MEA-MTWARO
Senior Member
- May 15, 2013
- 128
- 40
Kwanza napenda ifahamike kuwa, sijashurutishwa wala kushawishiwa na mtu yeyote kuandika haya ninayoandika bali natumia haki yangu ya kikatiba katika ibara ya 18(a) ambayo inaniruhusu kutoa mawazo yangu katika msuala mbalimbali.
Kwamba, takribani miezi minne sasa kuna neno limeanza kutumika ambalo kwa taathira yake linahisisha watu wanaomuunga mkono mmoja wa wagombea Uraisi kupitia vyama vinavyounda UKAWA. Neno hilo ni MAFURIKO, wakimaanisha umati wa watu katika mikotano ya kampeni ya Lowasa.
Wafuasi wa Lowasa na hata viongozi wa UKAWA, wamekuwa wakitumia mafuriko hayo kujithibitishia ushindi kuelekea Oktoba 25 huku wakisahau kuwaweka watu hao katika katogoria na/au kusahau hali ilikuwaje mwaka 2010.
Katika kuweka kumbukumbu sawa, mwaka 2010; mgombea Uraisi kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Slaa alionekana kuwa na mvuto mkubwa kuliko Raisi Kikwete na kwamba mahudhurio ya watu katika mikutano ya Slaa ilikuwa ni mara dufu ya ile ya Kikwete, hata hivyo Kikwete alishinda tena kwa 61%
Kwahiyo, ndio kusema kuwa, hatupati ushindi kwa kuwaangalia mafuriko ya watu mikutanoni kwa maana watu huenda mikutanoni kwa mambo tofauti.
Kwamba, mwaka ule 2010, watu wengi walihudhuria mikutano ya Slaa kwasababu kuu mbili. Mosi walienda mikutanoni kumshuhudia mtu shujaa aliyethubutu kuwataja wezi pale Mwembe Yanga mwezi sept. 2007 bila woga wowote. Pili watu walienda kumshuhudia mbunge machachali aliyelichachafya bunge la jamhuri tangu mwaka 1995. Watu hao waliyenda huku wakiwa na misimamo yao tayari. Hawakubadilika na hatimaye CCM ikashinda.
Mwaka huu 2015, watu wanafurika kwa mambo makuu matano:
1: Kwa mara ya kwanza katika historia ya Dunia; mawaziri wakuu wawili waliosimamia utekelezaji wa miradi na shughuli zote za serikali kwa miaka 13, waliokua na kulelewa na chama tawala; kufanya siasa za upinzani. Hii ina mvuto wake tena hasa pale mawaziri hao wanapohubiri kuwa, ccm haijafanya chochote kwa zaidi ya miaka 50 ilihali wao wenyewe walikuwa wanaserikali kupitia ccm hiyo hiyo. Hii inawafanya watu waende kuwashuhudia watu hao.
2. Watu wanafurika ili wakajihakikishie wenyewe kuwa, eti chama kilichojipatia umaarufu kwa kunadi wizi wa Lowasa; leo kinamsimamisha Lowasa yule yule kugombea Urais. Hii ina mvuto sana. Watu wanafurika kwa sababu hawaamini yanayotokea.
3. Wanafurika kwa sababu ta Helikopita. Wakati fulani nilikuwa huko Mtwara, wilayani tandahimba. Watu walifurika sana sana ila karibu nusu ya mafuriko yale hayakumsikiliza Lowasa wala Sumaye. Bali yalikuwa buzy kushangaa Helikopita.
4. Kujionea afya ya Lowassa. Vyombo vya habari vimekuwa vikiielzea afya ya Lowasa kwa namna tofauti. Hivyo, wanafurika ili kujishuhudia wenyewe.
5. Nikiwa huko Tandahimba nilishuhudia malori, mabasi, maguta, daladala, bodaboda zikiwabeba watu kuwaleta uwanjani Matogoro ambapo Lowassa alihutubia.
Nihitimishe kuwa, nikiwa katika mkutano huo, niliwatafiti baadhi ya wahudhuriaji endapo watampa kura Lowasa au Magufuli. Kati ya watu kumi, 7 walikanusha kumpigia Lowasa ingawa niliwaona wakimshangilia Lowasa. Mpaka sasa sijaelewa kuwa walinidanganya ama walimdhihaki Lowasa kwa kumshangilia. Jibu ni 25 Oktoba.
Kwamba, tofauti ya watu wa Magufuli; nilitathmini katika moja ya mikutano yake na kubaini kuwa 88% ya wahudhuriaji watampugia kura kwani wengi wao wanakuwa ni CCM ni kwasababu ukawa wengi hawaendi kwa magufuli wakiamini kuwa ni walewale tofauti na lowassa ambaye anapata wafuasi wa ccm kwenye mikutano yake
Kwamba, takribani miezi minne sasa kuna neno limeanza kutumika ambalo kwa taathira yake linahisisha watu wanaomuunga mkono mmoja wa wagombea Uraisi kupitia vyama vinavyounda UKAWA. Neno hilo ni MAFURIKO, wakimaanisha umati wa watu katika mikotano ya kampeni ya Lowasa.
Wafuasi wa Lowasa na hata viongozi wa UKAWA, wamekuwa wakitumia mafuriko hayo kujithibitishia ushindi kuelekea Oktoba 25 huku wakisahau kuwaweka watu hao katika katogoria na/au kusahau hali ilikuwaje mwaka 2010.
Katika kuweka kumbukumbu sawa, mwaka 2010; mgombea Uraisi kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Slaa alionekana kuwa na mvuto mkubwa kuliko Raisi Kikwete na kwamba mahudhurio ya watu katika mikutano ya Slaa ilikuwa ni mara dufu ya ile ya Kikwete, hata hivyo Kikwete alishinda tena kwa 61%
Kwahiyo, ndio kusema kuwa, hatupati ushindi kwa kuwaangalia mafuriko ya watu mikutanoni kwa maana watu huenda mikutanoni kwa mambo tofauti.
Kwamba, mwaka ule 2010, watu wengi walihudhuria mikutano ya Slaa kwasababu kuu mbili. Mosi walienda mikutanoni kumshuhudia mtu shujaa aliyethubutu kuwataja wezi pale Mwembe Yanga mwezi sept. 2007 bila woga wowote. Pili watu walienda kumshuhudia mbunge machachali aliyelichachafya bunge la jamhuri tangu mwaka 1995. Watu hao waliyenda huku wakiwa na misimamo yao tayari. Hawakubadilika na hatimaye CCM ikashinda.
Mwaka huu 2015, watu wanafurika kwa mambo makuu matano:
1: Kwa mara ya kwanza katika historia ya Dunia; mawaziri wakuu wawili waliosimamia utekelezaji wa miradi na shughuli zote za serikali kwa miaka 13, waliokua na kulelewa na chama tawala; kufanya siasa za upinzani. Hii ina mvuto wake tena hasa pale mawaziri hao wanapohubiri kuwa, ccm haijafanya chochote kwa zaidi ya miaka 50 ilihali wao wenyewe walikuwa wanaserikali kupitia ccm hiyo hiyo. Hii inawafanya watu waende kuwashuhudia watu hao.
2. Watu wanafurika ili wakajihakikishie wenyewe kuwa, eti chama kilichojipatia umaarufu kwa kunadi wizi wa Lowasa; leo kinamsimamisha Lowasa yule yule kugombea Urais. Hii ina mvuto sana. Watu wanafurika kwa sababu hawaamini yanayotokea.
3. Wanafurika kwa sababu ta Helikopita. Wakati fulani nilikuwa huko Mtwara, wilayani tandahimba. Watu walifurika sana sana ila karibu nusu ya mafuriko yale hayakumsikiliza Lowasa wala Sumaye. Bali yalikuwa buzy kushangaa Helikopita.
4. Kujionea afya ya Lowassa. Vyombo vya habari vimekuwa vikiielzea afya ya Lowasa kwa namna tofauti. Hivyo, wanafurika ili kujishuhudia wenyewe.
5. Nikiwa huko Tandahimba nilishuhudia malori, mabasi, maguta, daladala, bodaboda zikiwabeba watu kuwaleta uwanjani Matogoro ambapo Lowassa alihutubia.
Nihitimishe kuwa, nikiwa katika mkutano huo, niliwatafiti baadhi ya wahudhuriaji endapo watampa kura Lowasa au Magufuli. Kati ya watu kumi, 7 walikanusha kumpigia Lowasa ingawa niliwaona wakimshangilia Lowasa. Mpaka sasa sijaelewa kuwa walinidanganya ama walimdhihaki Lowasa kwa kumshangilia. Jibu ni 25 Oktoba.
Kwamba, tofauti ya watu wa Magufuli; nilitathmini katika moja ya mikutano yake na kubaini kuwa 88% ya wahudhuriaji watampugia kura kwani wengi wao wanakuwa ni CCM ni kwasababu ukawa wengi hawaendi kwa magufuli wakiamini kuwa ni walewale tofauti na lowassa ambaye anapata wafuasi wa ccm kwenye mikutano yake