Magufuli na Raila Odinga wafanya sala ya pamoja CHATO

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Sep 21, 2011
16,510
28,416
1-8-1024x657.jpg


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo amafanya ibada ya pamoja na mgeni wake Raila Odinga katia Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato.

Katika salamu zake kwa waumini wa Parokia ya Chato, Mheshimiwa Odinga aliyeambatana na mkewe Mama Ida Odinga, amewashukuru watanzania kwa uhusiano mzuri walionao na wakenya, huku akitoa mfano wa jinsi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyojitoa kupigania uhuru wa mataifa mengi ya Afrika ikiwemo Kenya.

Mheshimiwa Odinga ametoa mfano wake mwenyewe kuwa Mwalimu Nyerere alimpatia pasi ya kusafiria ya Tanzania, aliyoitumia kwa miaka mitatu kwa ajili ya kwenda kusoma nje ya nchi, baada ya utawala wa Kikoloni wa Kenya kukataa kumpa pasi hiyo.

Kuhusu urafiki wake na Rais Magufuli, Mheshimiwa Odinga amesema urafiki huo ulianza tangu Rais Magufuli alipoteuliwa kuwa Waziri wa Ujenzi na yeye kuwa Waziri mwenye dhamana ya ujenzi wa Kenya, ambapo mara kadhaa walibadilishana uzoefu na kushirikiana katika mipango ya miradi ya ujenzi wa barabara, na kwa umuhimu huo ametoa wito kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuendeleza ushirikiano na mshikamano ulioasisiwa na waasisi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania, Jalamogi Odinga wa Kenya na Milton Obote wa Uganda.

2-4.jpg


Akizungumza katika ibada hiyo Rais Magufuli aliyeambatana na mkewe mama Jannet Magufuli pamoja na mambo mengine amewahusia watanzania wote kuendelea kuliombea Taifa ili liendelee kuwa na amani.

“Niwaombe watanzania wote tuendelee kushirikiana na kushikamana, kwa umoja wetu na siku zote tumtangilize Mungu mbele.
“Wakati tunaadhimisha wiki moja baada ya kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo, Yesu Kristo alikufa kwa sababu ya dhambi zetu, sisi wote tujitahidi kufuata matendo ya Yesu Kristo ya kusameheana, kupendana, kushirikiana na tusibaguane”

Source: Rais Magufuli asali pamoja na Raila Odinga Mjini Chato | Magazeti ya leo| Tanzania News |Tanzania Today
 
Inapendeza sana, tumuombee na yeye odinga ashinde urais kwenye uchaguzi ujao ili ushirikiano huu ulete manufaa zaidi kwa nchi zetu
Shida ni Wakikuyu na hao Wakalenjini Odinga ni mtu anayefanyiwa mizengwe na vyombo vya usalama na taasisi zake huko Kenya kwani vyombo hivyo vyote vipo chini ya mabwenyenye wa Mt Kenya Mafia,Raila ni raisi wa Kenya asiye na serikali.
 
Shida ni Wakikuyu na hao Wakalenjini Odinga ni mtu anayefanyiwa mizengwe na vyombo vya usalama na taasisi zake huko Kenya kwani vyombo hivyo vyote vipo chini ya mabwenyenye wa Mt Kenya Mafia,Raila ni raisi wa Kenya asiye na serikali.
Jamaa kapokonywa sana ushindi wake kama muheshimiwa naniliu yule wa Zenzi alivyopokonywa juzi kati
 
"....kuendeleza ushirikiano ulioasisiwa na waasisi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania, Jalamogi Odinga wa Kenya na Milton Obote wa Uganda..."

Ina maana East Africa Community ya wakati huo Mzee Jomo Kenyatta hakushiriki kuiasisi?
 
"....kuendeleza ushirikiano ulioasisiwa na waasisi Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania, Jalamogi Odinga wa Kenya na Milton Obote wa Uganda..."

Ina maana East Africa Community ya wakati huo Mzee Jomo Kenyatta hakushiriki kuiasisi?
Ha ha ha ha
That name is skipped for special purpose, wanasiasa bana, every where is politics even in churches
 
Safi sana mkulu.tunaomba zidisha ushirikiano ili kulisongesha gurudumu la maendeleo kwa Africa mashariki Mungu akupe nguvu zaidi na zaidi.
 
Back
Top Bottom