Mkuu kwa uelewa wangu
1. Kama umefikia umri wa kustaafu unatakiwa uende NSSF wakupe fomu ya madai uijaze na mwajiri wako hiyo inaitwa kukclaim mafao.utapeleka NSSF kusubiri mafao yako.Mara nyingi ni miezi 3 hadi 6 unapata haki yako kama kila kitu kipo sawa.
2. Endapo hujafikia umri wa kustaafu yaani upo chini ya miaka 55/60 na una fani au taaluma ya kuajirika basi utafungua madai ila utapewa fao la kukosa ajira ambalo ni asilimia 13 kama sikosei la mshahara wa mwisho kwa miezi 6 baada ya hapo kama utakuwa hujapata kazi tena unaweza kudai fedha iliyobaki na ukapewa.
3. Ikiwa huna taaluma ya kuajirika mf usafi,ulinzi upishi,ukuli nk fao lako linatoka mapema tu ndani ya miezi 3-6 baada ya kufungua madai.
Angalizo usiachae kazi bila kupata kazi,mtaa ni mgumu hakikisha unakwenda kuwa na kazi nyingine.
Salaam