maishapopote
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 3,278
- 5,517
You are right, Nurdin ni mtoto wa Ibrahim. Mara ya mwisho huyu Nurdin alikuwa anagombana na ndugu zake kuhusiana na urithi wa mali za baba yake.
dah hii thread imenifurahisha sana,lakini nadhani hawa wa kina akasha hawakujua wadeal na watu wa aina gani,walifanya nao biashara na wakaanza kuwatishia...kweny kitabu cha 48 Rule of power,rule no 16 inasema,Knows who you dealing with...RIP Akasha family,lakini kinachonishangaza,Mafia huwa hawaui member wa familia ambae hashiriki kwenye biashara ya familia,au mwanamke,iweje watoto na mke na ndugu wauawe? eqylpz,any idea?
Niliyaona yale magari yake pale polisi Kilwa na polisi waliniambia kisa kushikwa ilikuwa ni kumnyima mfanyakazi wake pesa zake za likizo naye akawatonya polisi. Polisi waliyashika magari yake na ugumu ulikuwa ni kujua madawa yalikuwa yanabebwaje. Yale magari yalikuwa na trailer na number za nchi mbili lakini nimesahau. Trip zilikuwa ni kutoka mombsa mpaka south afrika kupitia Tanzania. Ajabu zilikuwa zikisafiri bila mzigo wowote. Mbinu waliyokuwa wanafanya ni kuweka matank mengi ya mafuta kumbe yale matank walikuwa wanajaza madawa. Polisi baada ya kutafuta kila mahali ndio wakasahangaa mbona kuna sehemu nying zimechomelewa. Kumbe wakifika south wanayakata na kurudi Kenya kuchomelea mengine wakati yale yakipakuliwa. Hilo ndilo lilifanya wakapata hayo madawa lakini haikuwa rahisi kwa sababu huyo mfanyakazi hakutoa habari kamilifu kwa polisi.
Mkuu story yako umeitia chumvi kidogo.
Ibrahim Akasha alikuwa ni supplier wa madawa kwa ndugu wawili waliokuwa wanaishi Netherlands Magdi Barsoum na Mounir Barsoum, hawa ndugu wawili wakawa wanauza madawa kwa jamaa anaitwa Sam Klepper. Ibrahim Akasha alienda Amsterdam kufuatilia malipo yake baada ya kuuza heroin na madawa mengine kwa mkopo na hakuwa amepokea malipo yoyote, alivyofika kule Magdi Barsoum aliact kama mpatanishi kati ya Akasha na mdaiwa (mafia wa kiyougoslavia). Kabla ya kwenda Amsterdam Ibrahim alianza kuwatishia hao mafia na kumteka mmoja wao hao mafia uko Mombasa na kusema hatomuachia mpaka alipwe malipo yake.
Siku aliyokumbwa na mauti alikuwa anatembea kwenye mtaa unaoitwa Bloedstraat yeye na mkewe Gazi Hayat na baadhi ya marafiki zake wa kikenya, Akasha alipigwa risasi sita na muuaji aliyekuwa kwenye pikipiki.
Sam Klepper aliuliwa miezi mitano baadaye, Magdi Barsoum alipigwa risasi 2002 na Mounir Barsoum alipigwa risasi kwenye mtaa ambao Ibrahim Akasha alipigiwa risasi mwaka 2004 style iliyotumika ni kama iliyotumika kumuua Akasha.
Tukirudi Mombasa mtoto wa Akasha, Kamaldin Akasha alipigwa risasi na kuuliwa mwaka 2002 haijulikani kama alirithi biashara za baba yake au la, kuna mwingine anaitwa Baktash Akasha kila siku yuko kwenye matatizo na sheria na kutwa kutishia tishia watu, mwaka 2011 mkewe alikutwa amekufa katika mazingira ya kutatanisha inasemekana alikuwa anajishirikisha kwenye biashara ya madawa.
Huyo Nurdin Akasha sijui alijificha wapi.
Da Wakuu mmenikumbusha mbali sana. Hivi vipi kuhusu mwanamama aliyekuwa anaitwa Simbaulanga?
Sarah Martin Simbaulanga kesi ya utakasaji wa pesa ya kwanza ambayo kwa waTz wengi kipindi kile kupitia mfululizo wa makala ktk gazeti la uhuru ilkua kama movie dah tumetoka mbali sana 30 million! Pesa mingi sana enzi hzo
Mkuu, kati ya Ibrahim Akasha na Nurdin Akasha nani hasa aliyekamatwa Tanzania? Ikiwa ni Nurdin ndiye akiyekamatwa, kuna uhusiano gani kati ya Nurdin na Ibrahim? Kwasasa kuna member yoyote wa familia ya Ibrahim Akasha anayeishi Tanzania?
dah hii thread imenifurahisha sana,lakini nadhani hawa wa kina akasha hawakujua wadeal na watu wa aina gani,walifanya nao biashara na wakaanza kuwatishia...kweny kitabu cha 48 Rule of power,rule no 16 inasema,Knows who you dealing with...RIP Akasha family,lakini kinachonishangaza,Mafia huwa hawaui member wa familia ambae hashiriki kwenye biashara ya familia,au mwanamke,iweje watoto na mke na ndugu wauawe? eqylpz,any idea?
Ina maana Sarah Simbaulanga naye alikuwa anafanya biashara ya unga? Kwasasa yuko wapi?
Hapana simbaulanga alikua mtumishi wa Benki kuu aliyelaghaiwa na mpenziwe kuiba fedha za benki kuu, baadae akakimbilia uingereza yeye pamoja na watoto wake, kosa lake kubwa lilikua kukosa viza ambapo akikamatwa uwanja wa ndege, mpenziwe alikamatwa kenya laikotorokea na kutumia fedha za wizi kununulia magari ya biashara
Hapana simbaulanga alikua mtumishi wa Benki kuu aliyelaghaiwa na mpenziwe kuiba fedha za benki kuu, baadae akakimbilia uingereza yeye pamoja na watoto wake, kosa lake kubwa lilikua kukosa viza ambapo akikamatwa uwanja wa ndege, mpenziwe alikamatwa kenya laikotorokea na kutumia fedha za wizi kununulia magari ya biashara
kumbe huu mtandao unaweza kuisha kwa kushughulikiana wao kwa wao.
siyo kwamba alikuwa mtumishi wa NBC kitengo cha pesa za kigeni?Hapana simbaulanga alikua mtumishi wa Benki kuu aliyelaghaiwa na mpenziwe kuiba fedha za benki kuu, baadae akakimbilia uingereza yeye pamoja na watoto wake, kosa lake kubwa lilikua kukosa viza ambapo akikamatwa uwanja wa ndege, mpenziwe alikamatwa kenya laikotorokea na kutumia fedha za wizi kununulia magari ya biashara
Nilhpata sikia kuwa huyo askari wa kike alitiwa kashikashi sana baadaye alijiua. Je! Hilo ni kweli?
.. mossad 11mtandao huo hauishi, akitoka huyu anaingiaaaa mwingine
Da Wakuu mmenikumbusha mbali sana. Hivi vipi kuhusu mwanamama aliyekuwa anaitwa Simbaulanga?