Maisha ya Mwanza

Mungu Mweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
1,474
Reaction score
1,086
Wadau mimi ni mtumishi wa umma sasa nimehamishiwa jiji la Mwanza nina mke na mtoto na mfanyakazi. Ishu ni kwamba ni sehemu gani naweza kupata nyumba au appartiment kwa bei nzuri na gharama imekaaje kama napanga nyumba nzima.
 
Kwahiyo pesa usisumbue madarali hapa mjini we nenda kisesa au Buhongwa au Ngombe kule utapata kivyepesi
 
Kuanzia 120000-50

Kwanza karibu rocky city.
Sasa hiyo hela kwa nyumba nadhani unaweza kupata nyumba ya chumba na sebure 'self' ila itakuwa maeneo ya nje kidogo na mji.
Jaribu kutafuta maeneo ya Igoma, Nyakato, Nyasaka, Kilimahewa, Pasiansi, Mkuyuni au Nyegezi.

Usihofu nyumba utapata tu ila inataka uvumilivu kidogo.
 
Hapana msimtishe bana, Nyumba atapata tena nzuri zipo za kutosha Kama bado hujapata ni pm namba yako nitakusaidia kupata Nyumba nzuri na ya kisasa. Mwanza hii yote ni yangu.
 
Ofisi ipo wapi? e.g huwezi kuishi nyasaka wakati ofisi ipo nyegezi, etc. be careful
 
Ahsanteni sana wadau kwa michango yenu kwani imenipa picha halisi ya jiji la Mwanza. Kuna wadau wameniuliza kwa nini naitwa MUNGU MWEUSI, sababu kubwa ni kwamba wazungu au watu wengi hata Waafrika, wa Asia, American wanaamini Mungu ni mweupe kutokana na historia ya vitabu vya dini lakini mimi naamini Mungu ni mweusi kwa sababu ya uwepo wetu watu weusi.
 

kwanza anatakiwa kujua anafanyia kazi wapi! Maana hilo litaweza kufanya ajue umbali na gharama za usafiri, maana anaweza kupanga nyumba mbali ambapo ukiangalia gharama za usafiri ni bora hata angepanga karibu kwa gharama zaid!!
 
Wadau mimi ni mtumishi wa umma sasa nimehamishiwa jiji la mwanza nina mke na mtoto na mfanyakazi. Ishu ni kwamba ni sehemu gani naweza kupata nyumba au appartiment kwa bei nzuri na gharama imekaaje kama napanga nyumba nzima.

kama una laki sita nyumba IPO mkolani INA kila kitu na ac zake mbili INA fence na CCTV camera
 
Karibu mkuu nipo nyansaka msumbiji pia na rafikizangu wengi tu madalali so ni pm tusaidiane
 
kahtaan, ile nyumba ya baba yako almarhum Ilunga imepata wapangaji?
 
Last edited by a moderator:
kahtaan, ile nyumba ya baba yako almarhum Ilunga imepata wapangaji?

Mke wake si yupo jamani! Haya mgeni karibu mwanza, naamini utafurahia uwepo wako mwanza
 
Last edited by a moderator:
Ni PM Kuna nyumba nzurii sana natumai unaipenda mitaa ya nyamanoro na ibungilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…