Madaktari walaani sakata la miili ya Bunju

Madaktari walaani sakata la miili ya Bunju

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,348
Reaction score
26,144
Chama cha Madaktari Tanzania kimelaani kitendo cha kutupwa miili ya binaadamu kilichofanywa na IMTU. Dr.Primu Saidia,Rais wa chama hicho ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam.

Dr. Saidia amesema kitendo hicho ni kinyume na taaluma ya udaktari,utu na haki za binaadamu. Amesema kitendo hicho kinatosha kabisa kuifungia taasisi iliyohusika.
=======================================================


imtu-college.jpg

CHAMA cha Madaktari Tanzania pamoja na Jamii ya Madaktari nchini Mathematical Association of Tanzania (MAT), kimeitaka Serikali kukifungia Chuo Kikuu cha Madaktari, International Medical and Tecknological University (IMTU) cha Dar es Salaam na kuwachukulia hatua wote waliohusika na sakata la utupaji wa masalia ya binadamu kwa kuwa kimekiuka sheria, taratibu, utu, maadili ya ufundishaji na taaluma ya udaktari.

Rais wa Chama Cha Madaktari Tanzania, Dkt. Primus Saidia, amekaririwa na FikraPevu Julai 23, 2014 na akisema miili na viungo vya binadamu hutumika kwa heshima kubwa kwa kufuata taratibu za kuipata, kuisafirisha, kuhifadhi, kuitumia na kusitiri mabaki baada ya matumizi hufanyika, kwa kufuata sheria, maadili na afya ya jamii, utamaduni miiko na utu kwa mwili wa binadamu na jamii husika.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Afya ya Akili katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Prakseda Swai, amesema kitendo kilichofanywa na IMTU kinaweza kuathiri wananchi kisaikolojia na kupata hisia yenye madhara kwa afya ya akili ikiwemo ndoto na msongo wa mawazo unaosababisha kumkosesha binadamu usingizi pamoja na kupoteza hamu ya kula.

Wakati huo huo...

Habari zaidi, soma=> http://www.fikrapevu.com/sakata-la-...ikifungie-chuo-cha-imtu/#sthash.0yLIht9F.dpuf
 
Kimsingi CADAVA humsaidia daktari pale mgonjwa anapojieleza tatizo lake daktari akiikumbuka ile CADAVA basi anatiririka mpaka basi! Kosa lao nikukiuka misingi na miiko ya udaktari hivyo sisi kama wadau tunaamini wamefanya makosa na adhabu yao ipo wala siyo siri tena.

Na kwa jinsi ushahidi ulivyo wa wazi haipashwi kuchukua muda wa zaidi ya siku tatu tunataka hatua kali zichukuliwe mara moja wamedhalilisha utu wa mwanadamu. Kuna watu walikuwa hawafahamu kitu kama hicho tangu wamezaliwa maana ni siri ya medical student lakini sasa imefahamika.hii haikubaliki kabisa
 
Kwa style hii inaelekea huko india miili ya watu inatupwa jalalani
 
Binafsi nilikuwa sijui jambo hili kama lipo toka nizaliwe,naanza kujenga fikra kwamba inawezekana watu wanaopotea ovyo huwa wanatumiwa na hicho chuo na kufanywa siri...,
 
Indian at large have no very low human dignity either dead or alive. It is no wonder this inhuman act has happened. The concern is who gave them permission to dispose of human body parts in such a shameful manner? Where were Tanzanians counterparts ? This is more than enough for the abuse of foreign investment
 
Back
Top Bottom