ili wawe mibaraka(mifereji ya kuwabariki) wengine, kama wenye fedha wakishindwa kuwahudumia wengine ambao ni maskini hawa ndio fedha huwa laaana kwao, lakini pia suala sio pesa au mtu kuwa na utajiri, bali suala ni namna gani unavyopata hizi pesa kama una fedha nyingi sana na njia uliyotumia kuzipata haipatani na njia ya mungu hiyo ndiyo laaana, na kwa kuwa wenye fedha wamejawa na kiburi na dharau, Yesu akasema "Ni vyepesi ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu" luka 18 : 25


Aidha kusema kuwa mafundisho ya dini yanawafanya watu kuwa maskini hiyo nayo sio kweli, hakuna fundisho la dini ya kikristo linasema watu wawe wazembe Mungu mwenyewe alisema

Oka 20:8-11 ....... Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote; lakini siku ya saba ni sabato ya bwana, Mungu wako.

Na mwenye hekima asema:Mithali 10 : 4 - atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini; bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.

Cha kufahamu ni kwamba :Yesu hakuja dunia ili kuwafanya watu wawe matajiri au maskini bali alikuja kuwatoa katika dimbwi la dhambi, mchakato wa kutolewa katika dimbwi hili wakati mwingine una maumivu makali ikiwa ni pamoja na umaskini kutegemea na mtu

Utajili wako shingongo wa kuuza magazeti ya udaku ? Kuchezesha kamali watu ,hivi ndivyo vitu vya kutambia watu ?

Ongeza ufahamu hapa

Luka 16 : 19 - akasema, palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.

Luka 16 : 20 - na maskini mmoja, jina lake lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi

Luka 16 : 21 - naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.
Luka 16 : 22 - ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

Luka 16 : 23 - basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

Luka 16 : 24 - akalia, akasema, ee baba ibrahimu, nihurumie, umtume lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

Luka 16 : 25 - Ibrahimu akasema, mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
 
Hata kwenye vitabu vya dini nilikuwa na mabwana na watwana lkn sijaona sehem ulofa ni laana
 
Haujamuelewa wapi,,? Kasema umasikini ni laana (jambo ambalo ni kweli) hajasema kuwa watu masikini ni watu waliolaaniwa,,
 
umasikini Laana??

utajuaje kama umelaaniwa?

kuna sehemu ya kwenda kutoa iyo laana??
 
Haujamuelewa wapi,,? Kasema umasikini ni laana (jambo ambalo ni kweli) hajasema kuwa watu masikini ni watu waliolaaniwa,,
Kwa hiyo watu masikini hawajalaaniwa ila wana laana tu?

Katika simulizi zake Eric uwa anasema kwamba wazazi wake walikuwa masikini. Kwa mantiki hiyo wazazi wake kwa kuwa na umasikini walikuwa na laana japo hawakulaaniwa? Kiswahili kigumu.
 
Kwa hiyo watu masikini hawajalaaniwa ila wana laana tu?

Katika simulizi zake Eric uwa anasema kwamba wazazi wake walikuwa masikini. Kwa mantiki hiyo wazazi wake kwa kuwa na umasikini walikuwa na laana japo hawakulaaniwa? Kiswahili kigumu.
Wala sio ugumu wa kiswahili ni ugumu wako katika kuelewa, umasikini ni laana ndio,, japo watu masikini hawajalaaniwa na ndio maana wapo waliokuwa masikini na wametajirika sana, je, na wao walikuwa na laana,,? Kama jibu ni ndio nani aliyewatakasa na laana ikawaondoka,?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Umasukuni ni laana ndio. Lakini haina maana maskini amelaaniwa. Ukisoma kwenye Biblia utatambua kwamba Mungu hataki sisi tuwe maskini.

2 Kor 8:9 inasema '...
Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Kumb 8:18 inasema '....... Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri....'

Kuna mistari mingine kadhaa inayoonyesha kwamba utajiri ni baraka kutoka kwa Mungu
na kwamba Mungu hataki sisi tuwe maskini
 
Umasukuni ni laana ndio. Lakini haina maana maskini amelaaniwa. Ukisoma kwenye Biblia utatambua kwamba Mungu hataki sisi tuwe maskini.

2 Kor 8:9 inasema '...
Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.

Kumb 8:18 inasema '....... Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri....'

Kuna mistari mingine kadhaa inayoonyesha kwamba utajiri ni baraka kutoka kwa Mungu
na kwamba Mungu hataki sisi tuwe maskini
Hebu nipe andiko moja linalosema kuwa umaskini NI laana (laaana kutoka Kwa Nani ??)

Mkuu Acha kujichanganya kama UMASKINI NI laana basi maskini wamelaaaniwa ni heaabu ya darasa la pili...huwezi kusema kuwa UMASKINI NI laana LAKINI maskini hajalaaniwa (huu ni uvivu wa connect dots... )
 
Mi nakubali kweli Umasikini ni Laana lakini Masikini sio Laana.

Mfano.
Je, wewe ukiwa na kitu kilicholaaniwa kinakufanya wewe mmiliki wa hicho kitu kulaaniwa pia.
Jibu Hapana. Laana inabaki kwenye hicho kitu unachomiliki.

Ndio maana Sentensi inasema, "Umasikini ni Laana" na sio "Masikini ni làana".
 
Ana utajiri gani Shigongo? Kama ada tu ya chuo imemshinda, akaenda kupanga que ili apate mkopo? Ni ulimbukeni na ushamba tu, kuigeuza dini na umaskini.
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Kwa hiyo watu masikini hawajalaaniwa ila wana laana tu?

Katika simulizi zake Eric uwa anasema kwamba wazazi wake walikuwa masikini. Kwa mantiki hiyo wazazi wake kwa kuwa na umasikini walikuwa na laana japo hawakulaaniwa? Kiswahili kigumu.
Hata yeye bado maskini tu!!
 
Kwa hiyo watu masikini hawajalaaniwa ila wana laana tu?

Katika simulizi zake Eric uwa anasema kwamba wazazi wake walikuwa masikini. Kwa mantiki hiyo wazazi wake kwa kuwa na umasikini walikuwa na laana japo hawakulaaniwa? Kiswahili kigumu.
Sorry kinyume cha umaskini ni utajiri,kinyume cha maskini ni TAJIRI.So SHIGONGO ni TAJIRI?
 
Umaskini ni nini? Unaufafanua vp? Tatizo watu wamefumbwa zaidi na starehe za dunia na ndio maana hii minabii uchwara kila siku inapotosha watu kwa kuhubiri utajiri wa vitu badala ya utajiri wA nafsi (rohoni) ina haja gani kuwa na material things lakini rohoni unateseka?
 
Back
Top Bottom