mzamifu
JF-Expert Member
- Mar 10, 2010
- 6,410
- 3,876
Wanajamvi nawasalimu na kuwaomba tujipongeze kwa kuingia mwaka mpya wa 2015.
Napenda kushauri tu kuwa mafunzo ya kijeshi yanayotolewa kwa mujibu wa sheria yazingatie mahitaji ya sasa.
Wakati yalipoanzishwa miaka ya 1960 vijana waliojiunga na mafunzo hayo walikuwa na uhakika wa kupata ajira mara baada ya kuhitimu. Kwa sababu hii wengi walihesabiwa kama waajiriwa tayari na sehemu ya mishahara yao ilikwenda serikalini na wao kupewa posho tu.
Hakuna aliyepita JKT halafu akakosa ajira labda akatae mwenyewe.
Wakati wa sasa vijana wanajuinga wanapomaliza kidato cha sita huku wakiwa hawana hata hakika ya kupata mkopo kwa masomo ya juu sembuse kuajiriwa!
Ni hatari kwa kijana aliyepata mbinu za kijeshi halafu hana hakika na hatima ya maisha yake. wanaweza kuongeza idadi ya mapanya road!
Kwa hivo ni lazima mafunzo haya yabadilike. makambi yote yageuzwe vyuo vya kutengeneza watanzania wa karne hii. masomo muhimu yawe ni ujasiria mali, uzalendo, ulinzi wa taifa, na ukakamavu. Mapinduzi ya sayansi na Teknolojia yanaweza kuaanzia katika jeshi.
Mfano ni kituo cha Nasa cha marekani.
Napenda kushauri tu kuwa mafunzo ya kijeshi yanayotolewa kwa mujibu wa sheria yazingatie mahitaji ya sasa.
Wakati yalipoanzishwa miaka ya 1960 vijana waliojiunga na mafunzo hayo walikuwa na uhakika wa kupata ajira mara baada ya kuhitimu. Kwa sababu hii wengi walihesabiwa kama waajiriwa tayari na sehemu ya mishahara yao ilikwenda serikalini na wao kupewa posho tu.
Hakuna aliyepita JKT halafu akakosa ajira labda akatae mwenyewe.
Wakati wa sasa vijana wanajuinga wanapomaliza kidato cha sita huku wakiwa hawana hata hakika ya kupata mkopo kwa masomo ya juu sembuse kuajiriwa!
Ni hatari kwa kijana aliyepata mbinu za kijeshi halafu hana hakika na hatima ya maisha yake. wanaweza kuongeza idadi ya mapanya road!
Kwa hivo ni lazima mafunzo haya yabadilike. makambi yote yageuzwe vyuo vya kutengeneza watanzania wa karne hii. masomo muhimu yawe ni ujasiria mali, uzalendo, ulinzi wa taifa, na ukakamavu. Mapinduzi ya sayansi na Teknolojia yanaweza kuaanzia katika jeshi.
Mfano ni kituo cha Nasa cha marekani.