Manara kwa kusambaza clip aliyokuwa akimshutumu Babra, alijifunga own goal na kuondoka Simba Sc wanamichezo na mashabiki walimlaumu na wengine walisema ni tabia yake mbovu. Hajji akaanza mikakati ya kushambulia na kusawazisha goli kuanzia na ile press yake japo hata hiyo press bado alionekana atapigwa goli lingine la counter attack kwani alijitolea full kushambulia bila kuangalia nyuma. Naam alishamwagiwa ugali swasa aliamua kumwaga mboga kabisa.
Mo Dewji naye kutokana na kupanic na mashambulizi mfululizo akajifunga own goal kwa kumvaa Chama. Matokeo ni 1-1 ila hadi sasa Haji ana advantage ya away goal (Hii kwenye mikeka inaweza kufanana na Handicap Suluhu). Manara amepata public sympathy aliyokuwa anaisaka. Mo anathibitisha baadhi ya tabia zake ikiwemo "Umimi" , anathibitisha kuwa ni kweli ameamua kuwaweka mfukoni uongozi wa timu na wachezaji, anathibitisha kuwa ana mpango kweli wa kuifanya Simba kuwa ndo sehemu ya Mo Enterprises yake, hata wengineo waliokuwa wakimsapoti wamemshangaa na wanajiuliza bado. Sasa Namuona Hajji akija kutafuta GG&3+ kwa mfumo kwa kushambulia kwa kustukiza huku akikaba sana. Namuona Mo akipanga mashambulizi yake aimalize mechi kipindi cha pili kikianza tu sababu yupo nyumbani na watu anao.
Kosa la Manara:
Kumshambulia Mo na Babra kwa uchungu baada ya kuzushiwa kuihujumu timu, lakini hakujali uwa kuna public damage itatokea kwa klabu. Content ya press yake inawenza kuwa chanzo cha baadhi ya migogoro ndani ya klabu. Kwa sasa kama mwanasimba anapaswa aache kumshambulia Mo kwani kuna madhara makubwa kwenye klabu. Manara anaujua udhaifu wa Mo hasa katika kupanic, anajua namna ya kumprovoke. Aache hilo kwa maslahi ya Simba.
Kosa la Mo:
Baada ya kukerwa na Dili za Manara nje ya Ofisi alipaswa kudeal naye kwa tahadhari ukizingatia bado mkataba wake na Simba una utata mwingi. Alikosea kumu"Underestimate" Manara . Press yake juzi ilikuwa na vijembe vya mbali kwa Manara ambavyo ni provocative. Alipaswa kukaa kimya na kutojibujibu, hakupswa kuonesha Chuki ya wazi kwa Manara. Ni kosa lilofanya kwa Kigwangala pia baada ya Kuhojiwa malipo ya 20B zilizopswa kuwekwa ile atumikie nafasi ya Uenyekiti wa Bodi na nafasi ya CEO wakati hakuweka hizo pesa. Majibu yake yalikuwa ni ya kupanic kuwa Kigwa alimkopa pikipiki akamtosa ndo maana ana hasira naye.
Mo anapaswa kumuangalia Babra kwa jichol la 3. Mo anapaswa kuunganisha makundi yanayoanza kujitokeza ndani ya klabu. Awaite wakae chini wayamalize.
Wote hawa wanabeba Mustakabali wa Klabu, Ishu ya Mo na Chama bado ni sehemu ya Moshi mweupe Klabuni. Ikumbukwe Manara nataka kumaliza mechi kwa counter attack , Mo anataka kutumia faida ya uwanja wa Nyumbani kupata ushindi. Hii ni mbaya sana kwa klabu!