Magufuli acha vitisho, tumebalehe kiakili

Magufuli acha vitisho, tumebalehe kiakili

DAMAS DAMIAN

Senior Member
Joined
Apr 8, 2011
Posts
115
Reaction score
54
Ni zaidi ya mara tatu mgombea wa CCM anasikika kwenye mikutano akiwataka watu wasifanye mabadiliko kwani yanaweza kutokea mambo kama ya Libya, hii ni dhahiri ya kwamba CCM hawana pakutokea maana wameona kuhubiri ubaguzi kumefeli, kuwatumia viongozi wa upinzani kumefeli na sasa wanawatisha wapiga kura kwa hoja za kitoto, hili nalo linafeli. CCM na Magufuli mnapaswa kujua yafuatayo:-

1. Libya Ghadafi aliingia kwa mtutu wa bunduki na ametolewa kwa mtutu wa bunduki, sisi kwetu tunapiga kura tena kwa amani.

2. Huu sio uchaguzi wa kwanza kufanyika Tanzania na tumekuwa tukipata viongozi kwa amani, mwaka huu kipi cha ajabu?

3. Hatuwezi kufikia walipo libya sababu ya undugu uliopo miongoni mwetu licha ya tofauti za vyama hata ndani ya familia.

4. Ni ujinga kuhubiri kwamba ukipewa ridhaa utafanya mabadiliko ndani ya chama na serikali halafu wakati huo huo unawatisha wananchi wasifanye mabadiliko.

Uhai unapotaka kutoka lazima kutapatapa, mabadiliko mwaka huu ni lazima.

Damas Damian,
Bavicha Korogwe
 
Siyo jambo zuri kiongozi kama yeye kuhubiri ya Libya, wakati suala la Libya liko wazi kuwa pale tatizo siyo wananchi pekee. Lakini ni msukumo kutoka mataifa makubwa katika kuondoa udikteta. Sasa nchi yetu tuna utaratibu wa kufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano. Hapo makufuli anapindisha ukweli.


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
DAMAS DAMIAN

Kwanza ajue Libya hawakufanya uchaguzi.Pili kwa mini hatolei mifano kama Zambia,Malawi,Nigeria ambapo uchaguzi ulifanyika na mabadiliko yakatokea smoothly?Mie nadhani anawatisha Tu watu coz sera zake anajua Ni za uongo miaka nenda Rudi.Watch out Tanzanians you are brain washed.Chose Changes,chose Lowasa
 
Last edited by a moderator:
anajua anaongea na kile kizazi cha 47 kumbe ni digital
 
mtanzania wa leo sio tena wa miaka ya 47 hatudanganyiki tena.Walete tena sinema zao za halaiki ya nchi jirani1994 ili kuwatish a watanzania wasifanye mabadiliko.VIVA LOWASA tukutane 25oct
 
Akawaambie waliomtuma kwamba wa Tz wa leo sio wale wa 2010.
 
Ni zaidi ya mara tatu mgombea wa CCM anasikika kwenye mikutano akiwataka watu wasifanye mabadiliko kwani yanaweza kutokea mambo kama ya Libya, hii ni dhahiri ya kwamba CCM hawana pakutokea maana wameona kuhubiri ubaguzi kumefeli, kuwatumia viongozi wa upinzani kumefeli na sasa wanawatisha wapiga kura kwa hoja za kitoto, hili nalo linafeli. CCM na Magufuli mnapaswa kujua yafuatayo:-
1. Libya Ghadafi aliingia kwa mtutu wa bunduki na ametolewa kwa mtutu wa bunduki, sisi kwetu tunapiga kura tena kwa amani.

2. Huu sio uchaguzi wa kwanza kufanyika Tanzania na tumekuwa tukipata viongozi kwa amani, mwaka huu kipi cha ajabu?

3. Hatuwezi kufikia walipo libya sababu ya undugu uliopo miongoni mwetu licha ya tofauti za vyama hata ndani ya familia.

4. Ni ujinga kuhubiri kwamba ukipewa ridhaa utafanya mabadiliko ndani ya chama na serikali halafu wakati huo huo unawatisha wananchi wasifanye mabadiliko.

Uhai unapotaka kutoka lazima kutapatapa, mabadiliko mwaka huu ni lazima.

Damas Damian,
Bavicha Korogwe
Kama hataki mabadiliko kwa nini anagombea? Si aache JK aendelee kutawala? Au atatawala kwa maelekezo ya JK?
 
Jmn mwenzenu anafanya tuu kampeni jmn. Na kuhusu swala la libya huenda mm na ww tusijue lkn habari gani Km kuna msukumo wa mataifa makubwa????
 
DAMAS DAMIAN

Unadhani nyomi ya UKAWA ni ya kuchezea lazima magufuli achanganyikiwe tu maana ameshajua urais haupo hivyo amekimbilia Libya,CCM mtaisoma namba bila akina diamond,na maonyesho ya nyoka mikutano haijai.
 
Last edited by a moderator:
CCM hata katiba yetu wameikataa..
hawataki mabadiliko kwa sababu kamba walizotufunga kutushikilia zikikatika hawana bahati.
rasilimali za nchi hawatozimiliki tena na kuzifanyia umangimeza..
 
Nilichomuelewa magufuli, ni mkiichagua ukawa ccm wataleta machafuko.
 
magufuli anadhani watanzania wa leo ni wakuwatishia picha ya nyau
 
Back
Top Bottom