Mafuta ya taa (kerosene)

kipara kipya

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2016
Posts
20,142
Reaction score
24,432
Mafuta ya taa ni nishati inayotumika katika matumizi ya vitu mbali mbali,lakini jina lake maarufu limebaki kuwa mafuta ya taa, swali ni nani alitunga hilo jina na kwanini yawe ni mafuta ya taa tu,wakati yanatumika kwenye vitu vingine zaidi ya taa!

Kuuliza si ujinga!
 
wakikupa jibu,then pia watuambie kwanini vituo vya kuuzia nishati za hayo mafuta vinaitwa sheli?
Shell ilikuwa ni moja ya kampuni za awali kufanya biashara ya kuleta nchini na kuuza mafuta katika nchi yetu kipindi cha nyuma.

Ndio maana wengi walipoliona jina la hiyo kampuni katika vituo vya kuuzia mafuta wakita hili jina la Sheli.
 
Kumbuka vipindi vya zamani watu walitumia zaidi nishati ya kuni na mkaa kidogo hasa mijini.
Mafuta haya yalitumika zaidi kwenye taa, ndipo lilipoanzia hili jina
 
wakikupa jibu,then pia watuambie kwanini vituo vya kuuzia nishati za hayo mafuta vinaitwa sheli?
Kampuni ya shell ni miongoni mwa makampuni ya kwanza kutoa huduma, ndipo yakawa mapokeo kwa vituo hivi kuitwa sheli.
Mfano watu wengi wa Arusha wanaita maduka makubwa ya kisasa (supermarket) wao wamezoea kuita SHOPRITE, hii inatokana na iliyokuwepo kampuni hii ya shoprite na kujizoelea umaarufu hadi kusababisha na wakazi kuyaita maduka kama hayo jina hilo
 
Kumbuka vipindi vya zamani watu walitumia zaidi nishati ya kuni na mkaa kidogo hasa mijini.
Mafuta haya yalitumika zaidi kwenye taa, ndipo lilipoanzia hili jina
Swadaktaaaa nakumbuka enzi zile mwanzoni mwa miaka ya 90 nikiwa kijijini kule basi mafuta ya taa ndio ilikua bidhaa muhimu sana pindi ifikapo usiku tunawasha koroboi zetu basi tunafanya yetu mpaka mida ya kulala, so hii ni sababu yakaitwa mafuta ya taa

Daaah ila binadamu tunatokea mbali aiseeee
 
Koroboi, Chemli na Karabai hizo ndizo taa zitumiazo mafuta hayo kabla umeme na solar havija enea
 
Sie bado tunayatumia huku kwetu Dar maeneo ya Tandale kuuzia miguu ya kuku na filigisi usiku...
 
Nilijua utazungumzia jinsi yalivyopanda bei kwa sababu ya kuzuia uchakachuaji! na labda ungeshauri yashushwe maana kwa sasa ubabaishaji umepungua kidogo.
 
Utakuwa Umeishi Mjini umeme umeukuta siye wengine Tulioishi Umeme ukatukuta Tunaelewa kuwa yanaitwa Hivyobkwa sababu yalikuwa yanatumika kwenye Taa za Chemli unaweka Mafuta Ili Uweze kuona
 
Yaliitwa mafuta ya taa (tar) kwa sababu yalitengenezwa kutokana na maligafi inayoitwa tar ama kwa neno jingine asphalt
 
Sie bado tunayatumia huku kwetu Dar maeneo ya Tandale kuuzia miguu ya kuku na filigisi usiku...
ha ahahahahah ndio maana asubuhi mama muuza filigisi huwa anaamka nostrills nyeusi tii kama exhaust ya gari la mashindano sababu ya hizo koroboi...
 
Utakuwa Umeishi Mjini umeme umeukuta siye wengine Tulioishi Umeme ukatukuta Tunaelewa kuwa yanaitwa Hivyobkwa sababu yalikuwa yanatumika kwenye Taa za Chemli unaweka Mafuta Ili Uweze kuona
Mkuu kijijini nakumbuka kila ikifika jioni kuna mzee alikua akipita na baiskeli ya huku akitangaza ya umemeee tunatoka na koroboi!
 
wakikupa jibu,then pia watuambie kwanini vituo vya kuuzia nishati za hayo mafuta vinaitwa sheli?
SHELL ilikuwa kampuni kubwa ya kuuza mafuta kama ilivyokua Total, esso, CALTEX, Agip, BP nk. SHELL ilipigwa marufuku pamoja na kampuni zake tanzu kuendesha biashara Tanzania, baada ya wamiliki wa kampuni hiyo kujihusisha na siasa za Zimbabwe. walimuunga mkono Ian Smith.Simith, mzungu aliyekuwa na uraia wa Zimbabwe, zamani ikiitwa Rhodesia. Smith alipewa madaraka kinafiki na Uingereza ili kuwatuliza wapigania Uhuru wa nchi hiyo wakiongozwa na ZANU PF. Tanzania iliyokuwa mwenyekiti wa nchi zilizo mstari wa mbele kwenye ukombozi wa nchi za kuzini mwa Afrika zilimkataa Ian Smith na hivyo SHELL ikatimuliwa Tanzania. Kwakuwa ilikuwa na vituo vingi vya kuuzia nishati hiyo jina lake bado linatamba. SHELL walikuwa wanatumia logo hii hapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…