Maendeleo Arusha mjini

kaluu

Member
Oct 5, 2011
17
1
Kwa ninavyo fahamu mimi Mbunge ni chachu kubwa ya maendeleo katika jimbo husika hivyo tunatarajia mabadiliko makubwa kutoka kwa mh Godbless Lema walao kupambana kero ndogo ndogo zikiwemo barabara za mitaa kama makao mapya kaloleni na sehemu nyinginezo ikiwemo mjini kati. Pia kero za msongamano wa wamama wauza mboga soko kuu na Kilombero.

Mh mbunge anaziona au ni hatua gani anategemea kuzichukua kwani kwa upeo wangu nafikiri kero ndogo kama hizi mbunge kwa jitihada zake binafsi anaweza kuzitatua kwa kushirikiana na wananchi bila kuisubiri serikali.

Ushauri wa bure:

Nikiwa kama mdau wa chama hiki anachowakilisha Mh Lema nisingependa kuona mategemeo ya wananchi kuondolewa kero ndogo ndogo kama hizi yanakwama kwa kuisubiri serikali ambayo kimsingi ni wapinzani wetu hivyo nategemea mh. mbunge uchukue hatua za makusudi kutatua kero hizi na kuachana na kupoteza mda mwingi kwenye malumbano na badala yake tengeneza njia mbalimbali za kupambana na kero hizo.

Naomba kuwasilisha
 
Ushauri mzuri, ila kumbuka malumbano yanaletwa na walioshika madaraka,kama mdau unaweza kumwandikia ushauri wako kwenye mail yake au kwa maandishi na kupost kwenye ofisi ya jimbo nadhana utamfikia na kufanyiwa kazi,hapa jamvini tegemea mixed approaches ambazo wanazotoa hata Arusha pengine hawajui kuna kero gani.
 
Back
Top Bottom