Lowasa ana busara na akili sana.
Huyu jamaa ni mstaarabu wa kweli na anapenda watu kweli.
Kwanza anatambua kuwa endapo atakaa sehemu moja na Magufuli ambaye ndiye rais kwa sasa basi anaweza akawapotezea watu nafasi zao za lazi.
Hii ni kutokana na ukweli kwamba watanzania wengi hata ndani ya serikali wana mahaba na mapenzi makubwa kwa Lowasa hivyo watajionyisha dhahiri kwa kumkimbilia Lowasa na kila mtu kutaka kusalimiana naye jambo litakalo mshushia Mkuu wa nchi heshma. Hata wasaidizi wa Magufuli watapata wakati mgumu wa kushindwa kuacha kumkimbila Lowasa jambo litakalo wafanya wengine kupatoza nafasi zao warakapo rejea ofisini.
Ikumukwe kuwa kundi kubwa lililomuunga mkono Magufuli ni lile lile kundi la Lowasa ndani ya CCM.
Hivyo ni kweli kabisa kuwa Lowasa bado ana kundi kubwa sana ndani ya taifa hili.
Tunaweza tu kujikumbusha yaliyotokea kule Dodoma kwa Rais Kikwete kuzomewa baada ya kukata jina la Lowasa huku mamia wa wajumbe wa CCM wakimshingilia Lowasa na kuimba kuwa wana imani naye. Hali ile iliwapandisha hasira makada wachache waandamizi na wenye nguvu kubwa ndani ya CCM kama Mzee Butiku na kusema hadharani kuwa Kikwete ni mpole sana ingekua ni nchi nyingine Lowasa angepotezwa. Sijajua maana halisi ya kupotezwa ! Ni kupotezwa njia au nini?
Hiyo ndiyo CCM inayoimba sisi wote ni ndugu lakini ndani kuna makada yanayotamani kumwona Rais akiwaangamiza wapinzani wake kwa kuwapoteza duniani.
Lowasa ana hekima za ajabu.
Naamini pia kutokana na ucha Mungu wa Mh.Magufuli naye pia ana shauku ya kukutana na mzee Lowasa na kusalimiana kwani yeye binafsi hana chuki na Lowasa na ameshaingia Ikulu na kuona kila mkataba na kugundua kuwa mengi yaliyovumishwa juu ya Lowasa ni uzushi.
Lakini poa hata kwa Magufuli endapo atakutana na Lowasa na kusalimiana kwa sura za amani na upendo basi itaweza kuwakatisha tamaa wale makada wote wa CCM wanaotamani kumwona Magufuli akiwaonea wapinzani na kupambana nao hata kama hawana hatia yoyote .
Pia kwa sasa Lowasa haamini tena marafiki wa kisiasa. Alikwisha kuumwa na nyoka na sasa akiona jani anakimbia.
Bado anakumbuka alichofanyiwa na rafiki yake enzi za BOYS II MEN.