Maisha ya kijijini yana raha zake

tutafikatu

JF-Expert Member
Dec 17, 2011
3,241
4,466
Gari ya ulanzi imepita mbele yangu, nikakumbuka mbali sana.

Mimi ni mtoto wa 'bush'. Nimebahatika kuishi miaka mitano kijijini uswekeni. Niliishi Njombe, ndaani kabisa huko, wanaita Palangawanu. Tulikuwa tukitembea kwa mguu toka Ilembula hospitali hadi Palangawanu (nadhani km 15 hadi 20, sikumbuki, nilikuwa mdogo sana). Mzazi wangu mmoja alikuwa mwalimu huko (si wenyeji). Basi tulikuwa kama miungu wadogo, hata ukicheza mpira wanaogopa kukukanyaga, "mtoto wa mwalimu huyo".

Nikiwa mtoto mdogo wa miaka sita hadi tisa, mzazi alikuwa na tabia ya kunituma kuchukua ulanzi na maziwa, kwa wana vijiji walioko mbali. Ni mazingira mazuri, ya kushuka mabonde, kuvuka mito, na kupanda vijilima. Njiani kumejaa mianzi inayogemwa. Kuna 'masasati', kuna 'vitowo', kuna miwa, kuna embe, kuna 'makusu' sijui. Yaani ilikuwa kwangu neema, sijui umaskini wala utajiri. Kwangu yale yalikuwa maisha. Wahindi wanasema "'fullu' life, no tension".

Ilikuwa kawaida kwa watoto kunywa ulanzi unaogemwa njiani na hata kunywa ule uliotumwa kuuchukua. Siku moja nimefika nyumbani hoooooi, nimekunywa ulanzi mtogwa mpaka nimelewa. Bahati mbaya, nusu ya lita tano ya maziwa iliishia tumboni. Nafika nyumbani napepesuka, badala ya kupata kichapo, mzazi akaishia kucheeeeka tu kwa vituko vya mlevi mtoto.

Ingawa sinywi tena pombe, na sidandii magari barabarani, lakini hizo ni baadhi ya siku nilizozifurahia maishani.

Umeishi kijijini? Unakumbuka nini?
 
Tutafika tuu nimecheka sana huku kijijni nilipo sasa ndo msimu wa ulanzi watoto wanalewa balaa watu kuanzia asubuhi ni kuswata ulanzi tu teh
 
Nimewahi kuishi kijijini,nilikuwa naheshimika....walikuwa wananiita mtoto wa mjini.
Raha sana
 
Bora niendelee kuishi huku ushirombo kijini imalamagigo aiseeee.......
 
Binafsi nimeishi maisha ya kijijini na kwa umri ule niliyafurahia sana. Maisha ya kijijini hasa vijiji visivyo na ukame.
Likizo zangu zote kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne nilikuwa namalizia kijijini.Kuna wakati niko sekondari nilikuwa nikitosha shule ya bweni wilaya ya jirani (Karagwe) nakwenda moja kwa moja kijijini bila kupitia home (Bukoba Mjini)

Ni umbali wa lisaa limoja kutoka Bukoba mjini mpaka kijiji cha Mugana.

Mambo yaliyonifanya nipende kijijini.
- Babu na Bibi (si unajua tena mjukuu wa mjini)
- Vyakula mbalimbali vya asili (Kijijini kulikuwa na kila aina ya chakula cha asili)
- Kuchunga ng'ombe na kukamua (Babu yangu alikuwa na mifugo,Kijiji kilikuwa na ushirikiano hivyo kila kaya ilikuwa lazima kutoa watu wa kuchunga mifugo ya kijiji walau kwa siku moja, kwangu ilikuwa fahari kwenda porini kuchunga.
- Msimu wa matunda (Maembe,mananasi,maberry berry ya kila aina, matunda passion ya asili,mafenesi nk.
- Kuchota maji mtoni
- Mkusanyiko wa watoto kila ikifika usiku
- Utengenezaji wa togwa ya asili
- Kuvuna kahawa
- Kuwinda wanyama (Swala,nguruwe pori nk)
- Kuchanja kuni msituni

Yapo mengi sana ila niishie hapa, nikikumbuka huwa nafarijika sana,natamani maisha yale kujirudia maana nili experiance maisha mengine tofauti na wenzangu.

Nashare na picha kidogo japo si za utotoni
970621_659079490786728_861712063_n.jpg
1000115_658591640835513_257299621_n.jpg
969538_658654127495931_33834844_n.jpg
992923_658602680834409_544237764_n.jpg
 
Gari ya ulanzi imepita mbele yangu, nikakumbuka mbali sana.

Mimi ni mtoto wa 'bush'. Nimebahatika kuishi miaka mitano kijijini uswekeni. Niliishi Njombe, ndaani kabisa huko, wanaita Palangawanu. Tulikuwa tukitembea kwa mguu toka Ilembula hospitali hadi Palangawanu (nadhani km 15 hadi 20, sikumbuki, nilikuwa mdogo sana). Mzazi wangu mmoja alikuwa mwalimu huko (si wenyeji). Basi tulikuwa kama miungu wadogo, hata ukicheza mpira wanaogopa kukukanyaga, "mtoto wa mwalimu huyo".

Nikiwa mtoto mdogo wa miaka sita hadi tisa, mzazi alikuwa na tabia ya kunituma kuchukua ulanzi na maziwa, kwa wana vijiji walioko mbali. Ni mazingira mazuri, ya kushuka mabonde, kuvuka mito, na kupanda vijilima. Njiani kumejaa mianzi inayogemwa. Kuna 'masasati', kuna 'vitowo', kuna miwa, kuna embe, kuna 'makusu' sijui. Yaani ilikuwa kwangu neema, sijui umaskini wala utajiri. Kwangu yale yalikuwa maisha. Wahindi wanasema "'fullu' life, no tension".

Ilikuwa kawaida kwa watoto kunywa ulanzi unaogemwa njiani na hata kunywa ule uliotumwa kuuchukua. Siku moja nimefika nyumbani hoooooi, nimekunywa ulanzi mtogwa mpaka nimelewa. Bahati mbaya, nusu ya lita tano ya maziwa iliishia tumboni. Nafika nyumbani napepesuka, badala ya kupata kichapo, mzazi akaishia kucheeeeka tu kwa vituko vya mlevi mtoto.

Ingawa sinywi tena pombe, na sidandii magari barabarani, lakini hizo ni baadhi ya siku nilizozifurahia maishani.

Umeishi kijijini? Unakumbuka nini?
umenikumbusha kwetu Kanamalenga.
 
Bora niendelee kuishi huku ushirombo kijini imalamagigo aiseeee.......
DUUUH!! Ushirombo Umenikumbusha Runzewe Moja Mkuu!! Juzi Tu 12 Jan 16 Nilipita Ushirombo, Kuna Mtu Mmoja Mwenyeji Wetu, Tukikaa Saana Bukavu, Bujumbura, Kigali Au Goma!! Tunapita Kusalimu Tu!!
 
Ulanzi asubuhi unakuwa mtamu kama juice ya miwa.

Sasa wewe fata sukari yake uone utakavyopotea baada ya jua kuwaka.
 
Pale kijijini kwetu kigera etuma nilikuwa nikienda kutoka musoma mjini lazima wanijue mtoto wa mzee Majaga kasundo kaja leo kutupa maujanja.Lakini nilienda nikaishi pale nikasoma pale primary school kuna samaki wakufa mtu bhana.Kijijini pana raha zake dem unamfata usiku wala hazingui.Ukionga sana mafuta ya kupaka ya mamis
 
Mi mpaka sasa wananiitaga 'Kamjini' ndo jina langu la utani.
Mimi hadi leo nikienda utasikia mtoto wa mjini kaja kwa bibi yake....
Loooh!
Hadi leo wale marafiki zangu wa bush huniambia "wewe mshenzi ulikuwa mjanja sana"
Maana ulipofikia wakati wa kuvunja ungo walikuwa hawajui Pads ni nini!
Mhhhhh ngoja niishie hapa wasije wakanijua mie!
 
Ngoja nipate ka annual leave kangu nikale ndizi zilizoivia mgombani na maparachichi yaliyoivia mtini na kujidondokea yenyewe Mwakaleli.
 
Back
Top Bottom