Madereva 3 wa bodaboda wanahitajika

Jokajeusi

JF-Expert Member
Joined
Jun 1, 2018
Posts
6,336
Reaction score
10,911
Habari wakuu.

Ninapiki piki tatu, nahitaji vijana watatu waadilifu wa kuziendesha. Boxer per day 8000/=, haugue per day 7000/=
Dereve anapaswa awe mkazi wa Dar.

Dereve unapaswa ulete kila siku hesabu na ukirusha siku mbili mfululizo utanyang'anywa pikipiki.

Dereva utaacha cheti chako cha kidato cha nne/sita kama mdhamini wako upewapo pikipiki.
Maana yake kama huna cheti usijihangaishe kuomba.

Kama upo tayari njoo Pm.
 
yaani niache cheti cha shule kisa bodaboda?? je ukifa au ukikitumia wewe kwenye mambo yako itakuwaje??


Hayo maswali utayauliza ukiwa huku na si hapa. Sheria na taratibu zipo na zitazingatiwa. Karibu
 
Utakuwa na matatizo ya akili wewe,, yaani mtu akuachie cheti chake teba bora ungesema copy, ila org!! Kwa ajili ya kimkweche chako!? Unajua thamani ya cheti kweli wewe, yaani amekipata baada ya kukisotea miaka kumi naa then akuletee ufanyie ubwisi kwa kujibodaboda!! Kapime tezi Dume!!
 


karibu sana Mkuu, unaonekana umemaliza chuo juzi. Pia unaonekana huna exposure ya dunia inaendaje.
Kama haupo tayari hukuwa na sababu ya kuandika upuuzi wako. Wakati wewe unafungia vyeti vyako wenzako wanapiga hela.
 
Mzee ni mkopo ama?I mean mkataba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…