Ado Shaibu
Member
- Jul 3, 2010
- 99
- 111
:A S 11:MAHABA MURUA
Niliripoti chuoni, sina kitu mfukoni
Mawazo tele kichwani, kijana takula nini?
Sina mwenyeji mjini, atanisitiri nani?
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Zikapita wiki mbili, mpenzi ukaingia,
Shida zangu za awali, taratibu kapungua,
Wewe ukanifadhili, mwandani ukanilea
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Umenipa pa kukaa, ada ukanilipia
Nikapata vya kuvaa, vyote umegharamia,
Hivi nani asojua, chakula wanipatia?
Penzi lako ni murua, usiniache mpenzi
Kwa vitabu hautoshi, desa* umenipatia
Mara chache kwa ubishi, hovyo ninakutumia,
Nawe vile si aushi*, huishia niumbua
Penzi lako ni murua, usiniache mpenzi
Amini nakuambia, umenitia kiwewe,
Tangu mwanzo wa dunia, jatokea kama wewe,
Penzilo menisisimua, sijaona mfanowe
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Nakupenda sana bumu*:A S wink:, mpenzi wa moyo wangu
Haitoshi kwa kalamu, kuchora hisia zangu
Ukawiapo kutimu, chuo chote ni kichungu
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Hata walio nyumbani, wengi wanakukumbuka
Wamehitimu chuoni, bado wanahangaika
Watakufuta kichwani, ndarama* wakizishika
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
©Ado Shaibu ( Komredi wa Malenga). 3/06/2014
Note:
*Desa/madesa: jina linalotumika kwenye vyuo vingi nchini kumaanisha vitini (hand-outs)
*Aushi: kitu cha kudumu/chenye kuishi kwa muda mrefu
*Bumu (Boom): Jina linalotumika kumaanisha pesa za malazi na chakula zitolewazo na Bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
*Ndarama: fedha
Niliripoti chuoni, sina kitu mfukoni
Mawazo tele kichwani, kijana takula nini?
Sina mwenyeji mjini, atanisitiri nani?
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Zikapita wiki mbili, mpenzi ukaingia,
Shida zangu za awali, taratibu kapungua,
Wewe ukanifadhili, mwandani ukanilea
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Umenipa pa kukaa, ada ukanilipia
Nikapata vya kuvaa, vyote umegharamia,
Hivi nani asojua, chakula wanipatia?
Penzi lako ni murua, usiniache mpenzi
Kwa vitabu hautoshi, desa* umenipatia
Mara chache kwa ubishi, hovyo ninakutumia,
Nawe vile si aushi*, huishia niumbua
Penzi lako ni murua, usiniache mpenzi
Amini nakuambia, umenitia kiwewe,
Tangu mwanzo wa dunia, jatokea kama wewe,
Penzilo menisisimua, sijaona mfanowe
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Nakupenda sana bumu*:A S wink:, mpenzi wa moyo wangu
Haitoshi kwa kalamu, kuchora hisia zangu
Ukawiapo kutimu, chuo chote ni kichungu
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
Hata walio nyumbani, wengi wanakukumbuka
Wamehitimu chuoni, bado wanahangaika
Watakufuta kichwani, ndarama* wakizishika
Mahaba yako murua, usiniache mpenzi
©Ado Shaibu ( Komredi wa Malenga). 3/06/2014
Note:
*Desa/madesa: jina linalotumika kwenye vyuo vingi nchini kumaanisha vitini (hand-outs)
*Aushi: kitu cha kudumu/chenye kuishi kwa muda mrefu
*Bumu (Boom): Jina linalotumika kumaanisha pesa za malazi na chakula zitolewazo na Bodi ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
*Ndarama: fedha