Mahitaji ya nyakati kisiasa yanakaribia kuleta maafa mapya

Mahitaji ya nyakati kisiasa yanakaribia kuleta maafa mapya

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,912
Reaction score
831,293
Bado miezi kuingia mwaka wa uchaguzi... Mojawapo ya nyenzo muhimu inayotumiwa kwenye jeki ya kushinda ni kaliba ya ulozi ushirikina, uchawi na mambo ya kienyeji bila kusahau shirki....

Awamu zilizopita kuna vifo vya ajali nyingi zilizopoteza maisha mengi kwa wakati mmoja... Bila kusahau mauaji ya wenye ulemavu wa ngozi... Kwakuwa mambo ni mengi na muda hautoshi tumekuwa na hulka ya kusahau haraka na kuacha maisha yasonge...!

Matukio ya matumizi ya nguvu za giza yalifika mahali yakaleta athari kubwa na mbaya kwenye jamii yetu.... Tukasimama kama taifa tukapiga kampeni kubwa na kuelimisha (nilikuwa mmojawapo) mpaka kidogo mambo yakatulia

Sitaki kuzungumzia kafara la kukimbiza moto lakini hivi karibuni nilipata mshtuko mkubwa nilipoona kundi kubwa la watu (wanaojiita waganga wa kienyeji.... Ikisemekana wanafikia mia moja) wakichimba bit kuwa wanakufa na wote wanataojaribu kwenda kinyume na taratibu fulani za mambo ya kisiasa
Nikabaki kinywa wazi na maswali haya

. Ni waganga wa kienyeji au ni wachawi? (Waganga hawaharibu wanatengeneza) iweje hawa watake kuharibu?
. Ni nani kawakusanya? Kawafadhili? Kawatuma?
. Tuna vyama vyetu na taratibu zetu kwenye hivi vyama.. Iwe ni vya wachawi au waganga.. Je hawa walitumia chama gani? Kupitia viongozi gani?
. Kwa mara ya kwanza kaliba ya tiba za kienyeji inakuwa na upande kwenye mambo ya kisiasa... Mmh hii ni very very brand new version....!!!

Uono kimo cha mbilikimo hauwezi kuona madhara yajayo mbeleni... Lakini kama mamlaka hazijakemea lile tangazo la wale waliojiita waganga wa kienyeji.... Kesho na keshokutwa wakianza kuua na kuumiza wengine kwa jina la kulinda mamlaka fulani tutamlaumu nani? Ama tutakuwa na pumzi ya kuwachukulia hatua?

Wengi wameshaanza kuzifufudua zana zao walizokuwa wamezificha mbali.... Maana sasa wana KIBALI....!!! LAKINI
SASA hii kaliba ikidhalilishwa na kuonekana ya kipuuzi tusilalame tena.... IMEINGILIWA.... pengine Kinyume

IMG_20190731_202751.jpeg
 
Nakubaliana na maoni yako. Tuchukue tahadhari kuhusu suala la waganga kuingilia mambo na kutoa vitisho dhidi ya wale wasiokubaliana nao. Tuvumiliane kwani kila mmoja wetu anayo maoni yake ambayo anaona yanafaa. Kama una maoni tofauti basi yatoe kwa njia inayofaa na uwe tayari kutetea hoja zako.
 
Mshana Jr wanishangaza jama
Mganga na mchawi wafanana tu
Tofauti upana makali ya wembe
Aumbaye ndiye auwaye, wabisha
Zama zabadilika kwa kasi kuu
Maisha yasonga mbele haraka
Maana za mambo zabadilika
Wabomoaji wawa wajengaji
Wajenga sehemu yenye ulaji

Sawa kwani mwajiri wao nani
Wataka nini hasa wajameni
Kulinda rais na taasisi yake
Au kulinda kabila Sukuma?
Kabila kuu nchi ya Bulicheka
Kabila la kanda ya ziwa jama
Lakini vitisho na nguvu zanini


Aaa! Nimechoka mwanamiye
Yanini kuumiza kichwa kwani
Nini napata kuililia nchi hii?
Kwenda mirembe kwa pingu?
Kukaa majalalani kuchakura?
Kutembeza uchi barabarani?
Aaah! Kukaa kimya kwafaa?
Ni dalili ya woga au ushujaa?
Mshana Jr napata wazimu

Acha nilale tu mwanakwetu.

Alamsiki

Bazazi
 
Mshana Jr wanishangaza jama
Mganga na mchawi wafanana tu
Tofauti upana makali ya wembe
Aumbaye ndiye auwaye, wabisha
Zama zabadilika kwa kasi kuu
Maisha yasonga mbele haraka
Maana za mambo zabadilika
Wabomoaji wawa wajengaji
Wajenga sehemu yenye ulaji

Sawa kwani mwajiri wao nani
Wataka nini hasa wajameni
Kulinda rais na taasisi yake
Au kulinda kabila Sukuma?
Kabila kuu nchi ya Bulicheka
Kabila la kanda ya ziwa jama
Lakini vitisho na nguvu zanini


Aaa! Nimechoka mwanamiye
Yanini kuumiza kichwa kwani
Nini napata kuililia nchi hii?
Kwenda mirembe kwa pingu?
Kukaa majalalani kuchakura?
Kutembeza uchi barabarani?
Aaah! Kukaa kimya kwafaa?
Ni dalili ya woga au ushujaa?
Mshana Jr napata wazimu

Acha nilale tu mwanakwetu.

Alamsiki

Bazazi
That's Bazazi
 
Bado miezi kuingia mwaka wa uchaguzi... Mojawapo ya nyenzo muhimu inayotumiwa kwenye jeki ya kushinda ni kaliba ya ulozi ushirikina, uchawi na mambo ya kienyeji bila kusahau shirki....

Awamu zilizopita kuna vifo vya ajali nyingi zilizopoteza maisha mengi kwa wakati mmoja... Bila kusahau mauaji ya wenye ulemavu wa ngozi... Kwakuwa mambo ni mengi na muda hautoshi tumekuwa na hulka ya kusahau haraka na kuacha maisha yasonge...!

Matukio ya matumizi ya nguvu za giza yalifika mahali yakaleta athari kubwa na mbaya kwenye jamii yetu.... Tukasimama kama taifa tukapiga kampeni kubwa na kuelimisha (nilikuwa mmojawapo) mpaka kidogo mambo yakatulia

Sitaki kuzungumzia kafara la kukimbiza moto lakini hivi karibuni nilipata mshtuko mkubwa nilipoona kundi kubwa la watu (wanaojiita waganga wa kienyeji.... Ikisemekana wanafikia mia moja) wakichimba bit kuwa wanakufa na wote wanataojaribu kwenda kinyume na taratibu fulani za mambo ya kisiasa
Nikabaki kinywa wazi na maswali haya

. Ni waganga wa kienyeji au ni wachawi? (Waganga hawaharibu wanatengeneza) iweje hawa watake kuharibu?
. Ni nani kawakusanya? Kawafadhili? Kawatuma?
. Tuna vyama vyetu na taratibu zetu kwenye hivi vyama.. Iwe ni vya wachawi au waganga.. Je hawa walitumia chama gani? Kupitia viongozi gani?
. Kwa mara ya kwanza kaliba ya tiba za kienyeji inakuwa na upande kwenye mambo ya kisiasa... Mmh hii ni very very brand new version....!!!

Uono kimo cha mbilikimo hauwezi kuona madhara yajayo mbeleni... Lakini kama mamlaka hazijakemea lile tangazo la wale waliojiita waganga wa kienyeji.... Kesho na keshokutwa wakianza kuua na kuumiza wengine kwa jina la kulinda mamlaka fulani tutamlaumu nani? Ama tutakuwa na pumzi ya kuwachukulia hatua?

Wengi wameshaanza kuzifufudua zana zao walizokuwa wamezificha mbali.... Maana sasa wana KIBALI....!!! LAKINI
SASA hii kaliba ikidhalilishwa na kuonekana ya kipuuzi tusilalame tena.... IMEINGILIWA.... pengine Kinyume

View attachment 1168668
waroge waganga wenzio.
 
Baada ya siku mbili tulisikia kamati ya UMOJA WA WAGANGA NA WACHAWI (Iringa) iliitisha kikao cha dharura, kulijadili kwakina lile tangazo kutoka Gamboshi. Muafaka wa kamati waliofikia ni kulipinga tamko la UMOJA WA WAGANGA NA WACHAWI (Gambosh), na kutoa wito yakua tamko lile ni BATILI na la KUPUUZIA tu, kisha wakasisitiza zaidi yakua kila mtu mwenye hadhi ya kuchukua form za kugombea urais ana haki ya kuchukua.

Sasa tunachosubiri ni KAMATI YA MARIDHIANO baina yao, au VIKWAZO VYA KIMATAIFA (Vya ushirikiano, Vya matumizi ya anga, Mauziano ya silaha n.k) kwa yule atakaekaidi.

*Mara paaaaaap tutasikia Iringa wameitungua DRONE ya Gamboshi iliopita katika anga yao na kukiuka masharti. Au utasikia Gamboshi wanajaribu MAKOMBORA yao ya masafa marefu kule kanda ya ziwa.

#Vita Baridi Ya Waganga Na Wachawi (North Korea VS South Korea)
 
Baada ya siku mbili tulisikia tamko kutoka kwa UMOJA WA WAGANGA NA WACHAWI (Iringa), wakipinga tamko la UMOJA WA WAGANGA NA WACHAWI (Gambosh), na kutoa wito yakua tamko lile ni BATILI na la KUPUUZIA tu, na wakasisitiza zaidi yakua kila mtu mwenye hadhi ya kuchukua form za kugombea urais ana haki ya kuchukua.

Sasa tunachosubiri ni VIKWAZO VYA KIMATAIFA kwa yule atakaekaidi kati yao.

#Vita Baridi Ya Waganga Na Wachawi (North Korea VS South Korea)
Sasa tunachosubiri ni VIKWAZO VYA KIMATAIFA kwa yule atakaekaidi kati yao.

#Vita Baridi Ya Waganga Na Wachawi (North Korea VS South Korea)
 
Mshana kuna naneno ningeyatumia hapa, ila kwa heshima yako naomba nisiyaseme. Lakini ni hatari sana kuwa na jamii ya namna hii. Ama kweli kuna uchawi mweusi na uchawi mweupe.
Kwa namna hii Urusi, China & Marekani waendelee tu na safari zao za kwenda anga la juu huku sisi tukijaribu kugawana keki ya taifa na walozi.
 
Mshana kuna naneno ningeyatumia hapa, ila kwa heshima yako naomba nisiyaseme. Lakini ni hatari sana kuwa na jamii ya namna hii. Ama kweli kuna uchawi mweusi na uchawi mweupe.
Kwa namna hii Urusi, China & Marekani waendelee tu na safari zao za kwenda anga la juu huku sisi tukijaribu kugawana keki ya taifa na walozi.
 
Back
Top Bottom