Magufuli: Manufaa ya ziara za nje za Rais Kikwete ni makubwa!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,405
23,581
Kwa CCM nachoka...! Flashback...30/9/2015

magufuli-akiongea-na-wakazi-wa-kijiji-cha-Pawaga.jpg

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM, Dk. John Magufuli, amewashangaa watu wanaokejeli safari za nje za Rais Jakaya Kikwete, akisema manufaa ya ziara hizo ni makubwa kuliko wanavyofikiri.

Amesema kupitia safari hizo, Rais Kikwete amefanikiwa kuwashawishi wafadhili kutoa misaada ya miradi mbalimbali nchini.

Aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni katika kata ya Mvumi Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma jana.

Dk. Magufuli alitoa mfano wa Sh. bilioni 992 zilizotolewa na Serikali ya Marekani hivi karibuni kupitia mfuko wa MCC kwa ajili ya miradi ya umeme kama sehemu ya matunda ya safari za Rais Kikwete nchi za nje.

Fast Forward...27/3/2016

az7.jpg

Rais Magufuli ametoa wito katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Rais Magufuli amesema tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi.

Katika kusisitiza amesema tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio kuomba misaada kutoka nchi nyingine.


Hii imekuja baada ya Marekani kusitisha msaada wake kupitia mfuko wa MCC kwa ajili ya miradi ya umeme aliodai awali kama sehemu ya matunda ya safari za Rais Kikwete nchi za nje
 
Anayekuroga anakujua siku zote kanzu ndo mpya ila shekhe n CCM yuleyule,mm huyu mtu Magufuli hata afanye lipi naona anataka sifa tu hana dhati moyoni na hata km anayo haiwezi kuwa na tija coz yy kawekwa na system na hawezi toka nje ya KEY.Ikumbukwe alitukana sana na kulaani safar hzo za nje na huku alisahau kuwa alishawahi kuziunga mkono.Au alichozungumza ktk maadhmsho ya miaka kadhaa ya CCM singida aliwazungumziaje wapinzani na wkt wa kampen alitoa ahadi gani kwa wapnzan na watz kwa jumla?wazi utajua kuwa yupo kwa system hawez toka nje watz n wepesi kudanganywa na ni wagumu kubadilika coz hatunaga kumbukumbu hata kwa mambo ya msingi
 
Kuna sababu huu UZI HAUNA WACHANGIAJI.
Nilitaka sana kuwasikia wale walio tayari kula nyasi wakidai hatuhitaji misaada wanasemaje kwa huu uliokuwa ni msimamo wa Magufuli wakati akiomba kura. Wakati huo Magufuli akiwa Waziri katika serikali ya Vasco Dagama alikuwa akitushangaa tuliokuwa tukiponda kuzurura kwa Kikwete ugenini akitembeza bakuli.

Kwa miaka kumi akiwa madarakani, miaka minne Kikwete aliimalizia angani huku mawaziri wake akiwemo Magufuli wakisubiri neema atakayowaletea bosi mtalii. Je wakati huo Magufuli hakujua Kwamba hapa nyumbani kwenye nchi iliyojawa neema tunahitaji tu kufanya kazi na si kuombaomba hadi tunafungiwa milango?
 
Kwa CCM nachoka...! Flashback...30/9/2015

magufuli-akiongea-na-wakazi-wa-kijiji-cha-Pawaga.jpg

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM, Dk. John Magufuli, amewashangaa watu wanaokejeli safari za nje za Rais Jakaya Kikwete, akisema manufaa ya ziara hizo ni makubwa kuliko wanavyofikiri.

Amesema kupitia safari hizo, Rais Kikwete amefanikiwa kuwashawishi wafadhili kutoa misaada ya miradi mbalimbali nchini.

Aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni katika kata ya Mvumi Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma jana.

Dk. Magufuli alitoa mfano wa Sh. bilioni 992 zilizotolewa na Serikali ya Marekani hivi karibuni kupitia mfuko wa MCC kwa ajili ya miradi ya umeme kama sehemu ya matunda ya safari za Rais Kikwete nchi za nje.

Fast Forward...27/3/2016

az7.jpg

Rais Magufuli ametoa wito katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Rais Magufuli amesema tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi.

Katika kusisitiza amesema tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio kuomba misaada kutoka nchi nyingine.


Hii imekuja baada ya Marekani kusitisha msaada wake kupitia mfuko wa MCC kwa ajili ya miradi ya umeme aliodai awali kama sehemu ya matunda ya safari za Rais Kikwete nchi za nje
 
Kwa hiyo unataka kutuambia nini?

Ni wapi na lini Rais Magufuli amesema hataki misaada?

Rais Magufuli amesema misaada ina masharti ambayo mengine haiwezekani kuyatimiza na kwa maana hiyo ni vizuri kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuepuka misaada yenye masharti.
 
Kweli ni unafiki. Ni zaidi ya Lowassa kuwa fisadi CCM na kuwa mtakatifu ndani ya UKAWA.

Kwa kauli yako hii unazidi tu kudhihirisha jinsi U-CCM na ufisadi ni pete na kidole. Umekiri mwenyewe kwamba huo unaodai ni ufisadi wa Lowassa unahusiana moja kwa moja na U-CCM wake wakati huo. Nachukua nafasi hii kukushukuru kwa kuliweka hili wazi na kwa hali itakayoeleweka kirahisi hata kwa wana CCM wenzako.
 
Hehee walishaanza kusema ooh nzi wa kijani hawatui ktk huu uzi. Sasa wametua naona nyumbu wamesepa. Mnafikiri wasio na kumbukumbu ni CCM tu eeh? Msipofushwe macho na kujiziba masikio kisa nyie ni wapinzani
 
Kwa hiyo unataka kutuambia nini?

Ni wapi na lini Rais Magufuli amesema hataki misaada?

Rais Magufuli amesema misaada ina masharti ambayo mengine haiwezekani kuyatimiza na kwa maana hiyo ni vizuri kufanya kazi kwa bidii na maarifa ili kuepuka misaada yenye masharti.
 
Back
Top Bottom