Magufuli aleta mkanganyiko kwa wananchi!!

Magufuli aleta mkanganyiko kwa wananchi!!

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
2,222
Reaction score
3,360
Ukimsikiliza vizuri Rais Magufuli jinsi anavyohutubia kuna kitu lazima utajiuliza hasa unapomlinganisha na mtangulizi wake Kikwete aliezoea kutuaminisha kwamba nchi iko mahali pazuri sana wala hakua anaorodhesha mapungufu makubwa ktk serikali yake kama afanyavyo Magufuli.

Kuna wakati akiongea Kikwete nilikuwa nazima tv/redio coz nilikua naona ni kama Tanzania anayoizungumzia yeye labda sio hii niishiyo mimi kutokana na tofauti kubwa ya kile alichokua akizungumza na hali halisi huku maishani.

Jambo hili limeibua maswali sana yupi ana tatizo kati yao je Magufuli anaongea kutaka sifa au Kikwete alikua jipu??
 
Mkwere alikua hastahili kuongoza tanzania hata kwa siku moja ni basi tu zali lilimwangukia
 
Anakurupuka mno!Ana visasi!Hajui itifaki.Anapenda sifa za kipuuzi.Kwa mfano kitendo cha rais Magufuli kulisifia gazeti La Jamhuri na kumtangazia Makonda promotion jukwaani NI ULEVI WA MADARAKA
 
Mkwere alikua hastahili kuongoza tanzania hata kwa siku moja ni basi tu zali lilimwangukia
Mkuu shule na kilometa za barabara zilizojengwa wakati wa Jk ni kubwa kuliko jumla ya barabara zilizojengwa wakati wa mkoloni, mwinyi na mkapa, what ele do you need from him? Au kisa amewazuia na kapi lenu kugusa ikulu?Jk is the real leader!
 
Mkuu shule na kilometa za barabara zilizojengwa wakati wa Jk ni kubwa kuliko jumla ya barabara zilizojengwa wakati wa mkoloni, mwinyi na mkapa, what ele do you need from him? Au kisa amewazuia na kapi lenu kugusa ikulu?Jk is the real leader!
Hizo zimejengwa kwa mikopo acha ujuha wewe hata wewe ungeweza kukopa ukajenga sio kitu cha kujisifu wakati tunadaiwa huku barabara zenyewe za kichina ni bora hata mkapa angetawala miaka ishirini
 
Anakurupuka mno!Ana visasi!Hajui itifaki.Anapenda sifa za kipuuzi.Kwa mfano kitendo cha rais Magufuli kulisifia gazeti La Jamhuri na kumtangazia Makonda promotion jukwaani NI ULEVI WA MADARAKA
Watanzania mna matatizo...kwani kuwa mkweli kuna shida gani
 
Mkuu shule na kilometa za barabara zilizojengwa wakati wa Jk ni kubwa kuliko jumla ya barabara zilizojengwa wakati wa mkoloni, mwinyi na mkapa, what ele do you need from him? Au kisa amewazuia na kapi lenu kugusa ikulu?Jk is the real leader!
Unafurahia barabara zilizojengwa kwa fedha za mikopo matupu. Jenga barabara kwa fedha za ndani, tungemkubali balaa
 
Mkwere alikua hastahili kuongoza tanzania hata kwa siku moja ni basi tu zali lilimwangukia

1) Tangu Dunia imeumbwa na Mola wetu mpaka 2005 Watanzania waliokuwa wanapata umeme walikuwa 10%. Kuanzia Dec 2005 mpaka Nov 2015 wamefikia 34%.
2) Shule za Kata alizojenga Jakaya nyingi zaid kuliko kuanzia Alizojenga Mkapa mpaka wakati wa Adam na EVA/Hawa.
3) Uhuru wa Kujieleza ulikuwa Mkubwa sana mpaka Wavuta bhangi kama Lema na Nasari kutangaza Jamhuri ya Kaskazini na Kumpiga Marufuku Rais wa Nchi asikanyake Arusha na hawakuguswa wala kusumbuliwa.
4) Barabara za Lami alizojenga haijawahi kutokea wala kusimuliwa kama alivosema Waziri wake wa Ujenzi.
5) Huduma za Moyo, Meno figo zimeboreka sana ukibisha waulize Mufti,Kardinali na Sumaye waliokabidhi Mustakabali wake kitengo cha Jakaya Kikwete Muhimbili badala ya kwenda Nje.
6) Urasimu kwny Ajira kaondoa kwa kuanzisha Secrtariet ya Ajira hivi leo sio ajabu kumkuta Mwazani,Karumanzira au Masanja kuwa Wizara ya fedha badala ya yale majina ya Shirima na Rweyemamu yaliyozoeleka tangu uhuru maana ukihitaji Mtumishi unapeleka maombi kule na wao ndo wanaajiri badala ya yale ya zamani Baba anatengeneza nafasi ya kazi halafu anamfanyia Mwanae interview n.k
7) Mahusiano ya Kimataifa yaliboreka sana sana sana hasa kuweza ku balance Urafiki wa Magharibi na Mashariki.
8) Kuzuia kwa ujasiri Mkubwa genge la wapiga dili kukabidhiwa Ikulu.

Anayo mapungufu yake mfano kuwapa Madaraka kwa kuangalia urafiki badala ya uwezo na uadilifu mf. Kuteua Waziri Mkuu mtu aliewahi kukataliwa na Mwl Nyerere kwa Wizi.
Kama Jakaya alipata Zali basi hata wewe una zali kutawaliwa nae!
 
Anakurupuka mno!Ana visasi!Hajui itifaki.Anapenda sifa za kipuuzi.Kwa mfano kitendo cha rais Magufuli kulisifia gazeti La Jamhuri na kumtangazia Makonda promotion jukwaani NI ULEVI WA MADARAKA


Sidhani kama ni ulevi wa madaraka ila inaitwa encouragement...learn from others.
 
M
Anakurupuka mno!Ana visasi!Hajui itifaki.Anapenda sifa za kipuuzi.Kwa mfano kitendo cha rais Magufuli kulisifia gazeti La Jamhuri na kumtangazia Makonda promotion jukwaani NI ULEVI WA MADARAKA
Mtalewa sana nyie majipu Magufuri mziki mzito bakini huko mkizungusha visigino sasa , tunamwamini atawatumbua hata mkihamia mgongoni ! Bravo Presida Magu
 
1) Tangu Dunia imeumbwa na Mola wetu mpaka 2005 Watanzania waliokuwa wanapata umeme walikuwa 10%. Kuanzia Dec 2005 mpaka Nov 2015 wamefikia 34%.
2) Shule za Kata alizojenga Jakaya nyingi zaid kuliko kuanzia Alizojenga Mkapa mpaka wakati wa Adam na EVA/Hawa.
3) Uhuru wa Kujieleza ulikuwa Mkubwa sana mpaka Wavuta bhangi kama Lema na Nasari kutangaza Jamhuri ya Kaskazini na Kumpiga Marufuku Rais wa Nchi asikanyake Arusha na hawakuguswa wala kusumbuliwa.
4) Barabara za Lami alizojenga haijawahi kutokea wala kusimuliwa kama alivosema Waziri wake wa Ujenzi.
5) Huduma za Moyo, Meno figo zimeboreka sana ukibisha waulize Mufti,Kardinali na Sumaye waliokabidhi Mustakabali wake kitengo cha Jakaya Kikwete Muhimbili badala ya kwenda Nje.
6) Urasimu kwny Ajira kaondoa kwa kuanzisha Secrtariet ya Ajira hivi leo sio ajabu kumkuta Mwazani,Karumanzira au Masanja kuwa Wizara ya fedha badala ya yale majina ya Shirima na Rweyemamu yaliyozoeleka tangu uhuru maana ukihitaji Mtumishi unapeleka maombi kule na wao ndo wanaajiri badala ya yale ya zamani Baba anatengeneza nafasi ya kazi halafu anamfanyia Mwanae interview n.k
7) Mahusiano ya Kimataifa yaliboreka sana sana sana hasa kuweza ku balance Urafiki wa Magharibi na Mashariki.
8) Kuzuia kwa ujasiri Mkubwa genge la wapiga dili kukabidhiwa Ikulu.

Anayo mapungufu yake mfano kuwapa Madaraka kwa kuangalia urafiki badala ya uwezo na uadilifu mf. Kuteua Waziri Mkuu mtu aliewahi kukataliwa na Mwl Nyerere kwa Wizi.
Kama Jakaya alipata Zali basi hata wewe una zali kutawaliwa nae![/QUOT



Tunahitaji kusema hivi kwa Mstaafu Mheshimiwa JK
 
Magufuli sio mwanasiasa, hafanani kabisa na mtu mwenye kutaka kumfurahisha kila mtu. Anaongea kile anachokiona kipo sahihi kwa wakati husika. Hataki kutabasamu kwa kila mtu anayekatiza mbele ya macho yake. Wazalendo wa kweli, wenye kuitanguliza nchi, watu waliozoea kuona haki ikitendekea, wanamuelewa sana kuliko wale waliozoea maisha ya kinafiki.
 
Mkwere alikua hastahili kuongoza tanzania hata kwa siku moja ni basi tu zali lilimwangukia

Mungu amuweke mahali pema peponi,Mwl Nyerere.Namlaumu kwa jambo moja tuu,ambalo hats yeye hakuli notice!
Alikuwa akitoa hutuba nzuri Sana na wasikilizaji kumshangilia bila kumuelewá!
Sasa hivi Naamini watu wengi sasa hivi ndiyo tunamuelewa alikuwa Ana maana gani? Rejea mikutano ya uteuzi ya chama JK alipo gombea Mara ya kwanza
.
 
Mungu amuweke mahali pema peponi,Mwl Nyerere.Namlaumu kwa jambo moja tuu,ambalo hats yeye hakuli notice!
Alikuwa akitoa hutuba nzuri Sana na wasikilizaji kumshangilia bila kumuelewá!
Sasa hivi Naamini watu wengi sasa hivi ndiyo tunamuelewa alikuwa Ana maana gani? Rejea mikutano ya uteuzi ya chama JK alipo gombea Mara ya kwanza
.

Endeleeni kujidanganya kuwa Kikwete hakuwa akikubalika kwa Mwl. Nyerere.
1) Mwl Nyerere ndio alimteua Katibu msaidizi wa CCM Singida April 1975.
2) Mwl Nyerere ndiye alimteua Kikwete 1977 kwenda ku harmonise ASP na TANU Kisiwandui Zanzibar kuileta CCM.
3) 1978 akateuliwa kuwa Mwandishi wa Minutes za vikao vya Vita ya Kagera akiwa tayari Mkufunzi Mwanajeshi na hata 1982 kwny Kikao cha Majumuisho ya Vita ndie alipewa Jukumu la ku destroy taarifa zote za siri za vikao vya kupanga mikakati ya vita.
3) 1989 Aliteuliwa Naibu Waziri wa Maji sambamba na Hayati Ditopile baada ya kikao cha NEC viwanja vya karimjee akiwa Ostybay hotel akijiandaa kurudi Nachingwea.
4) 1995 Mwl Nyerere alimtuma General Ulimwengu amfuate jk akiwa Waziri wa Fedha waje nae Ikulu ya Mzee Mwinyi wakamtaka akachukue form ya Urais. Lengo la Mwl Nyerere halikuwa Jk awe Rais kwa wakati ule bali alitaka apatikane Mtu atakaefifisha Nyota ya Mzee Malecela aliekatwa na kweli kukatwa kwa Malecela huku jina la kijana Jakaya likichomoza watu wakaacha kujadili Kukatwa kwa Malecela wakawa wanashangilia kuibuka kwa kijana Jakaya. Mwl akawa kawazidi akili wote akapata Fursa ya kumteua Benjamin Mkapa bila ya Heka heka sana kwa kuwa hata Jakaya mwenyewe aliona ni ngekewa kupata umaarufu ule wa ghafla.
Waliokuwa hawatakiwi na Mwl hawakupenya kwn Mchujo mf. EDWARD LOWASSA na JOHN SAMWEL MALECELA walikatwa kabisa Jakaya alitumika boshen kuingia 3 bora langu likiwa kumpitisha Mkapa kwa ahadi ya kufikiriwa baadae, kama walivotumika kina Asha rose na Amina Said. Baada ya uchaguzi kwny Baraza la Kwanza la Mkapa Malecela na Lowassa waliokataliwa na Mwl hawakuwemo kwny cabinet, baadae 1998 ndio kwny Mabadiliko madogo akaingia Lowassa. Lakin Jakaya tangu 1989 akipoingia Wizarani hakutoka mpaka akawa Rais.
 
Back
Top Bottom