Kitambi toroli
New Member
- Mar 29, 2013
- 2
- 5
kiukweli mimi sina shaka na kilewo juu ya uwezo wake, anajituma sana mimi mwenyewe ni miongoni mwa watu niliyomchangia mabati wa matatu. Hongera kilewo endelea kuchanja.Waziri Maghembe ni janga la Kitaifa na Kimataifa. Anakwenda kuomba msaada wa maji Misri wakati Misri ndiyo ndiyo tunawasaidia maji. Atokeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
well done kilewo, naimani wapare sasa wameamka, and r i p magembetunamkaribisha kata ya kilomeni aje kupata baraka za wazee
Mbunge wa Mwanga Jumanne Magembe ambaye pia ni Waziri wa maji ni miongoni mwa waziri ambao wamekwishawahi kukabidhiwa wizara mbalimbali lakini Jimbo lake ni Miongoni mwa majimbo yaliyopo nyuma kimaendelea Mkoani Kilimnjaro na kero nyingi kwa wananchi.
Sina maana kuwa apendelee jimboni kwake la hasha bali atambue wajibu wake wa kuwatumikia wananchi,Juzi katika pitapita zangu nilikutaka na wananchi wakijadili kijana mmoja Henry Kileo wa CHADEMA ambaye kwa sasa anamuumiza sana kichwa Magembe kuwa huenda akamtoa kwenye kiti hicho cha Ubunge kutokana na harakati zake.
Nilikuwa napita maeneo ya Kata ya Kigonigoni ndipo nilipokuta gunzo hilo,huku wazungumzaji wakiwa hawajui ni nani na nimetokea wapi,nilikuwa nimenyeshewa na mvua na nguo zangu zikawa zimechafuka hivyo walinihisi na mimi nimvuvi mwenzao kwenye ziwa Jipe.
kwenye Kata ya Kigoni goni yalitokea maafa ya mvua mwezi uliopita na wananchi wakaharibiwa nyumba zao,kwa kuezuliwa mabati,ila na nyingine kubomoka,lakini viongozi waliokuja kuwatembelea waadhirika hao hadi leo hawajegeuka tena.
Lakini Kileo alifika kwenye eneo hilo na kuwafariji waadhirika wa majanga hayo kwa kuwasaidia mabati ya nyumba mbili,ambapo kilichonifurahisha zaidi mmoja wa waliobomokewa na nyumba ni Katibu wa UWT Kata Shaina ally ambaye hata CCM imeshidnwa kumsaidai lakini kamanda huyo amewasaidia bila ubaguzi,huku watu wanasema Chaadema wanaubaguzi.
Kwa kweli kwa taarifa nilizongumza na wananchi wa eneo la Kata ya Kigonigoni kijana Kileo amefanya kazi kubwa na akiendelea na moto huo kwa kuwa karibu na wananchi maana wananchi wengine wanasema tangu wamemchangua hajawahi kumuona.
ndo hilo tu waungwana...
Nikweli nilikuwa na ziara ndefu Mwanga kwaajili ya kutoa mkono wa pole kwa wahanga wa mafuriko kwenye kata ya Jipe, Ukiachilia mbali uharibifu huwo, vile vile nilikuwa nimeenda kujionea kero za wananchi jinsi wanavyonyanyaswa na askari wakenya wakati wakifanya uvuvi kwenye ziwa jipe.
Wakazi wa kata hiyo wanailalamikia serikali kushindwa kuwalinda na kuonyesha mpaka sahihi wa uvuaji wa samaki kiasi kinachopelekea kushikwa mara kwa mara na askari wa kenya na kufungwa kifungo cha miezi 6 huko kenya na wakati mwingine askari wa kenya huvuka upande wa Tanzania wakiwa na watanzania na kwenda majumbani mwao kuchukua rushwa kisha kuwaachia huku tukisema nchi ipo salaama. Mzee mmoja ajulikanaye kwa jina la Ramadhani saidi mafuti alikamatwa na askari wa kenya na kuja nyumbani kwake kuchukua fedha kiasi cha shilingi laki mbili na kuwa patia askari hawo, miezi michache baadae mzee huyo alikufa kwa kuuwawa na tembo. Wakazi hawo vile vile wanailalamikia Tanapa kushindwa kuwalipa fidia zao baada ya mazao yao kuharibiwa na tembo na Tanapa kusema itawalipa gharama zao ila mpaka sasa hamna kitu.
Wananchi kiukweli wamekata tamaa kwani hawana kiongozi wa kushughulikia kero zao japokuwa wamewachagua viongozi hawo. Mmoja wa wahanga alikuwa ni mwenyekiti wa UWT kata ya kigonigoni, Neno laki" nimeamini ccm inatutumia kipindi cha uchaguzi na uchaguzi ukiisha hatuna thamani tena. Hayo ni maneno ya mama huyo. Kiuweli watu walifarijika sana kwani hawakutegemea kuwa tungeweza kuweka tofauti ya vyama pembeni na kusimama kama watanzania.
Nitaendelea kushughulikia matatizo ya wakazi wa mwanga kwa kupitia kambi yetu Rasmi ya upinzani bungeni....
Mkuu Kileo,Nimefurahi sana kusikia habari hizi njema..Ebana wilayani kwetu mwanga kuna shida sana ya hamasa kwa vyama vya upinzani.2010 alisimama mgombea wa CDM Ila hakusikika kabisa na wala hakuweza kuleta upinzani wowote!! SO SAD..
Nikushauri kitu kimoja,HAKIKISHA UNAPITA TARAFA ZA UGWENO,USANGI NA MWANGA KUNGALI MAPEMA....FANYA KILA JITIHADA WANANCHI WAKUFAHAMU KATIKA MAENEO YOTE HAYO KABLA YA UCHAGUZI..UKIFANYA HIVI,BASI 2015 UNAWEZA KUPATA NAFASI YA KUWATUMIKIA WANANCHI..
KUMBUKA 2015 UNAWEZA KUPAMBANA NA MAGHEMBE AU TADAYO,HIVYO SIO KAZI RAHISI SANA KUWANG'OA HAWA NA HASA UKIZINGATIA UPINZANI KTKA WILAYA YA MWANGA NI MDOGO SANA..
PIA OMBA COMPANY TOKA KWA WABUNGE WENGINE WA CDM KAMA LEMA NA NASARY MPITE KILA KONA MUHAKIKISHE NMAING'OA CCM TOKA NGAZI YA CHINI..
NI HAYO TU MKUU... Its me,Raia Toka Ugweno!!