Maisha ya mwanadamu ni hatma

Maisha ya mwanadamu ni hatma

mjizu123

JF-Expert Member
Joined
Mar 19, 2016
Posts
349
Reaction score
370
MAISHA YA MWANADAMU NI HATMA

Ulishawahi kujiuliza kwamba Maisha yetu yote ni hatma iliyopangwa au tunaishi kwa muongozo wa akili zetu kwa kufuata kanuni za maisha yetu.

Ni kawaida sana kwa watu wengi kusema kuwa kila kitu maishani kimepangwa na kila mwanadamu ataishi kwa mipango yake kwa kadri vile alivyopangiwa ila bado kwa kutumia hoja hii aina ya watu hawa huja kupingana nayo katika mambo mengine.

Kama kila kitu duniani kimepangwa basi hata ulimwengu umepangwa na unajiendesha kwa kadri ya mipango yake na maamrisho yake yote na ndio maana nyota huzaliwa kila baada ya muda na ndio maana hutanuka kwa nguvu ya ajabu na ndio maana kila sayari zipo katika mwendo wake na Mvua zinanyesha kila baada ya wingu zito kutanda angani na baadae kuyeyuka na kuanguka kama mvua.

Je, unakubaliana na Usemi huu?
 
Tunachochagua kwa akili zetu ni kukubali au kukataa njia fulani hapo tu basi, ila baada ya kukubali njia husika matokeo ya kukubali hupangi wewe ni hatma itaamua, na ukikataa pia vivyohivyo, matokeo baada ya kukutaa hujipangii wewe, ni sawa na form six leaver anayejaribu kuchagua course ya kusoma chuo, uhuru huwa anao kabla ya kuchagua, ila akiishachagua, matokeo ya uchaguzi hapangi yeye ni hatma itaamua,labda tuseme akachagua kusoma Sheria, hawezi tena kusema kupitia hii course ya Sheria nitakuja kuwa Daktari mzuri sana, hapo hachagui tena ila hupata matokeo kulingana na uchaguzi wa awali, yaani atakuwa tu mwanasheria maadamu ndicho alichochagua, mpaka labda akatishe masomo hayo, au aende mpaka mwisho, akiwa huru tena afanye maamuzi mengi labda tuseme akasome udaktari baada ya kumaliza au kukatisha masomo yake ya sheria, na akichagua udaktari hawezi sema kupitia udaktari huu nitakuja kuwa engineer mkubwa baadae ni kitu kisichowezekana, uhuru tulionao wanadamu ni katika kufanya maamuzi tu yaani kukubali au kukataa jambo, lakini ukishalikubali au kulikataa matokeo yake huamui wewe yaweje, ni hatma itaamua kulingana na ulivyochagua.
 
Tunachochagua kwa akili zetu ni kukubali au kukataa njia fulani hapo tu basi, ila baada ya kukubali njia husika matokeo ya kukubali hupangi wewe ni hatma itaamua, na ukikataa pia vivyohivyo, matokeo baada ya kukutaa hujipangii wewe, ni sawa na form six leaver anayejaribu kuchagua course ya kusoma chuo, uhuru huwa anao kabla ya kuchagua, ila akiishachagua, matokeo ya uchaguzi hapangi yeye ni hatma itaamua,labda tuseme akachagua kusoma Sheria, hawezi tena kusema kupitia hii course ya Sheria nitakuja kuwa Daktari mzuri sana, hapo hachagui tena ila hupata matokeo kulingana na uchaguzi wa awali, yaani atakuwa tu mwanasheria maadamu ndicho alichochagua, mpaka labda akatishe masomo hayo, au aende mpaka mwisho, akiwa huru tena afanye maamuzi mengi labda tuseme akasome udaktari baada ya kumaliza au kukatisha masomo yake ya sheria, na akichagua udaktari hawezi sema kupitia udaktari huu nitakuja kuwa engineer mkubwa baadae ni kitu kisichowezekana, uhuru tulionao wanadamu ni katika kufanya maamuzi tu yaani kukubali au kukataa jambo, lakini ukishalikubali au kulikataa matokeo yake huamui wewe yaweje, ni hatma itaamua kulingana na ulivyochagua.
Hakika kubwa.
 
Back
Top Bottom