1) Tangu Dunia imeumbwa na Mola wetu mpaka 2005 Watanzania waliokuwa wanapata umeme walikuwa 10%. Kuanzia Dec 2005 mpaka Nov 2015 wamefikia 34%.
2) Shule za Kata alizojenga Jakaya nyingi zaid kuliko kuanzia Alizojenga Mkapa mpaka wakati wa Adam na EVA/Hawa.
3) Uhuru wa Kujieleza ulikuwa Mkubwa sana mpaka Wavuta bhangi kama Lema na Nasari kutangaza Jamhuri ya Kaskazini na Kumpiga Marufuku Rais wa Nchi asikanyake Arusha na hawakuguswa wala kusumbuliwa.
4) Barabara za Lami alizojenga haijawahi kutokea wala kusimuliwa kama alivosema Waziri wake wa Ujenzi.
5) Huduma za Moyo, Meno figo zimeboreka sana ukibisha waulize Mufti,Kardinali na Sumaye waliokabidhi Mustakabali wake kitengo cha Jakaya Kikwete Muhimbili badala ya kwenda Nje.
6) Urasimu kwny Ajira kaondoa kwa kuanzisha Secrtariet ya Ajira hivi leo sio ajabu kumkuta Mwazani,Karumanzira au Masanja kuwa Wizara ya fedha badala ya yale majina ya Shirima na Rweyemamu yaliyozoeleka tangu uhuru maana ukihitaji Mtumishi unapeleka maombi kule na wao ndo wanaajiri badala ya yale ya zamani Baba anatengeneza nafasi ya kazi halafu anamfanyia Mwanae interview n.k
7) Mahusiano ya Kimataifa yaliboreka sana sana sana hasa kuweza ku balance Urafiki wa Magharibi na Mashariki.
8) Kuzuia kwa ujasiri Mkubwa genge la wapiga dili kukabidhiwa Ikulu.
Anayo mapungufu yake mfano kuwapa Madaraka kwa kuangalia urafiki badala ya uwezo na uadilifu mf. Kuteua Waziri Mkuu mtu aliewahi kukataliwa na Mwl Nyerere kwa Wizi.
Kama Jakaya alipata Zali basi hata wewe una zali kutawaliwa nae!