Madhila ya Barabara Rusahunga -Rusumo

Madhila ya Barabara Rusahunga -Rusumo

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
34,776
Reaction score
46,050
Kipande hiki cha barabara yapata 90km katika barabara kuu iendayo Burundi, Rwanda na DRC kimepigiwa kelele kwa muda mrefu.

Kwa sasa pana sehemu mbili Nyamalagala na Ngazi Saba njia haipitiki na hali inazidi kuwa mbaya zaidi. Misururu ya magari ni mirefu na hakuna natumaini ya ufumbuzi wowote.

Ajali katika maeneo haya ni jambo la kawaida. Ajali zote katika sehemu hizi ikiwa ni matokeo ya ubovu huu mkubwa wa barabara.

Kwa hakika barabara hii ni hatari kabisa kwa matumizi ya binadamu. Ni afadhali ingalifungwa tu likaeleweka kuwa haipo.

Wahusika wote katika wilaya za Biharamulo na Ngara bora wangeachia nyadhifa zao ilo kujisafisha kama hawana namna ya kufanya kuiachia hali kufikia hapa.

Vinginevyo hawa hawafai labda hata heri ya wale wa Rufiji waliotumbuliwa juzi.

Katika picha ni hali ya Barabara hii kama ilivyo leo:



Screenshot_20200802-182137.png


IMG_20200802_100856.jpg


IMG_20200802_124938.jpg


Screenshot_20200802-181339.png




Screenshot_20200802-181451.png

Screenshot_20200802-181442.png

Screenshot_20200802-181339.png




NB: Picha zaidi zaja
Screenshot_20200802-181442.png
Screenshot_20200802-181324.png
 
Achilia mbali upepo wa siasa ulivyo hivi sasa. Kwa hali ilivyo kwenye hicho kipande sijui nani pande za huko ataelewa pana miundo mbinu imejengwa wapi au ndege gani zimenunuliwa.

Kama wajumbe ilivyo kuwa kwa watia nia. Oktoba ndiyo hiyo inajongea.

IMG_20200804_183306_204.jpg


Yawezekana ni sabotage kutokea kwa wahusika. Hata kuziba mashimo hakuna?!

Yetu macho.
 
Photoshop

Photoshop?!

Itakuwa ni Kuwa cheza shere watu wa huko. Usisahau Oct 2020 ndiyo hiyo.

Nita upload videos pia.

Tanroads, wahusika wote na yeyote aliye wahi kupita huku atakushangaa.

Chini hapa ni nyuzi za nyuma kuhusu barabara hii.

Hiyo ndiyo awamu ya tano:

TANROADS Biharamulo, Ngara wanadunda TARURA Arusha kama vile


Barabara ya Rusahunga - Rusumo ifungeni tu ieleweke


Zipo nyuzi lukuki kuhusiana na barabara hii.

Tembea uone usingoje kuambiwa.

My take: inaweza kuwa ni sabotage (deliberate)!
 
hiyo road ni dhahma tupu..waziri wa mambo ya usafirishaji sijui anasubiri kupigiwa simu na mkuu?
 
Mkuu hizi picha za hii barabara mbona kama umeleta nzuri? Kusema ukweli hii barabara ni mbovu tena mbovu haswa, tena usiombe ukapita na gari ndogo utajuta. Mara ya kwanza napita hii njia niliuliza wenyeji ni kwa nini hii barabara ni mbovu hivi inamaana wahusika hawaoni? Nikajibiwa na raia tu ambaye naye sikuweza kumwamini sana eti kuwa hi barabara ni yakimataifa hivyo hizi nchi tatu yaani Rwanda, Tz na Burundi zinategeana.

Ubovu wa miundombinu unachelewesha sana maendeleo na ndio husababisha gharama za maisha kupanda, leo hii kutoka Ngara to Mwanza gari zipo mbili tu na zinaondoka asubuhi, kutoka Ngara mjini kwenda Rusumo unapaswa uzungukie Benaco. Ile njia ya mkato mto umejaa hivyo magari hayapiti maana kivuko hakifanyi kazi.

Gari zinazofanya safari kutoka Ngara mjini na viunga vyake ni kama tax hakuna daladala na watu hujazwa kweli bila kuzingatia usalama. Kwa kuwa gari ni ndogi hivyo nauli huwa kubwa.

Pamoja na yote hayo pia niipongeze TARURA Ngara kwa kweli wanarekebisha sana barabara hasa kwa kiwango cha Lami, Zege na Changarawe.
 
Mkuu hizi picha za hii barabara mbona kama umeleta nzuri? Kusema ukweli hii barabara ni mbovu tena mbovu haswa, tena usiombe ukapita na gari ndogo utajuta. Mara ya kwanza napita hii njia niliuliza wenyeji ni kwa nini hii barabara ni mbovu hivi inamaana wahusika hawaoni? Nikajibiwa na raia tu ambaye naye sikuweza kumwamini sana eti kuwa hi barabara ni yakimataifa hivyo hizi nchi tatu yaani Rwanda, Tz na Burundi zinategeana.

Ubovu wa miundombinu unachelewesha sana maendeleo na ndio husababisha gharama za maisha kupanda, leo hii kutoka Ngara to Mwanza gari zipo mbili tu na zinaondoka asubuhi, kutoka Ngara mjini kwenda Rusumo unapaswa uzungukie Benaco. Ile njia ya mkato mto umejaa hivyo magari hayapiti maana kivuko hakifanyi kazi.

Gari zinazofanya safari kutoka Ngara mjini na viunga vyake ni kama tax hakuna daladala na watu hujazwa kweli bila kuzingatia usalama. Kwa kuwa gari ni ndogi hivyo nauli huwa kubwa.

Pamoja na yote hayo pia niipongeze TARURA Ngara kwa kweli wanarekebisha sana barabara hasa kwa kiwango cha Lami, Zege na Changarawe.

Picha hizi ni amateur siyo professional. Zinapigwa na watu safarini na penye sehemu zilizofunga na ajali peke yake.

I wish a professional akatembelea huko na kuja na proper documentary.

Wapinzani kazi kwenu maana wenye nchi wameziba masikio. Haipo miundo mbinu huko.

TARURA Ngara?

Sikijui kipande kuelekea Rusumo border kipo mikononi mwa nani. TARURA au TANROADS.

Benako rusumo kumechoka kama huko kwingine hivyo hivyo.

IMG_20200804_202628_283.jpg
 
Kwanza nikupongeze kwa kuibua hiyo kero ya hiyo barabara
Pili mimi ni mtumiaji wa hiyo njia japo ni mara chache ila inakera sana.
Mbaya zaidi usiombe uipite hiyo barabara msimu wa mvua, yaani maderava wa hizo nchi hovyo sana ikiwa gari likishindwa kupanda kwenye muinuko yupo tayari kuziba njia ili mkifika mpeane company.
Sasa kimbembe ukute hajui kiswahili au umwambie ashuke umtolee hilo gari hataki. Kwa ujumla hiyo njia ni shida.
Hakuna siku utaipita hiyo njia usikute lories zimeanguka never ever mbaya zaidi ni mapori tena yakutisha ukiiacha tu Lusahunga mpaka ufike Nyakahula hadi njia panda ya kuingia Ngara au Benaco unamshukuru Mungu.
Kuna sehemu ukipata tatizo la gari mpaka usaidiwe ushakoma, center na center zipo mbali hakuna raia wanapita aah shida tupu kule.
Mi nafiki hiyo njia pa1 kuwa ni sehem ya Tz ila ishasuswa.
 
Kwanza nikupongeze kwa kuibua hiyo kero ya hiyo barabara
Pili mimi ni mtumiaji wa hiyo njia japo ni mara chache ila inakera sana.
Mbaya zaidi usiombe uipite hiyo barabara msimu wa mvua, yaani madera wa hizo nchi hovyo sana ikiwa gari kilishindwa kupanda kwenye muinuko yupo tayari kuziba njia ili mkifika mpeane company.
Sasa kimbembe ukute hajui kiswahili au umwambie ashuke umtolee hilo gari hataki. Kwa ujumla hiyo njia ni shida.
Hakuna siku utaipita hiyo njia usikute lories zimeanguka never ever mbaya zaidi ni mapori tena yakutisha ukiiacha tu Lusahunga mpaka ufike Nyakahula hadi njia panda ya kuingia Ngara au Benaco unamshukuru Mungu.
Mi nafiki hiyo njia pa1 kuwa ni sehem ya Tz ila ishasuswa.

Wapambe wao wanaita zile picha Photoshop. Wajiandae na kura za Photoshop pia.
 
Back
Top Bottom