Mahari ni Jukumu la nani?

Mahari ni Jukumu la nani?

Desidii

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2007
Posts
1,201
Reaction score
86
Kwanza habari zenu nimewamisi sana kitambo sijatia timu hapa.

Hii imenitokea mimi mwenyewe na kunikosesha raha kabisa.

Wiki kama mbili hivi tulipata barua ya uchumba ya mtoto wa dada yangu tunaishi nae kwa wazazi wangu baada ya dada kufariki. Wazazi waakaijibu vizuri haikuchukua muda tukaambiwa mahari inaletwa wiki inayofata, tukawakubalia nilihusishwa nikiwa kama mwanafamilia na mtoto wa mwisho kuzaliwa na ambaye naishi na kuwatunza wazazi. Nilikuwa na mawasiliano na mtoto wangu kwa karibu na huwa ni rafiki ndugu haya tukaandaa kila kitu nikashangaa usiku wa kuamkia hiyo Jumapili ambayo ndo wanaleta mahari ananimbia Mama Mdogo niazime tsh.... Nikamuuliza za nini? Jibu nililopata nusu nizimie eti mkwe kapungukiwa mahari mie kijasho kikanitoka na kumuulizaa kulikuwa na haja gani ya kukimbilia kuja wakati hamjajipanga? Hakuna jibu la kueleweka hata chembe nikanyamaza maandalizi yanaendelea akaona haitoshi kampa namba ya simu yangu huyo mkwe aniombe nikashangaa sana tena sana nikaona huruma nikamwazima huku nikiwa sielewi ni nini maana ya hii. Mimi kama kawaida ya kutaka kujua kwanini iwe hivi nikachukua simu yake nakuiangalia na kukuta mpango umepangwa kunidanganya mimi. Wakati nimeshatoa tayari iliniudhi sana na kumuuliza mwanangu why unanifanya mimi mjinga? Majibu anayonipa namuonea sababu mama yake amekufa najiuliza jukumu la kutoa mahari ni la nani jamani? Ama mimi ndo mshamba sana au bado nina mambo ya kale?? Nisaidieni plz
 
....wanakuhujumu hao ndugu...na ukikaka vibaya wanakupa sumu kabisa ufe wabaki wanafaidi wenyewe..
 
....wanakuhujumu hao ndugu...na ukikaka vibaya wanakupa sumu kabisa ufe wabaki wanafaidi wenyewe..

Inabidi nikae chonjo kwa kweli naona hali si nzuri asante
 
jukumu la muoaji mkuu;maadam umeingizwa mjini kuwa mpole.
 
jukumu la mwanaume, lazma walipie huduma watakayoenda kuipata.
 
Dah! Namuonea huruma huyo mwanao inawezekana bado hajajitambua!! Atapata shida kwa hiyo ndoa!! Mpe darasa!!
 
Mimi nadhani ni mambo ya 'digitali'. Kuna mshkaji wangu alipendana na binti, bahati nzuri ama mbaya,upande wa binti mambo safi,kuanzia familia hadi binti mwenyewe,ilhali mshkaji wangu mimi hali yake ni 'tia maji tia maji',familia kama dizaini haikufarahishwa na muunganiko wa wawili hawa ika-set mahari 'karibu na ceiling'. Kwakua wanapendana, 'njiwa' hawa wawili wakatengeneza mpango baina yao,bi harusi mtarajiwa akatoa mzigo kama 95% akamkabidhi mshkaji akatop up 5% akaukabidhi mzigo kwa wazazi wa binti. Hali kadhalika kama ilivyotarajiwa send-off ilikua funika bovu,harusi 'mchele mchele', bi harusi akawashirikisha 'ndugu waaminifu' wakatema kitu kama 6M harusi 'mchele-mchele' ukapungua picha likawa clear wakaoana! So, kusaidiana kupo kama nia ni njema na mapenzi ni ya dhati. By the way, si 'wanawake nao wanaweza ama'?
 
Back
Top Bottom