Mafunzo ya mgambo na ajira ya malipo madogo

Mafunzo ya mgambo na ajira ya malipo madogo

sulai

Member
Joined
Jan 11, 2017
Posts
58
Reaction score
32
Hivi kwanini Serikali huwa wanapotezea sana askari mgambo katika upatikanaji wa ajira serikalini?

Unakuta kijana amefanya mafunzo ya mgambo tena kwa uzalendo wake kabisa lakini ajira zinapotoka za vyombo vya ulinzi wanawapatia vijana wa JKT tu lakini waliopitia mafunzo ya mgambo huwa hata hawawaomei huruma kwamba nao hawa ni vijana wa kitanzania na ni wazalendo lakini hawapatiwi ajira kama zinapotokea hadi labda kwa amri ya amiri jeshi mkuu (Rais).

Sasa huwa najiuliza kuna umuhimu gani wa kuendelea kutoa mafunzo hayo wakati ajira zinapendelea upande mmoja tu? Je, hili suala Chief wa Mgambo huwa halioni?

Kuna vijana wengi waliopitia mgambo na wana sifa nzuri umri sahihi wa kupata ajira katika vyombo vya ulinzi na usalama lakini wanawapotezea tu, hebu tunaomba Serikali itukumbuke na sisi wanamgambo pia tuna mchango pia katika taifa hili japo huwa hatusikilizwi na wakati mwingine huwa hata kombati zenyewe huwa tunajinunulia sijui ni kwanini
 
Sijui kama umefikiria mara mbili mbili kabla ya kuja kulalamika humu. Ivi unajua utofauti wa mafunzo ya JKT hasa kujitolea na ya mgambo?
 
Kama umepitia mafunzo ya mgambo ni sifa ya ziada na inayokupa kipaumbele kuchaguliwa kujiunga na JKT kwahiyo usikate tamaa nenda kajiunge JKT
 
Sijui kama umefikiria mara mbili mbili kabla ya kuja kulalamika humu. Ivi unajua utofauti wa mafunzo ya JKT hasa kujitolea na ya mgambo?
umeelewa mada ya mtoa uzi
 
umeelewa mada ya mtoa uzi
Anaongelea pale zinapotokea nafasi za ajira kwa nini mgambo wanabaguliwa badala yake kipaumbele wanapewa waliopitia JKT tu..! Anashindwa kutofautisha kwamba hizo ni kozi mbili tofauti.
 
Anaongelea pale zinapotokea nafasi za ajira kwa nini mgambo wanabaguliwa badala yake kipaumbele wanapewa waliopitia JKT tu..! Anashindwa kutofautisha kwamba hizo ni kozi mbili tofauti.
narudia tena umemuelewa mtoa mada?
 
Mgambo ni geshi la akiba na sikuzote akiba haiozi na ikioza hainuki.....hapo kwenye geshi msinisahihishe tafadhali
 
Sijui kama umefikiria mara mbili mbili kabla ya kuja kulalamika humu. Ivi unajua utofauti wa mafunzo ya JKT hasa kujitolea na ya mgambo?
Hebu tupe hiyo shule, kama nawe upo vizuri!
 
Sijui kama umefikiria mara mbili mbili kabla ya kuja kulalamika humu. Ivi unajua utofauti wa mafunzo ya JKT hasa kujitolea na ya mgambo?
mafunzo ya jkt na ya mgambo yakoje utafauti? ikiwa we mwenyewe sheria haisemi kule unapokwenda kujitolea sio kama utapewa ajira hapana ata form za jkt hazina sehemu ya kusema kama ukimaliza mafunzo ni kwamba eti utaajiriwa sio kweli alafu kuhusu mafunzo wote tunapewa na jwtz sasa tafauti iko wapi?
 
Mtoa mada elewa tu hili, Maisha hayapo fair, hao watu waliopitia mafunzo ya jkt nao wanalalamika hivyohivyo, so jaribu kujitengenezea mazingira wewe pasipo kumuangushia yeyote lawama. Una ujuzi fulani, tafuta namna ya kuigeuza kuwa fursa kwako uishi maisha ya ndoto yako kwasababu usipojipangia maisha yako, kuna mwingine atakuja kukupangia.

Chagua moja, kupanga au kupangiwa.
 
Back
Top Bottom